Naomba ushauri: Kijana wangu amepata kazi Shirika la Good Neighbors na Halmashauri, aende wapi?

Maandiko yanasema mwenye nacho ataongezewa na asiye nacho ata kile kidogo alichonacho atanyang'anywa Mkuu.
 
Ni kitinda mimba wangu. Amepata kazi Serikalini kwenye Halmashauri moja Mkoani Shinyanga na pia kwenye Shirika linaitwa Good Neighbors Tanzania. Mishahara ni kama inalingana, aende wapi?

Naomba ushauri wapendwa.
kwa upande mwingine muache achague nini anataka
 
Kama ni wakike aende zake Good Neigbours.

Ila kama ni wakiume mwache aamue mwenyewe aende wapi.
 
Aende Halmashauei akithibitishwa kama ana hulka ya kufanya kazi kwenye mashirika anaomba likizo bila malipo anapiga mzigo huko mashirikani kwenye mashara mnono na nafasi yake huko halmashauri inabakia kumsubiria.
 
Aende halmashauri akiiacha hiyo nafasi atajuta. Serikalini nafasi ni chache na wanaopata ni bahati.
 
Ni kitinda mimba wangu. Amepata kazi Serikalini kwenye Halmashauri moja Mkoani Shinyanga na pia kwenye Shirika linaitwa Good Neighbors Tanzania. Mishahara ni kama inalingana, aende wapi?

Naomba ushauri wapendwa.
Ha!! Unajiuliza.Aende Halmashauri maana kama kweli mishahara inalingana ujue Halmashauri utazidi...usiulize sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…