My Son drink water
JF-Expert Member
- Nov 30, 2016
- 4,932
- 13,306
Jibu hoja za bandiko langu na siyo kuni attack binafsi mbumbumbu mkubwa weweMy Son drink water,
Unaendeshwa na mihemko. Punguza munkari uusome vema mchezo. Hasira zako kwa mtu mmoja zisikufanye utuandikie upupu. Kwani una bifu nasi. Mjinga mwenyewe.
Hili la NIDA ni upigaji wa pesa tu wameutengeneza kwa makusudi.Unaweza kujiuliza maswali 200,na usipate jibu hata moja juu ya taifa la Tanzania hasa watu wake.
Hivi hawa ni Binadamu kutoka sayari hii ya Dunia au ni viumbe kutoka Planet X?
Binadamu aliyekamilika ni lazima awe na kumbukumbu za kutosha juu ya kila Tukio analopitia.
Tanzania hii hakuna tena anayekumbuka juu ya vitambulisho vya kupigia kura na Driving Licence kuwa vyote vina mfumo wa Biometric (unaohifadhi alama za vidole).
95% ya Watanzania wana vitambulisho vya kupigia kura vyenye mfumo wa Biometric sawa tu na Vitambulisho vya Taifa, lakini leo hii eti hivyo Vitambulisho havitakiwi kusajilia line za simu hadi viwe Vitambulisho vya Taifa.
Eti lengo ni kudhibiti uhalifu, sasa binadamu mmoja ana fingerprints ngapi kama ID za kura ambazo pia zilipatikana kama Vitambulisho vya Taifa kwa njia hiyo hiyo ya alama za vidole leo tena havifai?
Wenye akili wameshasoma mchezo, kuna kitu kinatafutwa hapo, kwa sababu fingerprints tayari watu walishachukuliwa kwenye Vitambulisho vya kura na Driving Licence, sasa kuna haja gani ya kutesa watu kiasi hiki?
Details za kila raia na fingerprints zake zipo Tayari kupitia Vitambulisho vya kura. Taifa lenye mamilioni ya wajinga wamesahau kuwa information zao zilishachukuliwa na fingerprints pia.
Neno la Mungu katika Kitabu cha Mithali linasema "Mwanangu mtafute sana Elimu na wala Usimwache aende zake”.
Poleni Watanzania.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kuna sababu gani ya kukusanya taarifa ambazo tayari unazo?. Nadhani hilo ndo swali la msingi la mleta mada.Umeandika kwenye mada yako;
''Wenye akili wameshasoma mchezo, kuna kitu kinatafutwa hapo, kwa sababu fingerprints Tayari watu walishachukuliwa kwenye Vitambulisho vya kura na Driving Licence,sasa kuna haja gani ya kutesa watu kiasi hiki?''.
Ni kitu gani kinachotafutwa? Naomba unielimishe!
Nimekuomba unielimishe kwa sababu kwa sasa hapa Jamiiforums kumejitokeza baadhi ya wanachama ambao wanadhani hisia zao ndio ukweli lakini kibaya zaidi wanataka kuwalazimisha na watu wengine kwa hoja za nguvu waamini hisia zao!
Wewe unayejua jibu hoja zangu kwa hoja ili watu wakueleweHuyu jamaa ana mihemko ya kisiasa kiasi kwamba anaropoka mambo mengi sana hasiyo yajua.
Afadhali mkuu na wewe umeliona hilo, hili ni taifa la mambumbumbu kupindukia, majitu yapo tu hata kuhoji hayatakiMy Son drink water,
Umesahau na passport, yaani mpaka hivi vidole vyangu vimeanza kufutika hizo alama kila siku wanaviramba, hata ukisafiri pia wanaramba vidole, I’m tired
Kazi yako ni kuunga mkono hoja bila kupembua, kuna siku utakuja kuungua badala ya kuunga, sasa kwa nini Vitambulisho vya kupigia kura bado vinatumika Kama details zake hazikuwa sawa?Naunga mkono hoja
P
Si kweli, ndugu Yangu alipoteza voting ID akapewa mpya bila Fingerprints walichofanya ni ku retrieve tu data zake na kumpiga picha, fingerprints walikuwa nazo TayariVitambulisho vya zamani hizo data zilikua zipo kama hardcopy, vitambulisho vya taifa wanascan kwa machine zinaingia kwenye computer, huwezi chukua karatasi za zamani za fingerprints ukaziscan, fingerprint scanner zinahitaji kidole sio karatasi.
