Namna ya kuwaona wachawi kwa kutumia Kisamvu

Namna ya kuwaona wachawi kwa kutumia Kisamvu

Duniani kuna miti mingi sana yenye nguvu za asili za miujiza

Katika miti hiyo mmoja wapo ni mti wa kisamvu

Kisamvu ni mboga, mizizi yake ni chakula na hata shina lake huweza kutumika kama kuni

Lakini siri kubwa iliyopo katika mti huu ni kuwa, majani yake yana uwezo mkubwa wa kukufanya uwaone wachawi live wakiwa kwenye kazi zao.

Kama na wewe ni mtu anayetamani sana kuwaona viumbe hawa basi fuata taratibu zifuatazo.

Sharti
1. Usiwe muoga
2. Utakapowaona usikimbie wala kuonesha mshtuko bali tulia mpaka watakapotoweka

Tahadhari

Ni vyema uwe na kinga dhidi ya nguvu zao hasi, ili pindi utakapovunja sharti lolote hapo juu usiweze kupata madhara yoyote

MAANDALIZI
~Ponda kisamvu mpaka kiive vizuri

~Kamua ili upate maji yake

~Chukua maji hayo nawa usoni huku unanuia

Ukimaliza hapo nenda sehemu ya soko ama panapokuwa na mkusanyiko mkubwa wa watu ama kasimame njia panda, pia hata ukiwa ndani umelala kama watakuja utawaona

Zingatia masharti.

Leteni mrejesho mtakao waona [emoji2][emoji2][emoji2][emoji28]
Nitafanya ili nione ulimwengu ulivyo na mambo aise na kama wanatembea uchi ndio ntaenjoy zaidi ili nione walivyoumbika
 
Unapokutana na kiumbe chochote kisicho cha kawaida hata shetani, wewe uliza WHO ARE YOU?

Kumbuka viumbe visivyo na mwili vinabeba umbo lolote kwa malengo wanayoyatarajia.

Mzee, nimekutana nao, nimeongea nao na pia nimechepushwa njia za kifo mara tatu zaidi.

Mtu anapokupa mbinu za kigiza giza ili uyaone yaliyogizani huyo anatafuta new members. Ukitaka kuyaona ya gizani just tumia light
Mkuu nimependa hii verse ya mwisho “Ukitaka kuona ya gizani just tumia light”
 
MREJESHOO....

Baada ya kusoma uzi nikaenda kwa jirabi Mama mwaju nikachuma kisamvu nikafata masharti ya Uzi pale kwenye kupata usoni sana nikaisi kama nimeweka uso kwenye ziwa la pilipili macho yaliwasha SANAAAA nkavumilia baada ya apo Uso ukawa umekakamaa vby sana nikasubr ukauke ukakauka ila bado ulkua umekakamaa 7bu kisamvu kina utomvu mzito sana.....Basi nikatoka ndani nishuhudie ao viumbe patupu nikaenda sokoni patupu nikaenda barabarani patupu nikarudi zangu kunawa uso mfyuu
 
[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2] Utarukwa na akili kwakuwa hutawaona wachawi tuu.. Utaona mpaka viumberoho wengine wenye kuogofya mno..!!!
Nknk


Sent using Jamii Forums mobile app
nahitaji hii.kitu
 
Hiki kikao cha mkoa kinakuwa kama kikao cha kamati ya ulinzi na usalama cha mkoa, RCC kinachoendeshwa na mkuu wa mkoa?
Yani unajadiliwa kimapana..na kikosi kazi cha kukushughulikia kinaundwa...na mrejesho inabidi wapeleke kwa mkuu wao kuhusu kazi waliyopewa
 
Yaani kutumia mbinu ya kuzimu kuwaona watumishi wake? Nehi

Mimi nimeona mpaka majini, mapepo na Malaika lakini sijawahi kunuizia kuwaona.

Hapa ninaishi kwa neema kwani nimeshapitia deathrow zaidi ya mara tatu na sifi.

Mungu ndiye mpango mzima
Duuh hadi malaika na mapepo [emoji23][emoji23]

Wewe kweli msanii
 
Yani unajadiliwa kimapana..na kikosi kazi cha kukushughulikia kinaundwa...na mrejesho inabidi wapeleke kwa mkuu wao kuhusu kazi waliyopewa
Nafikiri kwa sisi tunaomwamini Mungu wakikuwekea RCC yao, basi na malaika kule mbinguni wanakaa kwenye RCC.......sasa hapo ndo itajulikana kama viwavi jeshi nao wanavaa kombati au laa!
 
Mi nataka kuona wapi watu wanaficha hela ktk maeneo ninayoweza kuyafikia na kuzichukua bila Masharti.
We donlucchese kweli we si mtu, umenilazimisha kumuomba Mshana Jr msamaha baada ya kugundua kuwa nimemuona yeye na wenzake sokoni Tandale jana usiku wakiwa njiani kuelekea Mwanga (Kilimanjaro). Alikuja Mshana na wenzake wakanipiga vibao na kuniambia niache upuuzi wa kuwafuatilia. Sina hamu na kisamvu kwa kweli.
Mtakuja kufa kizembe sana [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom