Namtetea mtoto wa Simbachawene, askari wachunguzwe

Namtetea mtoto wa Simbachawene, askari wachunguzwe

Hao askari wanatakiwa washtakiwe kwa kumpiga picha bila idhini yake.
Mbona wakiwa wanapokea rushwa hawajipigi picha.
Sasa wamenipa warrant wa kuwapiga picha pindi nikiwapa buku mbili halafu narusha mtandaoni
Mimi nataka kudeal na police wanaokunywa pombe wakiwa kwenye unifomu na smg siku nikibahatika video nitaitupa hewani waone km ni mazuri
 
Alipe gari za Watu alizogonga au apelekwe court kuendesha gari akiwa amelewa na kusababisha ajali.Lakini hayo matusi ni zao la Ulevi tu siyo kwamba ndiyo tabia yake .
Element ni club kubwa ni Night club ametoka kupombeka hivyo tujue ukishalewa busara kwa Watu hupungua halafu msiunganishe Ulevi wake na malezi maana hakuna anayefundisha Mtoto wake Ulevi Ila Mtu kunywa pombe siyo kosa pia.
Ukiwa club Matusi vitu vya kawaida Sana au kipigana ndiyo maana tunaweka Mabaunsa kudhibiti Ubabe ndani ya Club.
Ondoeni hoja ya Ubaba hapo na Malezi hakuna Uhusiano Tambo baada ya kulewa kawaida tu kila Mtu akilewa anataka kuoneka Msomi na anaongea kiingereza hata Kama hajui vizuri ataropoka tu,anazo pesa ,anayo mamlaka pia.Vitu vya kawaida Sana hasa wenye tuluozoea kushinda club na kupombeka.
Jifunze tabia za Watu wakishakunywa Pombe.
Hiyo ndio hoja ya msingi.
Wakienda mahakamani hakuna uthibitisho kuwa alikuwa amelewa maana , hakuchukuliwa vipimo.

Tumekumbwa na pepo baya la kuchukia wateuliwa na Familia zao, pasipo sababu ya msingi.
Na kuhisi kuwa wao ndio waliotusababishia umaskini.
 
Kwanza nianze kwa kukiri ya kuwa pamoja ya kuwa Mimi ni mtu mzima, na mtoto wa Askari polisi aliyetukanwa sijapokea na kumsamehe Joji Simbachawene.

Siwezi msamehe Mh Waziri Simbachawene kamwe na Sitofanya hivyo maana Baba yangu mzazi amefedheheshwa sana sana sana sana mbele ya macho ya umma.

Siwezi kubali hakika ya kuwa Baba yangu atukanwe kwani yeye ndiye aliyenizaa Mimi Nina hakika ila sio sana maana mwenye hiyo hakika ni mama yangu.

Ila nimeamua kwenda mbele zaidi baada baba kurudi nyumbani kimefanyika kikao kizito cha kujadili ilihali wa baba yetu aliyetukanwa, Ili kudhibitisha yakuwa sio kweli tusi alilotukanwa na sisi tu wanae.

Katika kikao hicho tumekubaliana yafatayo.

Kwanza watoto wote tufanyiwe vipimo vya DNA testing.

Pili Ikibanika tu Wana wa baba mmoja basi baba atukubalie sisi tufungue kesi dhidi ya Simbachawene kwa malezi yake mabaya kwa vijana nguzo ya Taifa hili.

Niliwahi jiuliza Kwanini mwendazake aliwahi mwambia Simbachawene yakuwa hakuwa Ikulu kuuza sura? Sasa naanza pata majibu.
Hii mada yako na ile ya wakili msomi Pascal Mayalla zimedhihirisha namna gani makosa ya Tort ni mageni kabisa Tanzania.

Kikubwa kinachoangaliwa kwenye makosa haya ni :-
1.Duty of care
2. Breach of that duty
3.Demage
Sasa huyu ndugu Simbachawene ambaye naye ni msomi wa sheria kutoka chuo kikuu huria kama ilivyo kwa wakili msomi Pascal Mayalla , je! ana duty of care kisheria kwa lijitu lizima ambalo limezidi miaka 18 na lina familia yake? Nadhani Simbachaweze ameamua kutokahadharani na kulaani kitendo hicho lajitu ka,a raia mwingine aliyekerwa na kitendo hicho cha kumdhoofisha afisaa akiwa anafanya kazi yake na tutambue kuwa bado simbachawene ni mwanafamilia wa taasisi hiyo kwani aliwahi kuwa waziri wake , hivyo kuna yale mahusiano ya kufaamiana kwaz kufanya kazi pamoja.

Kwangu mimi, kwa njia yoyote ile hutuwezi kumuunganisha Simbachawene kwenye ujinga alioufanya mtu huyu na sijawahi kusikia tort ya aina hiyo.

Tort kama ilivyo kwenye makosa ya jinai huwezi kuhukumiwa kwa kosa ambalo halipio kisheria (Nulla poena sine lege ), Kadhalika baba wa Jurisprudence duniani Salmond alifafanua vilevile kuwa Tort nayo ina makosa yake, hivyo sio kila kitu utakifananisha na tort na kukipeleka mahakamani. Hapa alitolea ufafanuzi na kulinganisha na matundu ya nyumba ya njiwa kuwa ili njiwa aingie kwenye tundu lake lazima hilo tundu liwe na ukubwa ambao njiwa anaweza kukaa ( PEGION HOLE PRINCIPLE)

According to Salmond, “Tort is a civil wrong for which the remedy is a common-law action for unliquidated damages, and which is not exclusively the breach of contract, or, the breach of trust, or, other merely equitable obligation.”
Hivyo kwa maoni yangum wanaharakati wanaoliongelea hili, wanaongea kufurahisha jukwaa tuu au kwa sababu kuna mtu mkubwa katajwa lakini ilkienda mahakamani kama Simbachaweze atakuwa jointed inapigwa P.O asubuhi na mapema, lakini Polisi wana nafasi kubwa ya kumshitaki huyo kijana aliyefanya kosa hilo ( in his individual capacity) kwa makosa ya jinai cum usalama barabarani na Tort ikiwezekana ijapokuwa kupata UNLIQUDATED DEMAGES kwa askari kwa makosa ya tort yanayotokea kutokana na majukumu yake ni ngumu sana na hii nilisoma kesi nyingi za kizungu za askari waliopata madhara ya Post-traumatic stress disorder (PTSD) pale ambapo wanaposhukulikia matukio ya kutisha kama ajali, mauji nk na kuishia kupata mishtuko inayowaletea madhara ya kiakili na kimwili, kuna debate kubwa sana kwenye sheria kuhusu injury wanazozipata watu lakini hazionekani kwa macho na ni mbaya zaidi kuliko pysical injuries

Avogadro. LLB hons OUT
 
Tulia. Baba yako akileta nyoko nyoko ata hamishwa babarani, apelekwe kuwa Askari magereza, huko Mpanda.
 
Inafedhehesha Sana mshua akiitwa hivyo mbele ya watu au mtu wa karibu wa bi mkubwa akitukanwa na mtoto mbele ya watu.
Huyo Askari angekua mhehe au mchaga Sasa hivi mawaziri wangekua wanapishana Muhimbili.
Labda useme Mhehe, ila si Mchagga.
 
Hawa jamaa zetu chenga sana,
Anzia wachimba madini wa Mahenge chini ya Zombe,
Njoo 150m jangwani chini ya Kova.
Njoo ya Juzi Mtwara.

Kama imethibitika ni mkosaji , sheria ifuatwe pasipo kuacha shaka.
Haya mambo ya kaa kwenye kiti ,umemtukana nani sijui nini , hayana nafasi ktk traffic case.
Dah umenikumbushs ya Mtwara na yule askari mwenzao waliyemnyonga. Halafu eti leo wawe wadilifu
 
Hapana hao askali ni waongo. Yule dogo siyo kichaa afanye hayo aliyoyafanya. Nina uhakika kulikuwa na mazingira ya rushwa.

Kuna mtu mmoja siku moja Dar alikuwa hizi hoteli za uswahilini, tena ni dereva wa serikali, sasa askali wakapita walikuwa na ukaguzi wa kawaida.

Basi wakamgongea mshikaji akafungua, bahati mbaya jamaa alikuwa kaweka waleti yenye hela zimetuna na zingine zimetokezea (zilikuwa per diem na mafuta ya safari), basi yule askali alivyoona jamaa alipigwa bonge la kofi na mateke bila hata kumuuliza na akasema nyie ndiyo majambazi tunawatafuta.

Baada ya hapo jamaa kapigwa pingu na kupelekwa mahabusu, alijitahidi kujielezea wapi, akaenda kuwekwa mahabusu na waleti yake na hela zimechukuliwa.

Wakaanza kumuandikisha maelezo yeye kama jambazi. Bahati nzuri alifahamiana na watu, yule askali alifukuzwa kazi baada ya kujulikana ukweli.

Naamini watoto wa viongozi wanapaswa kupewa heshima na siyo kuwadhalilisha.
Sema watanzania wanatakiwa kupewa heshima na hao poliCCM sio kusema watoto wa viongozi?
Kwani hao watoto wa viongozi ni akina nani?
Acha uchawa wa kingese!!
 
Wamemrekodi clip nyingi nyingi tu kuanzia nje hadi ndani ya kituo, na wao wana makosa. Aligoma kuingia kituoni ikabidi wamfosi wakawa wanamsukuma ndio maana akawa anatukana pale ndani ya kituo na yeye anataka kulipwa kwa kudhalilishwa
Kwanin akatae amri halali au kibao cha tii sheria bila shuri hakukiona?
 
Shida kubwa sana ipo kwa jamaa zetu.
Tukio limetokea namba za gari mmezipata, mmiliki mnamfahamu, kuna haja gani kumkimbiza?

Shida imetokea hakuna kifo, wahusika wapo tayari kuyamaliza Nyie mnang’ang’ania twende kituoni, wakafanye nini?.

Ila pia kuna kipimo cha pombe ili kuthibitisha kiasi alicholewa dereva, je hicho kilifanyika?

Ya wezekana alikuwa element anakunywa Maji.

Hivi leo hii wakipanda mahakamani nani anashinda kwa mazingira kama hayo.?

Kila mtu akitimiza wajibu wake hatuwezi fika huku.
Kwahiyo ukisababisha ajari, wenye mali mkiamua kulipana ndiyo basi, askari wa usalama barabarani, hawana chao tena siyo, kwa mujibu wa sheria zetu?
 
GTs,

Kama tulivyoona kijana wa Mh. Simbachawene alivyoingia kituoni halafu kuna askari akamchoza kwa tusi. Je, hiyo ni sahihi? Je, ni kweli alitukana na je, ndiyo njia sahihi ya askari kufanya kazi?

Je, haki za kijana wa Mh. Simbachawene zilifuatwa, au alitishiwa na hao askari ili atoe rushwa ila baada ya hao askari kujua ni mtoto wa kiongozi, ikabidi wamrekodi na kumchokoza ili akasirike warekodi na kumdhalilisha?

Naamini jeshi la polisi litafanya uchunguzi ili kubaini hasa kitu gani kilitokea. Maana hao askari inaonekana walijipanga kuhakikisha dogo wana mdhalilisha.

Na kibaya walilenga kumdhalilisha Mh. Simbachawene, na huyo kijana inaonekana ni mtu mwenye heshima na anajitambua ila hao askari walimtengenezea mazingira baada ya kuona wamekosea ili kujikosha kwa jamii.

Ila mtindo wa askari ndiyo huo kudhalilisha na kusumbua ili wapate rushwa.

Naamini Mh. Simbachawene atamlinda mwanae, akiwaachia hao askari Polisi wamshughulikie mwanae wanaweza kufanya yale ya Mtwara.

Chonde chonde Mh. Simbachawene, hukupaswa kabisa kutoa ruhusa mwanao ashughulikiwe wanaweza kumuua ili wapoteze ushahidi maana mifano ipo mingi ya askari kuua watuhumiwa ili kuficha ushahidi.
Hebu kakae na babaako nyumbani muyaongee kifamilia, sio Kuja humu JF.
 
Back
Top Bottom