Najiskia kuwa mnyonge, na moyo wangu umebondeka sana. Eehh Mungu nitie nguvu

Usihofu wewe simama na unayemuabudu tu yataisha sihitaji kujua ni yepi lakini hiyo ni mitihani tu, niliyopitia kuanzia November mwaka jana ni mazito mno lakini kila siku naiona nuru ikirejea na kuzidi iliyokuwepo kabla ya mapito, ndio maana nakushauri usikate tamaa, vaa furaha usoni japo moyoni una magumu yatakwisha fanya ibada hata usiku wa manane kwa imani yako nakuombea yawe mepesi pole sana mkuu
 
Kujua tatizo la mtu ili kumuingiza kwenye maombi ni bora zaidi huenda anataka kuombewa matatizo anayopitia kumbe amebaka katoto ka mtu kesi inaanza kufukuta anataka tumuombee je hiyo ni sawa? huo ni mfano tu simaanishi ndg ushimeni amebaka but ingependeza akashare mapito hayo japo kwa kuhide vipande
 
Pole sana
Nini shida??
Mmepatwa na nini??

You're in my prayers.
Mungu awavushe[emoji120][emoji120][emoji120].


Bwana awainulie Nuru za uso wake na awape Amani[emoji120]
 
Asante mtoa madam na Mimi nimepata matumaini mapya kupitia thread hii.
 
Jirani nyakati ngumu ni kwaajili ya binadamu wote, Mimi huwa nina msemo wangu kuwa hili ni langu, limenifika na linatakiwa kupita, tofauti ya anayelia na asiyelia ni imani na tumaini.

Take heart brother, Sending hugs πŸ«‚
 
Pole sana Ushimen ,, amini hili nalo litapita kadiri muda unavyosogea.. na mimi nakuweka kwenye sala zangu pia ili Mungu akufanyie njia pasipo na njia
Kwa hakika maombi yenu yamekua nguzo kubwa sana kwetu, na hakika Mungu ameonyesha utukufu wake ulivyo mkuu..πŸ™
 
Mungu akutie nguvu. cha muhimu tafuta uwe na Mungu ukiwa naye una matumaini ya kweli. katika maisha yangu pia hua napitishwa nyakati mbalimbali za huzuni na furaha pia, mapambano na mtelemko. kuna wakati unaweza kudhani Mungu kakuacha kabisa, na pengine ukaanza kuhesabu makosa yako uliyofanya kwasababu sisi sio malaika ukasema labda unapokea adhabu. katika hali hiyo hiyo, huwa nakuja kusikia uwepo wa hali ya juu ghafla, unaoashiria kabisa kwamba ni uwepo wa Mungu, ni kama anatuma malaika wake vile hata sijui, anaonyesha uwa bado yupo pamoja nawe, regardless of what. ila cha muhimu ni kwamba unatakiwa uwe umejisajili kwa Mungu, uwe wake, kama sio wake utabaki peke yako.

huwa tunawaambia watu mara nyingi waokoke, jibu wanalotujibu ni kuwa, kwani walokole huwa hawatendi dhambi? mnachotakiwa kujua ni kwamba kumwamini Yesu na kumpa maisha yake ni kama kujisajili kwake uwe mali yake na yeye awe mwokozi wako na mwombezi wako. waraka wa Yohana anasema Yesu ni mwombezi, ni kama advocate wetu, ukifanya kosa au hata kama sio kosa ukiwa unaomba anakuwa kama wakili wako mbele za Mungu Baba (kama nafsi kwasababu alishafanyika mwili na mwili ule ule ulienda mbinguni hivo yupo), shida ni kama hujampa maisha yako hawezi kuwa advocate wako. ndio utofauti wetu though haitupi tiketi ya kutenda dhambi kwa sababu neema na advocate wetu yupo.
 
I echo what everybody else has posted here. Take heart, sali na pumzika. Pole Mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…