Nakusudia kuishtaki Serikali (TCRA) kuzima Simcard za wateja wa mitandao

Nakusudia kuishtaki Serikali (TCRA) kuzima Simcard za wateja wa mitandao

Unaweza kujiuliza maswali 200,na usipate jibu hata moja juu ya taifa la Tanzania hasa watu wake.

Hivi hawa ni Binadamu kutoka sayari hii ya Dunia au ni viumbe kutoka Planet X?

Binadamu aliyekamilika ni lazima awe na kumbukumbu za kutosha juu ya kila Tukio analopitia.

Tanzania hii hakuna tena anayekumbuka juu ya vitambulisho vya kupigia kura na Driving Licence kuwa vyote vina mfumo wa Biometric (unaohifadhi alama za vidole).

95% ya Watanzania wana vitambulisho vya kupigia kura vyenye mfumo wa Biometric sawa tu na Vitambulisho vya Taifa, lakini leo hii eti hivyo Vitambulisho havitakiwi kusajilia line za simu hadi viwe Vitambulisho vya Taifa.

Eti lengo ni kudhibiti uhalifu, sasa binadamu mmoja ana fingerprints ngapi kama ID za kura ambazo pia zilipatikana kama Vitambulisho vya Taifa kwa njia hiyo hiyo ya alama za vidole leo tena havifai?

Wenye akili wameshasoma mchezo, kuna kitu kinatafutwa hapo, kwa sababu fingerprints tayari watu walishachukuliwa kwenye Vitambulisho vya kura na Driving Licence, sasa kuna haja gani ya kutesa watu kiasi hiki?

Details za kila raia na fingerprints zake zipo Tayari kupitia Vitambulisho vya kura. Taifa lenye mamilioni ya wajinga wamesahau kuwa information zao zilishachukuliwa na fingerprints pia.

Neno la Mungu katika Kitabu cha Mithali linasema "Mwanangu mtafute sana Elimu na wala Usimwache aende zake”.

Poleni Watanzania.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hili la NIDA ni upigaji wa pesa tu wameutengeneza kwa makusudi.
 
Umeandika kwenye mada yako;
''Wenye akili wameshasoma mchezo, kuna kitu kinatafutwa hapo, kwa sababu fingerprints Tayari watu walishachukuliwa kwenye Vitambulisho vya kura na Driving Licence,sasa kuna haja gani ya kutesa watu kiasi hiki?''.

Ni kitu gani kinachotafutwa? Naomba unielimishe!

Nimekuomba unielimishe kwa sababu kwa sasa hapa Jamiiforums kumejitokeza baadhi ya wanachama ambao wanadhani hisia zao ndio ukweli lakini kibaya zaidi wanataka kuwalazimisha na watu wengine kwa hoja za nguvu waamini hisia zao!
Mkuu kuna sababu gani ya kukusanya taarifa ambazo tayari unazo?. Nadhani hilo ndo swali la msingi la mleta mada.
 
My Son drink water,

Umesahau na passport, yaani mpaka hivi vidole vyangu vimeanza kufutika hizo alama kila siku wanaviramba, hata ukisafiri pia wanaramba vidole, I’m tired
Afadhali mkuu na wewe umeliona hilo, hili ni taifa la mambumbumbu kupindukia, majitu yapo tu hata kuhoji hayataki

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vitambulisho vya zamani hizo data zilikua zipo kama hardcopy, vitambulisho vya taifa wanascan kwa machine zinaingia kwenye computer, huwezi chukua karatasi za zamani za fingerprints ukaziscan, fingerprint scanner zinahitaji kidole sio karatasi.

Tatizo ni technology tu, hizo data hawana katika format inayotakiwa ndiyo maana wameamua kutengeneza mfumo moja ambao ni standard sasa hivi ambao dunia nzima wanatumia, so nenda kafanye acha lawama.
Si kweli, ndugu Yangu alipoteza voting ID akapewa mpya bila Fingerprints walichofanya ni ku retrieve tu data zake na kumpiga picha, fingerprints walikuwa nazo Tayari

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuwa na national ID ni jambo la muhimu. Tatizo NIDA inafanya kazi kimasikini sana na hawakujipanga kama serikali kwa jambo hili. Huwezi kusema Watanzania wote 18+ wawe na ID ndani ya muda mfupi huku hujawekeza vya kutosha kwenye rasilimali vifaa, ofisi na watu kwa ajili ya kazi hiyo. Ilitakiwa kila ofisi ya kijiji na mtaa pawe na kitengo cha NIDA kwa kazi hizi.
 
