Naomba ushauri kuhusu biashara yangu inakoelekea inaenda kukata roho sio muda

Naomba ushauri kuhusu biashara yangu inakoelekea inaenda kukata roho sio muda

Pole mkuu...

Ila unatakiwa ujue kwamba asilimia kubwa ya watu ambao wamefanikiwa kwenye maisha ya utafutaji hasa kupitia kwenye upande huo wa kibiashara ni kwamba wameweza kujiungamanisha na upande wa kiroho iwe kwa kujua au kwa kutokujua na iwe upande wa kiroho wa gizani au upande wa kiroho wa nuruni, huwa haijalishi Ila nguvu za umiliki huwa haziko upande huu wa damu na nyama bali zipo upande wako wa pili ambao ni upande wa kiroho.

Kwahiyo Kuna watu ambao walijaribu biashara nyingi sana ambazo zote hazikuwapa mafanikio Ila baadae walikuja kukutana na biashara moja tu ambayo walivyoamua kuifanya hapo hapo wakaanza Kuona mafanikio ambayo hawajawahi yaona kwenye biashara nyingi walizowahi kuzifanya na hii biashara ndio tunasema sasa kwamba inayo muunganiko wa moja kwa moja na upande wako wa kiroho Kwahiyo inakuunganisha pasipo wewe mwenyewe kujua.

Inawezekana hujaelewa hapo Ila nakuhakikishia kwamba biashara ni kama mila na desturi zilizopo kwenye makabila, kwamba Kuna mila inaaminiwa sana na kabila fulani na wanaifuata kwasababu inawapa matokeo wanayoyataka pindi wanapoifuata Ila wewe mtu wa kabila lingine ukienda kuifuata hiyo mila haitakupatia chochote unachotaka kwasababu wewe asili yako haiko huko Kwahiyo na wewe ukitaka ufanikiwe kwenye mambo ya kimila nilazima ufuate zile mila ambazo zinafungamana na asili yako.

Tukirudi kwenye biashara ni the same, biashara ambayo inampa faida kubwa sana rafiki yako wewe ukienda kuijaribu unaweza usifanikiwe hata kwa japo faida kidogo, sana sana utapoteza mtaji wote huko kwasababu hiyo biashara haifungamani na wewe kiasili ila biashara hiyo hiyo ambayo wewe hufanikiwi nayo unakuta Kuna rafiki yenu mwingine kwenye hiyo cycle yenu nae anajaribu kuifanya ghafla anafanikiwa, sasa wewe unaweza kujihisi unagundu na mikosi ila wala sio kweli ni vile tu haujui namna ya ulimwengu unavyofanya kazi.

Kuna biashara ambazo zinafungamana na watu fulani fulani na Kuna biashara ambazo hazifungamani na watu fulani fulani.

Najua ni mambo ambayo yanashangaza halafu yamekaa kufikirika fikirika sana, ila ndio asili ilivyo na ndio maana always unaambiwa dunia inaendeshwa na watu wenye nguvu, sasa watu wenye nguvu sio kwamba wako na misuli mingi, hapana ila watu wenye nguvu huwa wanajua namna universe inavyofanya kazi na ndio maana unaona matajiri wengi huwa wanawekeza pesa nyingi kwenye vistartup venye idea nyepesi sana wakati wangeamua wangeweza kununua hizo algorithm na kuzifanya wao wenyewe ila wanafanya hivi kwasababu wanajua sio kila biashara lazima wewe uwe main player lakini unaweza kutembelea migongo au nyota ya watu wengine kwa kuwekeza kwao kwenye zile biashara ambazo zinafungamana na wao moja kwa moja na ukaendelea kula share zako kwa kadri ya ulivyowekeza.

NB
Hii ni code nimewafungulia sasa unaweza ukapita nayo au ukaipita... Yesu mwenyewe alikua fundi selemala kwani unadhani hakuona kazi zingine za kufanya 😆😆😆😆

Unatakiwa ujue hatima yako kwanza... kila mtu huko hapa duniani kwa lengo maalumu na hilo lengo ndio hatima na kwenye hatima yako ndiko kuliko na bahati yako... kwa hiyo ukijua hatima yako ndio umejua asili yako na ukijua asili yako basi itakua rahisi kujua biashara zinazoendana na asili hiyo... ukishindwa ndio unafanya try and error hadi utakapojipata though hii ni very boring na inachukua muda sana kujipata.

Baki kwenye huu uzi hadi ukimalizika kuna kitu unaweza ukatoka nacho Thread 'Dunia ni uwanja wa vita za hatima.' Dunia ni uwanja wa vita za hatima.
Yap 100%. Nilijaribu kumwelezea na mimi sema sikufunguka vizur. Ishu za kibiashara zipo kiroho sasa aangalie wapi pa kwenda na kufanikiwa. Pia ajitathimin yeye mwenyewe sio kila mtu anaweza kuwa mfanyabiashara ndo maana unaweza mpa mtu hata 100M ikafa yote.
Kabla ya kuingia kwenye biashara aangalie hayo mambo uliyomfafanulia hapo juu.
 
Pole kwa bei hiyo mimi naona umejikita uuze kwa bei ya chini mzigo mzuri na uwe unatoka ila umefeli kwani unaambulia faida kiduchu,

Badili mfumo weka mali kali na bei pia iwe mkasi ila usiwasahau wa bei ya chini wawekee nao mzigo wao.. wapo wateja ambao bei kwao sio ishu wanataka mali safi utawapata.

Weka na bidhaa nyingine za kusindikiza mchele kama mafuta unga Dagaa Mayai.

Ukifeli pia usikate tamaa utakua umejifunza angalia location nyingine au badiri biashara.
Mkuu hongers kwa ushauri wako. Mlengwa asipoufanyia kazi basi kutakuwa na tatizo sehemu.
 
Mzee ninavioo pale ofisini achaa nina super za kila aina tena zinanukia blaaa ila ujinga wake zeneywe utokaji wake ni mudg kwa sabab mbagala wengii ni kipato cha chini kwaiyo wanahitaji michele ya bei ndg na ndo yenye mznguko mkubwa
Kama ulivyosema ndivyo ilivyo basi hiyp location sio sahihi kwako. Jaribu kutanuo wigo fungua branch sehemu nyingine ya watu wengi wa kipato cha kati + weka huo mchele wako gredi za juu na hapo bakiza mchele unaoendana na mahitajo soko la hapo.
 
Kama ulivyosema ndivyo ilivyo basi hiyp location sio sahihi kwako. Jaribu kutanuo wigo fungua branch sehemu nyingine ya watu wengi wa kipato cha kati + weka huo mchele wako gredi za juu na hapo bakiza mchele unaoendana na mahitajo soko la hapo.
Shukranii sana ndo nalifanyia kazi hilo wazo
 
Sina uzoefu wa biashara ya mchele ila sababu nilishafanya biashara zingine so naomba nikushauri kulingana na uzoefu wangu kwenye biashara nyingine.

Umesema mpaka sasa una miezi saba,basi hiyo miezi ni michache kwa biashara kukomaa na kuweza kukupa faida ile uliyoipanga.Mara nyingi biashara nyingi huwa zinaanza kukua kwenye miezi sita ya pili,haani ndio angalau unaanza kufikia biashara kujiendesha bila hata ya kutengeneza faida.
Chakufanya chukua daftari lako la mauzo tangu umeanza biashara,piga hesabu ya kila mwezi kwa miezi hiyo saba uangalie je mauzo yalikua yakiongezeka kila mwezi? Tafuta wastani wa mauzo wa kila mwezi kwa siku kujua uhalisia wa ukuaji wa biashara yako,kama mauzo yanaongezeka hata kama ni kidogo basi jua biashara yako inakua ila ni kaa speed ndogo na inazidiwa na expenses so unahitaji kufikiria njia ya kupambana na hilo.Kwa hiyo mtaji unakata kwa sababu biashara ina matumizi makubwa.

Kwa upande wa kuhama biashara moja kwenda nyingine ni lazima ujue kuwa unaenda kuanza upya na kuanza upya kunahusisha kufanya makosa mengi ambayo huku kwenye mchele ulishayafanya na ukajisahihisha kufikia hapo ulipo sasa hivi.Tunapozungumzia uzoefu kwenye jambo fulan huwa tunamaanisha na hayo makosa ambayo kivyovyote hayaepukiki na yana gharimu muda,pesa,taarifa na network ya watu.
Pia lazima ujue kuwa classes kwenye maisha zipo na haziepukiki,kama unauza bidhaa fulani,huwa ni ngumu sana kuuza sana kama utachanganya watu wa tabaka la juu na watu wa tabaka la chini.Yaani huwezi kuwa na duka moja ukajaza bidhaa za matajir na masikini halaf ukategemea hao watu wote watakuja kwako,huo ni uongo hapo ni lazima tabaka moja litajichuja na hivyo utapata hasara tu.
Mfano matajiri watahitaji eneo lako lionekane kitajir yan lina mvuto na high classic sasa ukiweka eneo lako hivyo lower class wataogopa kuja hapo maana wao saikolojia yao na vitu hivyo haiendani kabisa kwa kuhofia bei,na kama watakuja wale wa juu hawatakuja maana aina ya wateja wako itawafukuza kwa kuona pamekaa kiswazi na ikitokea wakaja,wakiingia ndani wakakuta unavitu vya bei rahisi sana kwenye akili yao wanaogopa kuwa vitu vyako vyote havina quality hata kama ni kweli umejitahidi kuvitenga kulingana na ubora wake.
So chagua tabaka unalotaka kudeal nalo halafu komaa mpaka wakujue ujenge uaminifu nao na hapa utahitaji huduma bora kulingana na tabaka unalolilenga lakini pia uweze kutoa huduma hiyo muda wowote watakao hitaji huduma yako bila kupunguza ubora.
Kama unauza jumla kweli basi ni lazima uwe na jumla mbili,jumla kwa ajili ya watu wanaochukua kwa ajili ya matumizi ya kifamilia na jumla kwa ajili ya watu unaowajua kuwa wanamaduka.Bei ya mtu ambaye unajua kuwa anaduka inatakiwa iwe tofauti kabisa na bei uliyoibandika kwenye gunia kuwa ni bei ya jumla.Na mfanye mteja ajue kwamba kwako kuna bei fulani za wateule ambazo hazipo kwenye magunia ya mchele hapo utatengeneza wateja permanent,hii phyilosophy kajifunze kwenye maduka ya jumla kkooo
Cha mwisho wewe pita kwenye maduka ya rejareja ukatangaz3 mchele,waachie namba yako waambie wakupigie pindi wanapphitaji mchele ili uwape bei
Nakutakia kazi njema,usikate tamaa maana familia yako inakutegemea.Haya ndio maoni yangu kwako na samahani maana kuna maeneo nimechanganya vimisamiati vya kiingereza ila natumai tumeelewana.
 
Sina uzoefu wa biashara ya mchele ila sababu nilishafanya biashara zingine so naomba nikushauri kulingana na uzoefu wangu kwenye biashara nyingine.

Umesema mpaka sasa una miezi saba,basi hiyo miezi ni michache kwa biashara kukomaa na kuweza kukupa faida ile uliyoipanga.Mara nyingi biashara nyingi huwa zinaanza kukua kwenye miezi sita ya pili,haani ndio angalau unaanza kufikia biashara kujiendesha bila hata ya kutengeneza faida.
Chakufanya chukua daftari lako la mauzo tangu umeanza biashara,piga hesabu ya kila mwezi kwa miezi hiyo saba uangalie je mauzo yalikua yakiongezeka kila mwezi? Tafuta wastani wa mauzo wa kila mwezi kwa siku kujua uhalisia wa ukuaji wa biashara yako,kama mauzo yanaongezeka hata kama ni kidogo basi jua biashara yako inakua ila ni kaa speed ndogo na inazidiwa na expenses so unahitaji kufikiria njia ya kupambana na hilo.Kwa hiyo mtaji unakata kwa sababu biashara ina matumizi makubwa.

Kwa upande wa kuhama biashara moja kwenda nyingine ni lazima ujue kuwa unaenda kuanza upya na kuanza upya kunahusisha kufanya makosa mengi ambayo huku kwenye mchele ulishayafanya na ukajisahihisha kufikia hapo ulipo sasa hivi.Tunapozungumzia uzoefu kwenye jambo fulan huwa tunamaanisha na hayo makosa ambayo kivyovyote hayaepukiki na yana gharimu muda,pesa,taarifa na network ya watu.
Pia lazima ujue kuwa classes kwenye maisha zipo na haziepukiki,kama unauza bidhaa fulani,huwa ni ngumu sana kuuza sana kama utachanganya watu wa tabaka la juu na watu wa tabaka la chini.Yaani huwezi kuwa na duka moja ukajaza bidhaa za matajir na masikini halaf ukategemea hao watu wote watakuja kwako,huo ni uongo hapo ni lazima tabaka moja litajichuja na hivyo utapata hasara tu.
Mfano matajiri watahitaji eneo lako lionekane kitajir yan lina mvuto na high classic sasa ukiweka eneo lako hivyo lower class wataogopa kuja hapo maana wao saikolojia yao na vitu hivyo haiendani kabisa kwa kuhofia bei,na kama watakuja wale wa juu hawatakuja maana aina ya wateja wako itawafukuza kwa kuona pamekaa kiswazi na ikitokea wakaja,wakiingia ndani wakakuta unavitu vya bei rahisi sana kwenye akili yao wanaogopa kuwa vitu vyako vyote havina quality hata kama ni kweli umejitahidi kuvitenga kulingana na ubora wake.
So chagua tabaka unalotaka kudeal nalo halafu komaa mpaka wakujue ujenge uaminifu nao na hapa utahitaji huduma bora kulingana na tabaka unalolilenga lakini pia uweze kutoa huduma hiyo muda wowote watakao hitaji huduma yako bila kupunguza ubora.
Kama unauza jumla kweli basi ni lazima uwe na jumla mbili,jumla kwa ajili ya watu wanaochukua kwa ajili ya matumizi ya kifamilia na jumla kwa ajili ya watu unaowajua kuwa wanamaduka.Bei ya mtu ambaye unajua kuwa anaduka inatakiwa iwe tofauti kabisa na bei uliyoibandika kwenye gunia kuwa ni bei ya jumla.Na mfanye mteja ajue kwamba kwako kuna bei fulani za wateule ambazo hazipo kwenye magunia ya mchele hapo utatengeneza wateja permanent,hii phyilosophy kajifunze kwenye maduka ya jumla kkooo
Cha mwisho wewe pita kwenye maduka ya rejareja ukatangaz3 mchele,waachie namba yako waambie wakupigie pindi wanapphitaji mchele ili uwape bei
Nakutakia kazi njema,usikate tamaa maana familia yako inakutegemea.Haya ndio maoni yangu kwako na samahani maana kuna maeneo nimechanganya vimisamiati vya kiingereza ila natumai tumeelewana.
Ushaurii mzuri sana kk nashukur sana
Leo kuna jirani kahama afu pembeni yangu anazidi kunitisha sio pekee angu tu kumbee ninaepitia kipind kigumu
Ila ngoja nikomae
 
Ushaurii mzuri sana kk nashukur sana
Leo kuna jirani kahama afu pembeni yangu anazidi kunitisha sio pekee angu tu kumbee ninaepitia kipind kigumu
Ila ngoja nikomae
Biashara inahitaji uvumilivu mkubwa sana,pigana unavyojua wewe ila siku ukisema unataka kuchange basi hakikisha umepiga hata miaka miwili kwa kuzingatia niliyokwambia.
Ogopa sana kuhama hama location na kudandia business mpya zinazoingia town kabla ya kuisimamisha hiyo uliyonayo.Na baadae utakuja kugundua kuwa hata "chimbo unalochukulia mzigo sio chimbo" zingatia sana hapo nilipoweka hizo alama.
 
Mkuu kwanza nikushauri location uliyopo ndio location sahihi kwa biashara ya mchele.Hii biashara nimezaliwa nimekuta wazazi wangu wanafanya mpaka sasa wanafanya
Biashara ya mchele inahitaji ujanja yaan ubadilike kulingana na mahitaji ya wateja hata kama shamba bei zimepanda jitahidi kutengeneza mchele wa bei ndogo nazani unajua namna ya kutengeneza, kingine tunaelekea kwenye miezi ya 12,1,2na3 hiyo miezi ndio muda wa kupata wateja maana huwa kunakuwa na uhitaji mkubwa wa mchele sababu ya bei.
Sasa hapo jitahidi kuandaa zana kwaajili ya kutengeneza mchele wa bei ndogo maana hicho kipindi wateja huwa hawaangalii uteja wanaangalia wapi kuna bei ndogo.
Kingine kila mteja wa jumla yaani kuanzia kg 50 anaekuja iwe kwabahati mbaya au makusudi hakikisha unachukua namba yake zingatia hilo halafu kila unaposhusha mzigo unawatumia sms au unawapigia kabisa simu kuwaambia mzigo umefika wa bei hii hii na hii hata kama hujashusha mzigo ikipita week tuma sms au piga simu tengeneza urafiki na wateja.
La mwisho biashara inahitaji uvumilivu na muda wa watu kukuzoea pia epuka kufunga funga ofisi yako wateja watajua haupo serious na kazi hata kama unafata mzigo tafuta mtu wa kumwachia usifunge ofisi.
Kwa uzoefu wangu maeneo sahihi kwa biashara ya nafaka yaan mchele ni tandika, mbagara, gongolambo,kawe na maeneo yote wanaopenda kuvaa madela 😂. (Sehemu zenye jamii ya waislamu wengi) All the best
 
