Nani aliwachagua kuwa viongozi wa dunia? G7 ni viongozi wa nchi 7 tu si zaidi ya hapo

Baada ya Marekani inafuatiwa na China ndio taifa la pili kwa kuichangia UN na taasisi zake

UN regular budget 2023:

USA 🇺🇸 (22%),
China 🇨🇳 (15.25%),
Japan 🇯🇵 (8.03%)
Germany 🇩🇪 (6.11%)
 
Hapa nakubaliana na wewe...Lakini siyo kweli, Africa na dunia ikiamua G7 inaweza kufanya lolote...Hao wanatumia psychology kuaminisha watu kwamba wao ni super beings...
Mkuu, tatizo ni kwamba watu wasiosimamia tunu na maadili ya pamoja hawawezi kuungana kwa lolote. Si rahisi kwa Afrika na dunia kuamua kupambana na G7 wakati utajiri wa viongozi wetu unatunzwa katika nchi za G7 na wengi wetu tukiwa machawa wa hao viongozi mafisadi.

Ni miaka mingi Afrika imeshindwa kusimama pamoja kupigania maslahi yake. Waafrika wamekuwa wakiuzana wenyewe kwa wenyewe tangu enzi za utumwa, ukoloni hadi leo wanasaidia wageni kuhujumu rasilimali za taifa. Na huko duniani kwingi, viongozi hawana mipaka mbele ya rushwa na ufisadi. Maslahi binafsi yanazidi uzalendo kwa nchi zao.

Nchi za G7 zina viongozi na raia wengi wenye akili kubwa na misimamo imara ya kuimarisha himaya za nchi zao kwa vizazi vingi vijavyo. Hawaendekezi ujinga kama huku kwetu. Viongozi mafisadi wanadhibitiwa na mifumo imara. Hiyo ndiyo kete kuu ya G7.
 
Eti Nchi zinazoendelea kiviwanda,shortly Nchi zinazoongoza kiuchumi.Kati ya hayo mataifa 7 ukichukua uchumi wa Mataifa 5
Uchumi wa Uingereze,,Germany,Italy,Canada & France bado hawafiki uchumi wa China but cha ajabu China hayumo kwenye umoja huo.

Wazungu wanafiki sana,
 
Reactions: Ame
Soko kubwa la China ni Nchi za Sea, ikifuatiwa na Us halafu ndio Ulaya
🇨🇳China's top trading partners (% of China's total exports):

1.🇺🇸US: 16%
2.🇭🇰HK: 8%
3.🇯🇵Japan: 4%
4.🇰🇷S Korea: %4%
5.🇻🇳Vietnam: 4%
6.🇮🇳India: 3%
7.🇳🇱Netherlands: %3
8.🇩🇪Germany: 3%
9.🇲🇾Malaysia: %2
10.🇹🇼Taiwan: 2%
11.🇬🇧UK: 2%
12.🇸🇬S'pore: 2%
13.🇦🇺Australia: 2%
14.🇹🇭Thailand: 2%
 
Ujifungie utaishije?. Mikopo Nani atakupa. Maana nchi nyingi za Africa zinaishi kwa madeni kutoka G7.
Nimetoa mfano, wanaihitaji Africa kuliko Africa inavyowahitaji wao.

Miaka ya 1970s mfalme wa Saudia Faisal alitoa hii kauli,

Hapo ni baada ya wamarekani kutishia kulipua Visima vya mafuta vya Saudi jamaa akawajibu kwamba "ni Nyie ndio Hamuwezi kuishi bila mafuta, sisi tumetoka jangwani na wazee wetu waliishi kwa kutegemea Tende na Maziwa tunaweza kurudi kuishi kama hivyo tena"

Jiulize kitu Kimoja mkuu, Dhahabu, Almasi, Tanzanite na madini mengine nani anayahitaji sana? Mzungu ama Mu africa? Tusipochimba tunakosa nini? Pengine 5 ama 10% tu, wao wanayahitaji zaidi kuliko sisi tunavyoyahitaji

Juu hapo kama umeona Comment yangu kuhusu Indonesia, jamaa wametoboa na raw Materials tu, sidhani kama Indonesia ana utajiri hata robo tu ya Congo, ila jamaa wamelinda Resource zao na zinafaidisha nchi, ila sisi Chawa pro max tunagawa tu.
 
Hata china ana BRICS kila nchi ina kundi lake, lakini G7 ndio inasidia nchi nyingi hasa mikopo na nk
Kaka acha kuchanganya madesa,hapo issue sio mataifa yanayosaidia Nchi zingine Mikopo bali zinazoongoza kiuchumi.
Kama ni Mikopo,Mikopo iliyotolewa na China jumla ukiijumuisha utawezankujumuisha hayo mataifa 5 hapo hata wasimfikie.
Nchi kama Italy anatoa Mikopo gani.
 
Wanauwezo wa kutawala akili za watu...Wanaijua sana psychology ya mwanadadamu, ki kama imami ya ukristo inavyotufundisha shetani alivyo...Anatumia FEAR ku oppress powerful christians...

Ni matapeli wazuri
 
Vietnam, Singapore, Malyasia etc zote zinakuja kama Sea Region, inategemea na utakavyo categorize.

Source
 
Kuna wanaoitwa "maskini jeuri". Wanajali heshima yao na hawako tayari kuiuza kwa gharama yoyote!! Watakuambia "potelea mbali na pesa yako". Watu kama mwalimu Nyerere, Robert Mugabe, Fideral Castro nk.
Labda panya wa nyumbani kwako wakuheshimu
 
Kuna tofauti ya kubweka na kung'ata...fikiri
 
Baada ya Marekani inafuatiwa na China ndio taifa la pili kwa kuichangia UN na tasisi zake

UN regular budget 2023:

USA 🇺🇸 (22%),
China 🇨🇳 (15.25%),
Japan 🇯🇵 (8.03%) and
Germany 🇩🇪 (6.11%)
Mrusi yuko kama jibwa KUBWA lisilo ng'ata hana faida kimataifa
 
ukichukua uchumi wa Mataifa 5
Uchumi wa Uingereze,,Germany,Italy,Canada & France bado hawafiki uchumi wa China but cha ajabu China hayumo kwenye umoja huo.

Wazungu wanafiki sana,
Kigezo kimojawapo cha kuwa member wa G7 eti wanasema lazima taifa lako liwe na uchumi mkubwa na la democracy na uheshimu aspects za democracy kama human rights n.k

Ndio maana wanajiita bloc of industrialized democracies

China sio nchi ya kidemokrasia ndio maana wanasema hana sifa na hajawahi hata kualikwa kwenye vikao vya G7 kama mataifa mengine yenye uchumi unaokua kwa kasi na ya kidemokrasia kama India, Brazil na South Korea yanavyoalikwa

Mwaka huu 2023 India na Brazil zilialikwa kuhudhuria G7 summit kule Japan

China kuja kuwa member wa G7 hilo sahau hata awe na uchumi kumzidi Marekani
 
Nakubaliana na point zako nyingi isipokuwa pale uliposema Tanzania haiisaidii chchote USA. Hivi ukae ukijua kuwa mi binafsi na watanzania kama wote hivi wanaweza kuishi (na tunaishi) bila msaada wa Marekani. So usije kujidanganya kamwe kwamba kuna model ya aina moja ya maisha ya utoshelevu hapa duniani. Vivyo hivyo kanuni za maisha na utawala wa dunia wanazoziweka Marekani na washirika wake zitakuwa na nguvu only kama umejiweka akili kutawaliwa na hizo kanuni. Mfano mdogo ni jinsi walivyotaka kuweka makanuni ya jinsi ya kuishi baada ya corona. Ukiwa mpuuzi utaishi kama wanavyotaka wao uishi.
 
Reactions: Ame
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Wana dunia yao.....
 
Sawa kabisa, ni propaganda tu na kuna watu wanaamini hilo. Ukitaka kuongea na viongozi wa dunia basi ni pale unapoongea kwenye viunga vya umoja wa mataifa New York. Tatizo vyombo vyenu vya habari ni dhaifu sana na vinategemea vyombo vyao kupata habari
 
Unasahau kwamba hawa unaowaita viongozi wa dunia hawawezi kumpangia China, Russia, Syria wala Iran
 
Reactions: Ame
Hao ndio wanaoishape Dunia iwe namna ilivyo. Ndio wamiliki wa karibu tekinolojia tekinolojia zote za Dunia.
Yes, wanamiliki teknolojia lakini kuna utofauti kati ya kuwa na teknolojia ikakusaidia kuwa na uwezo wa kiuchumi na kutaka kuwatawala watu wote wa dunia hii waishi kama unavyotaka waishi. Ile ya kwanza ni nguvu ya uchumi ila hii ya pili ni ulevi tu wa kikoloni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…