Unaweza kujiuliza maswali 200,na usipate jibu hata moja juu ya taifa la Tanzania hasa watu wake.

Hivi hawa ni Binadamu kutoka sayari hii ya Dunia au ni viumbe kutoka Planet X?

Binadamu aliyekamilika ni lazima awe na kumbukumbu za kutosha juu ya kila Tukio analopitia.

Tanzania hii hakuna tena anayekumbuka juu ya vitambulisho vya kupigia kura na Driving Licence kuwa vyote vina mfumo wa Biometric (unaohifadhi alama za vidole).

95% ya Watanzania wana vitambulisho vya kupigia kura vyenye mfumo wa Biometric sawa tu na Vitambulisho vya Taifa, lakini leo hii eti hivyo Vitambulisho havitakiwi kusajilia line za simu hadi viwe Vitambulisho vya Taifa.

Eti lengo ni kudhibiti uhalifu, sasa binadamu mmoja ana fingerprints ngapi kama ID za kura ambazo pia zilipatikana kama Vitambulisho vya Taifa kwa njia hiyo hiyo ya alama za vidole leo tena havifai?

Wenye akili wameshasoma mchezo, kuna kitu kinatafutwa hapo, kwa sababu fingerprints tayari watu walishachukuliwa kwenye Vitambulisho vya kura na Driving Licence, sasa kuna haja gani ya kutesa watu kiasi hiki?

Details za kila raia na fingerprints zake zipo Tayari kupitia Vitambulisho vya kura. Taifa lenye mamilioni ya wajinga wamesahau kuwa information zao zilishachukuliwa na fingerprints pia.

Neno la Mungu katika Kitabu cha Mithali linasema "Mwanangu mtafute sana Elimu na wala Usimwache aende zake”.

Poleni Watanzania.

Sent using Jamii Forums mobile app
Pia sheria ya mawasiliano uvitambua vitambulisho vinne yaani unawezasajili kupitia driving license,passport,national id au kadi ya kura na hivi vyote vina fingerprint,labda wanna lengo nyuma ya pazia.Kupitia sheria hii wanaweza wakasthakiwa kama watafungia watu Simu.
 
Wewe nawe msahaulifu mkubwa zaidi.
Umesahau wakati wa vitambulisho vya mpiga kura au leseni ya udereva hakukuwa na uhakiki/usahili wa idara ya uhamiaji kujiridhisha uraia wa muombaji.
Umesahau ktk vitambulisho vya kura hakukuwa na uwasilishaji cheti cha kuzaliwa.

Umeasahau passport za zamani ilikuwa sio lazima upeleke cheti cha kuzaliwa, kuna waliopeleka affidavit tu ambazo ni rahisi kughushi(forge), unaenda na mtu yeyote mahakamani au kwa mwanasheria unasema alikuwepo nilipozaliwa kisha unalipia stamp duty haifiki mwekundu wa msimbazi mmoja au balimi 5.
Umesahau wakati wa vitambulisho vya wapiga kura haikuwa lazima kutambuliwa nambari ya nyumba au kitalu kwa wakazi wa mijini ambako wageni ni wengi.

#Ujuaji mwingi mbele giza.
#Waacheni wenye wajibu na taaluma zao wafanye kazi zao kitaalamu, sio kila kitu siasa.
Asante sana !!! Sasa mleta mada ajipime kama anatosha kujinasibu kuwa yeye kashaitafuta elimu na kuipata ama bado anazurula na kijiba rohoni kuitafuta elimu.
 
Mchakato wa vitambulisho vya taifa ni muhimu kwa usalama wa nchi yetu, kwasasa kabla ya kutoa kitambulisho unafanyika uchunguzi tofauti na jinsi zinavyotolewa leseni za udereva na vile vya kupigia kura, wale wanaotiliwa shaka wanachunguzwa zaidi.