Tatizo ni technology tu, hizo data hawana katika format inayotakiwa ndiyo maana wameamua kutengeneza mfumo moja ambao ni standard sasa hivi ambao dunia nzima wanatumia, so nenda kafanye acha lawama.
Pia sheria ya mawasiliano uvitambua vitambulisho vinne yaani unawezasajili kupitia driving license,passport,national id au kadi ya kura na hivi vyote vina fingerprint,labda wanna lengo nyuma ya pazia.Kupitia sheria hii wanaweza wakasthakiwa kama watafungia watu Simu.Unaweza kujiuliza maswali 200,na usipate jibu hata moja juu ya taifa la Tanzania hasa watu wake.
Hivi hawa ni Binadamu kutoka sayari hii ya Dunia au ni viumbe kutoka Planet X?
Binadamu aliyekamilika ni lazima awe na kumbukumbu za kutosha juu ya kila Tukio analopitia.
Tanzania hii hakuna tena anayekumbuka juu ya vitambulisho vya kupigia kura na Driving Licence kuwa vyote vina mfumo wa Biometric (unaohifadhi alama za vidole).
95% ya Watanzania wana vitambulisho vya kupigia kura vyenye mfumo wa Biometric sawa tu na Vitambulisho vya Taifa, lakini leo hii eti hivyo Vitambulisho havitakiwi kusajilia line za simu hadi viwe Vitambulisho vya Taifa.
Eti lengo ni kudhibiti uhalifu, sasa binadamu mmoja ana fingerprints ngapi kama ID za kura ambazo pia zilipatikana kama Vitambulisho vya Taifa kwa njia hiyo hiyo ya alama za vidole leo tena havifai?
Wenye akili wameshasoma mchezo, kuna kitu kinatafutwa hapo, kwa sababu fingerprints tayari watu walishachukuliwa kwenye Vitambulisho vya kura na Driving Licence, sasa kuna haja gani ya kutesa watu kiasi hiki?
Details za kila raia na fingerprints zake zipo Tayari kupitia Vitambulisho vya kura. Taifa lenye mamilioni ya wajinga wamesahau kuwa information zao zilishachukuliwa na fingerprints pia.
Neno la Mungu katika Kitabu cha Mithali linasema "Mwanangu mtafute sana Elimu na wala Usimwache aende zake”.
Poleni Watanzania.
Sent using Jamii Forums mobile app
Asante sana !!! Sasa mleta mada ajipime kama anatosha kujinasibu kuwa yeye kashaitafuta elimu na kuipata ama bado anazurula na kijiba rohoni kuitafuta elimu.Wewe nawe msahaulifu mkubwa zaidi.
Umesahau wakati wa vitambulisho vya mpiga kura au leseni ya udereva hakukuwa na uhakiki/usahili wa idara ya uhamiaji kujiridhisha uraia wa muombaji.
Umesahau ktk vitambulisho vya kura hakukuwa na uwasilishaji cheti cha kuzaliwa.
Umeasahau passport za zamani ilikuwa sio lazima upeleke cheti cha kuzaliwa, kuna waliopeleka affidavit tu ambazo ni rahisi kughushi(forge), unaenda na mtu yeyote mahakamani au kwa mwanasheria unasema alikuwepo nilipozaliwa kisha unalipia stamp duty haifiki mwekundu wa msimbazi mmoja au balimi 5.
Umesahau wakati wa vitambulisho vya wapiga kura haikuwa lazima kutambuliwa nambari ya nyumba au kitalu kwa wakazi wa mijini ambako wageni ni wengi.
#Ujuaji mwingi mbele giza.
#Waacheni wenye wajibu na taaluma zao wafanye kazi zao kitaalamu, sio kila kitu siasa.
NIDA wangeachiwa zoezi la kuprint tu id kwanza hawana elimu ya utambuzi kujua yupi raia yupi sio,jukumu la taarifa wangeachiwa polisi na uhamiaji kwani wako nchi nzima wakusanye taarifa wanazituma NIDAMchakato wa vitambulisho vya taifa ni muhimu kwa usalama wa nchi yetu, kwasasa kabla ya kutoa kitambulisho unafanyika uchunguzi tofauti na jinsi zinavyotolewa leseni za udereva na vile vya kupigia kura, wale wanaotiliwa shaka wanachunguzwa zaidi.
Ushauri.
NIDA hawatozi hela yoyote kwenye huduma yao, kwa uzoefu wangu serikalini, taasisi zinazotegemea ruzuku kwa 100% hua zinakumbana changamoto ya fedha na vitendea kazi kutokana na ukiritimba uliopo kwenye kupata fedha toka mfuko mkuu, serikali iwapatie fungu la kutosha tena kwa wakati na iwaongezee nguvu kazi.
Wewe nawe msahaulifu mkubwa zaidi.
Umesahau wakati wa vitambulisho vya mpiga kura au leseni ya udereva hakukuwa na uhakiki/usahili wa idara ya uhamiaji kujiridhisha uraia wa muombaji.
Umesahau ktk vitambulisho vya kura hakukuwa na uwasilishaji cheti cha kuzaliwa.
Umeasahau passport za zamani ilikuwa sio lazima upeleke cheti cha kuzaliwa, kuna waliopeleka affidavit tu ambazo ni rahisi kughushi(forge), unaenda na mtu yeyote mahakamani au kwa mwanasheria unasema alikuwepo nilipozaliwa kisha unalipia stamp duty haifiki mwekundu wa msimbazi mmoja au balimi 5.
Umesahau wakati wa vitambulisho vya wapiga kura haikuwa lazima kutambuliwa nambari ya nyumba au kitalu kwa wakazi wa mijini ambako wageni ni wengi.
#Ujuaji mwingi mbele giza.
#Waacheni wenye wajibu na taaluma zao wafanye kazi zao kitaalamu, sio kila kitu siasa.
Ukitaka kuchunguza kwa undani uraia wa watu wote itakuchukua milele. Kinachofanywa na NIDA ni sahihi kabisa, wanafanya 'quick screening' kama taarifa zako zinaviashiria vya udanganyifu ndipo wanafanya uchunguzi zaidi, hata ukienda kuomba passport uhamiaji utaratibu ni huohuo, hawapotezi muda na mtu ambaye taarifa zake hazioneshi shaka yeyote.NIDA wangeachiwa zoezi la kuprint tu id kwanza hawana elimu ya utambuzi kujua yupi raia yupi sio,jukumu la taarifa wangeachiwa polisi na uhamiaji kwani wako nchi nzima wakusanye taarifa wanazituma NIDA
Hebu hii iweke vzr MkuuPia sheria ya mawasiliano uvitambua vitambulisho vinne yaani unawezasajili kupitia driving license,passport,national id au kadi ya kura na hivi vyote vina fingerprint,labda wanna lengo nyuma ya pazia.Kupitia sheria hii wanaweza wakasthakiwa kama watafungia watu Simu.
Utatekwa na kupotezwa ukifungua hiyo Kesi, Tuna Rais hatari sana!Kwanza ni kinyume cha Katiba ya uhuru wa kupata mawasiliano, pili ni uhujumu uchumi kwa serikali yenyewe na tatu kuzuia wananchi kupata habari kupitia mitandao ya kijamii. Kesi inafunguliwa jumatatu kanda ya Dar es Salaam.
Mimi sio wakili ila nimewasiliana na mawakili wangu 3 na tunakusudia kupeleka hoja za msingi mahakamani ili kuzuia watu zaidi ya milioni 24 kupoteza mawasiliano.
Soma sheria ya mawasiliano i googleHebu hii iweke vzr Mkuu
MTC | 101| [emoji769]