Najiskia kuwa mnyonge, na moyo wangu umebondeka sana. Eehh Mungu nitie nguvu

Mzee wangu Ushimen Mungu akujalie upite katika hiki kipindi ambacho unapitia nimezoea kukuona mcheshi na utani mwingi sana.

ila leo unaonekana mnyonge sana ni dhahiri shahiri kweli mambo yamekuzidia...

M/Mungu akufanyie wepesi uweze kupita hapo..
Kwani kwenye vitabu vyenu Rejea Quran na Biblia ameahidi hivyo...
Katika 1 wakorintho 10:13


Na katika Quran Suratul baqara aya 286 (Quran 2:286)


Nhamala ooneee ni hakika kama aliahidi mwenyewe atatenda Hivyo bhasi amini atatenda kikubwa ni subira..

Kwa maana wanasema hakika Mungu yuko pamoja na wenye kusibiri
 
I'm so sorry brother.
Katika maisha kwa ujumla wake kila kitu kina pende mbili , upande usio mzuri na upande ulio mzuri .
Ukiweza kulifamu hilo hakuna hali yoyote itakayo kusumbumbua sana kwa vile wakati haudumu.

Kuna wakati unakuwa kwenye mazuri , huo wakati haudumu, unakuja wakati unakuwa kwenye mabaya, nao haudumu, hivyo unapokuwa kwenye wakati wowote uzingatie saa yoyote uta change kuelekea wakati wa namna nyingine.

Sote hatupendezwi na chochote kisicho tupa furaha, ndio maana huwa tunauzingatia sana wakati mbaya.

Binafsi huwa nadhani ni ile kukumbushwa nawe uwe unajali yoyote anaepitia changamoto kwa vile nawe kuna wakati utapitia changamoto na utatamani kupata hata mtu wa kukufariji.

Kwa ujumla pole ndugu, shika sana kuvumilia, jaribu pia kupuuza yale yasio na muhimu sana ambayo yaweza kuwa sababu moja wapo ya kukosa furaha, lakini pia unaweza ukafanya kitu kama kumtembelea mtu mwenye changamoto ili kumtia moyo, inaweza kuwa mfungwa gerezani, mgonjwa hospitali, ama yatima au mzee au mhitaji yoyote, au kwenda kwenye nyumba ya ibada hapo ukasali si kwa kujiombea wewe bali wengine, toa kabisa kujiombea wewe na familia bali fanya hivyo kwa wengine.
Na kuhakikisha ndugu yangu Ushimen kama ukifanya hivyo asubuhi jua halita zama kabla hujarelewa na amani, ukifanya hivyo jioni asubuhi haitafika kabla haujarelewe na furaha .

Yote ya yote Mungu asimame nawe ndugu yangu.
 
Bwana Mungu akupelekee msaada wake kutoka Patakatifu pake. Akuangazie Nuru ya uso wake na kukupa amani. Akusamehe na maovu yako yote. Kwa jina la Mwanae mpendwa Yesu Kristo naomba na kuamini.
 
Safii Sana The Best Comment Ever ❤️❤️❤️📌📌📌📌📌📌📌
 
Anza kuswali saala tano kwa siku.

Kama siyo Muislam, shahadia uanze kwenda msikitini kusali.

Hii haitaondoa mitihani ila ni njia nzuri inayoleta ustahimilivu na subra pale inapotokea tumefikiwa na majaribu. Wengi wetu tunakosa utulivu na tunaishia kujisumbua Kwa mambo ambayo tulitakiwa kuyakabidhi Kwa Mwenyezi Mungu.
 
MHU 3
Kila jambo na Wakati wake

1 Kwa kila jambo kuna majira yake,
Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.
2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa;
Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa;
3 Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza;
Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;
4 Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka;
Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza;
5Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe;
Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia;
6Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza;
Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa;
7 Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona;
Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;
8 Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia;
Wakati wa vita, na wakati wa amani.
 
Ngoja kidogo nimtie moyo Ndugu yangu Ushimen
Huku nikimfurahisha Bibie FaizaFoxy
Soma Quran sura ya 93 yote...
WADH DUH'AA


ikuupendeza Aya ya 4 ni bora Kuliko
Quran 93:4

"Na bila ya Shaka wakati ujao utakuwa Bora kwako kuliko uliotangulia "

 
Ni maumivu ya moyo mama mkwe, na kwakua limekua kubwa na hatuwezi kukibeba kama binadam basi tumemuachua Mungu
Mwisho ukubali kuwa pesa haiwezi kukupa furaha.

Mungu ni Mwaminifu kiasi cha Kuaminiwa.

Mwambie Mungu anaweza.
 
Ameein.
 
Huwa na soma post zako classmate Ushimen kimya kimya nakuona ni mmoja wa member wako very strong emotionally sijawahii kuona ukijokes kutafuta attention kiasi hiki hata mara moja...Naamini unapitiaa katika moja ya mitihani ambayo ukuitegemea katika maisha yako na unajihisi hauna majibu,

Tunaishi katika Dunia moja lakini Mungu anatupa mitihani tofauti tofauti kwa wakati tofauti na mitihani hiyo haiwezi kuwa imeishaa mpaka siku tutakayokuwa tumemaliza muda wetu wa kuwepo hapa Duniani.Ishi mkuu,tafakarii na rudi kwake YEYE atupaye mitihani hakika majibu yake utayapata na utapita kwenye mitihani hiyo...Sio rahisi,lakini ni Rahisi mno kwa wale wanaoamini and you are among of them.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…