Ushauri.
NIDA hawatozi hela yoyote kwenye huduma yao, kwa uzoefu wangu serikalini, taasisi zinazotegemea ruzuku kwa 100% hua zinakumbana changamoto ya fedha na vitendea kazi kutokana na ukiritimba uliopo kwenye kupata fedha toka mfuko mkuu, serikali iwapatie fungu la kutosha tena kwa wakati na iwaongezee nguvu kazi.
NIDA wangeachiwa zoezi la kuprint tu id kwanza hawana elimu ya utambuzi kujua yupi raia yupi sio,jukumu la taarifa wangeachiwa polisi na uhamiaji kwani wako nchi nzima wakusanye taarifa wanazituma NIDA
 
Hili ndio jibu sahihi kwa mtoa mada
Wewe nawe msahaulifu mkubwa zaidi.
Umesahau wakati wa vitambulisho vya mpiga kura au leseni ya udereva hakukuwa na uhakiki/usahili wa idara ya uhamiaji kujiridhisha uraia wa muombaji.
Umesahau ktk vitambulisho vya kura hakukuwa na uwasilishaji cheti cha kuzaliwa.

Umeasahau passport za zamani ilikuwa sio lazima upeleke cheti cha kuzaliwa, kuna waliopeleka affidavit tu ambazo ni rahisi kughushi(forge), unaenda na mtu yeyote mahakamani au kwa mwanasheria unasema alikuwepo nilipozaliwa kisha unalipia stamp duty haifiki mwekundu wa msimbazi mmoja au balimi 5.
Umesahau wakati wa vitambulisho vya wapiga kura haikuwa lazima kutambuliwa nambari ya nyumba au kitalu kwa wakazi wa mijini ambako wageni ni wengi.

#Ujuaji mwingi mbele giza.
#Waacheni wenye wajibu na taaluma zao wafanye kazi zao kitaalamu, sio kila kitu siasa.
 
NIDA wangeachiwa zoezi la kuprint tu id kwanza hawana elimu ya utambuzi kujua yupi raia yupi sio,jukumu la taarifa wangeachiwa polisi na uhamiaji kwani wako nchi nzima wakusanye taarifa wanazituma NIDA
Ukitaka kuchunguza kwa undani uraia wa watu wote itakuchukua milele. Kinachofanywa na NIDA ni sahihi kabisa, wanafanya 'quick screening' kama taarifa zako zinaviashiria vya udanganyifu ndipo wanafanya uchunguzi zaidi, hata ukienda kuomba passport uhamiaji utaratibu ni huohuo, hawapotezi muda na mtu ambaye taarifa zake hazioneshi shaka yeyote.
 
Ok' huenda kama taifa watawala wanahitaji information zetu zifahamike, tunafanya nn? Wapi? Na nani?. Tatizo ni hiyo deadline. Why? Kwann usingetafutwa mfumo endelevu urenew kwa mfumo huo wa vidole? Kwann tukimbizane na deadline? Line mpya zingeweka na mfumo wa vidole, mtu akipoteza mfumo wa vidole utumike kurenew, mtu akihitaji msaada basi aambiwe sajili kwa mfumo kwanza ndo usaidike, taratibu mpaka wote wanasajili. Sasa speed yote ya nini?
 
Pia sheria ya mawasiliano uvitambua vitambulisho vinne yaani unawezasajili kupitia driving license,passport,national id au kadi ya kura na hivi vyote vina fingerprint,labda wanna lengo nyuma ya pazia.Kupitia sheria hii wanaweza wakasthakiwa kama watafungia watu Simu.
Hebu hii iweke vzr Mkuu

MTC | 101| [emoji769]
 
Kwanza ni kinyume cha Katiba ya uhuru wa kupata mawasiliano, pili ni uhujumu uchumi kwa serikali yenyewe na tatu kuzuia wananchi kupata habari kupitia mitandao ya kijamii. Kesi inafunguliwa jumatatu kanda ya Dar es Salaam.

Mimi sio wakili ila nimewasiliana na mawakili wangu 3 na tunakusudia kupeleka hoja za msingi mahakamani ili kuzuia watu zaidi ya milioni 24 kupoteza mawasiliano.
Utatekwa na kupotezwa ukifungua hiyo Kesi, Tuna Rais hatari sana!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo hii nchi katika taasisi nyingi za serikaki na wizara zake zinaendeshwa na watu wajinga wajinga. Mambo bado yanaendeshwa kwa kutumia mifumo ya zamani sana.

Hakuna mawasiliano mazuri wala uhifadhi wa kumbukumbu wa pamoja (central system); na ndio maana kila siku mambo yale yale yanajirudia.

Ni aibu kwa kweli.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom