Naomba kujuzwa gharama za msingi kwa nyumba ya ghorofa moja

Naomba kujuzwa gharama za msingi kwa nyumba ya ghorofa moja

Mtoa mada tunakungoja mana wewe ndio utakuja na hesabu halisi
 
ushauri tu awe na hiyo kitu. kuna chuma zinasukwa chini (base) na kuzunguka msigi wote, kuna tofali zinazikwa kozi zaidi ya saba za kulaza, kuna mkanda unapigwa mzunguko wote, kuna zege chini kwenye base na huo mkanda, kuna kifusi cha kujaza, kuna framework za kufunga na mambo ya mafundi. Basically, ata cement. mchanga, na kokoto zote zimepanda
Screenshot_20230521-132046.jpg

Screenshot_20230521-132004.jpg

Ghorofa Moja mkuu no way
 
Wataalam naomba rough estimate ya msingi wa kijumba chenye GHOROFA MOJA, ukubwa wake ni 7680x9270.

Gharama ya msingi hadi kufunga mkanda ni kiasi gani cha fedha, Eneo ni flat kabisa.

Je, hatua au mbinu gani unaweza kufanya kupunguza gharama zisizo za lazima?

Nimefuatilia hii post kwa umakini mtoa maada Wewe ni mtu na nusu
Barikiwa sana political Engineer 2
 
samahani mleta mada nipo nje ya mada kidogo,mimi ni fundi wa kufunga cctv camera,electric fence,gate motor pamoja na video door bell,kwa mwenye kuhitaji huduma naomba tuwasiliane kwa namba 0622667749 au 0674376787 nipo Dar es Salaam
 
Natumia uzoefu wangu maana vipimo havionekani vizuri. Hapo roughly andaa 15M mpaka 17M kutegemea na mahali ulipo bei ya materials ikoje na utatumia njia ipi kujenga i.e mkandarasi (kampuni), fundi maiko au utanunua materials na kumtafuta mtaalam (engineers) akujengee.
Vipimo vingeonekana ningekusaidia vizuri zaidi mkuu.
Kwa 17m msingi, hilo ghorofa litaanguka mara baada ya kukamilika. Huyo jamaa aliyesema 50m yawezekana (kwa kutumia Wataalam sio Fundi Maiko). Maana binafsi nilitumia 40m kabla bei ya Nondo haijaongezeka.
 
Unaweza kunikadiria yangu mkuu. Ina upana wa 17' na marefu 21 eneo pia ni tambarare...hadi sasa tayari nimeshakusanya Nondo mm 16 Tani 2; Nondo MM 8 ziko 100, Mchanga CBM 70, Kokoto nene CBM 50, Tofali 6' ziko 2,500, Misumari nchi 3 na 4 kigunia kimoja kimoja, binding wire roller moja na marine boards ziko 10. Mkuu hapo nimebakiza nini ili nikamilishe msingi peke yake hadi hatua ya kufuta kiti na kuachia matoleo ya nondo. Plani yangu nataka nimtumie Fundi Maiko. Tafadhali naomba makadirio yako...hizi BOQ nimegundua zimekuwa zinadanganya sana... Tafadhali
Mkuu tupe mrejesho umefikia wapi, wapw experience wakuu
 
Kwa 17m msingi, hilo ghorofa litaanguka mara baada ya kukamilika. Huyo jamaa aliyesema 50m yawezekana (kwa kutumia Wataalam sio Fundi Maiko). Maana binafsi nilitumia 40m kabla bei ya Nondo haijaongezeka.
M17 inatosha kulingana na ukubwa wa Hilo ghorofa, ambayo yana chini ya 100sqm huwa inatosha kulingana na gharama za fundi

Kwa hizi za kawaida za kuishi zinazojengwa, hizi za residential hiyo 50m huwa Kuna uongo. Wengi hupenda kuonekana wametumia gharama ili kuongeza value ya kitu chake na yeye kuonekana yupo vizuri.

Ujenzi wa ghorofa upo overrated na watu ndio maana hutaja overprice. Ni gharama, lakini sio kama zinazotajwa na watu. Nimeongea through experience kwa maana naujua uhalisia
 
M17 inatosha kulingana na ukubwa wa Hilo ghorofa, ambayo yana chini ya 100sqm huwa inatosha kulingana na gharama za fundi

Kwa hizi za kawaida za kuishi zinazojengwa, hizi za residential hiyo 50m huwa Kuna uongo. Wengi hupenda kuonekana wametumia gharama ili kuongeza value ya kitu chake na yeye kuonekana yupo vizuri.

Ujenzi wa ghorofa upo overrated na watu ndio maana hutaja overprice. Ni gharama, lakini sio kama zinazotajwa na watu. Nimeongea through experience kwa maana naujua uhalisia
Bora wewe unaandika uhalisia maana wengine dah ukiwasoma ni mwijaku style
 
Uzi mzuri sana, hongera mtoa mada,
Kuna maswali tumekosa majibu, pia tulipenda kuona picha ya msingi wa 9 M.

Mtoa mada amepotea au ndo alidondokewa na ghorofa goba au lile la kigamboni(jokes)
Mtoa mada hataki kuongea na nyie ambao hamna maghorofa.. 😁 panapo majaaliwa si kitambo kirefu, mimi pia naanza ujenzi wa ghorofa yangu, uzuri ni kwamba site engineer ni mimi mwenyewe, nina degree ya civil engineering, ramani nimekwishachora (both architectural and structural).

Najaribu kufanya material estimation naona kabisa sipo mbali sana na mtoa mada, gharama zangu na zake hazitofautiani sana (zangu zipo juu kidogo).
Column natumia nondo 4 za 16mm
Plinth beam na beam ya floor ya kwanza pia natumia 16mm
Slab na stair nasuka top na bottom kwa 12mm 200c/c.
Stirrups au ringi natumia 8mm.
Msingi ni mrefu kidogo. 900mm

Aina ya nyumba ni victorian gothic.
Nyumba ina 9x9m
Ground floor kuna.
Self contained room 1.
sitting room 1.
Dinning room.
kitchen & store

1st floor kuna.
Master bedroom kubwa tu
Self contained room 1.
library.

Aidha kwa mwenye uhitaji wa ramani ya nyumba au ushauri wa masuala ya ujenzi.
Kindly pm.
Kuna jambo likitimia naanza kutafuta mafundi tufanye kazi.

Nikimaliza ujenzi ntaanza kuongea na wenye maghorofa wenzangu tu kama alivyofanya mtoa mada. 😁(jokes)
 
Back
Top Bottom