Biashara inahitaji uvumilivu mkubwa sana,pigana unavyojua wewe ila siku ukisema unataka kuchange basi hakikisha umepiga hata miaka miwili kwa kuzingatia niliyokwambia.
Ogopa sana kuhama hama location na kudandia business mpya zinazoingia town kabla ya kuisimamisha hiyo uliyonayo.Na baadae utakuja kugundua kuwa hata "chimbo unalochukulia mzigo sio chimbo" zingatia sana hapo nilipoweka hizo alama.
We jamaa unakitu kwenye chimbo hapo umenena mimi bado cjalifahamu chimbo la kuchukua mzgo ili kushindana na ushindani mkubwa huu nilionao aisee
 
Biashara inahitaji uvumilivu mkubwa sana,pigana unavyojua wewe ila siku ukisema unataka kuchange basi hakikisha umepiga hata miaka miwili kwa kuzingatia niliyokwambia.
Ogopa sana kuhama hama location na kudandia business mpya zinazoingia town kabla ya kuisimamisha hiyo uliyonayo.Na baadae utakuja kugundua kuwa hata "chimbo unalochukulia mzigo sio chimbo" zingatia sana hapo nilipoweka hizo alama.
We jamaa unakitu kwenye chimbo hapo umenena mimi bado cjalifahamu chimbo la kuchukua mzgo ili kus
Mkuu kwanza nikushauri location uliyopo ndio location sahihi kwa biashara ya mchele.Hii biashara nimezaliwa nimekuta wazazi wangu wanafanya mpaka sasa wanafanya
Biashara ya mchele inahitaji ujanja yaan ubadilike kulingana na mahitaji ya wateja hata kama shamba bei zimepanda jitahidi kutengeneza mchele wa bei ndogo nazani unajua namna ya kutengeneza, kingine tunaelekea kwenye miezi ya 12,1,2na3 hiyo miezi ndio muda wa kupata wateja maana huwa kunakuwa na uhitaji mkubwa wa mchele sababu ya bei.
Sasa hapo jitahidi kuandaa zana kwaajili ya kutengeneza mchele wa bei ndogo maana hicho kipindi wateja huwa hawaangalii uteja wanaangalia wapi kuna bei ndogo.
Kingine kila mteja wa jumla yaani kuanzia kg 50 anaekuja iwe kwabahati mbaya au makusudi hakikisha unachukua namba yake zingatia hilo halafu kila unaposhusha mzigo unawatumia sms au unawapigia kabisa simu kuwaambia mzigo umefika wa bei hii hii na hii hata kama hujashusha mzigo ikipita week tuma sms au piga simu tengeneza urafiki na wateja.
La mwisho biashara inahitaji uvumilivu na muda wa watu kukuzoea pia epuka kufunga funga ofisi yako wateja watajua haupo serious na kazi hata kama unafata mzigo tafuta mtu wa kumwachia usifunge ofisi.
Kwa uzoefu wangu maeneo sahihi kwa biashara ya nafaka yaan mchele ni tandika, mbagara, gongolambo,kawe na maeneo yote wanaopenda kuvaa madela 😂. (Sehemu zenye jamii ya waislamu wengi) All the best
Unajua biashara ya mchele siriii imejificha kwenye sehem za kununua mchele basiii huko ndo siri ya wanaofanikiwa na wanaofelii ilipo
 
We jamaa unakitu kwenye chimbo hapo umenena mimi bado cjalifahamu chimbo la kuchukua mzgo ili kus

Unajua biashara ya mchele siriii imejificha kwenye sehem za kununua mchele basiii huko ndo siri ya wanaofanikiwa na wanaofelii ilipo
Naumiza kichwa kupata machimbo ambayo bei itakuwa rafiki nakosa kabisa aiseee
 
Yap 100%. Nilijaribu kumwelezea na mimi sema sikufunguka vizur. Ishu za kibiashara zipo kiroho sasa aangalie wapi pa kwenda na kufanikiwa. Pia ajitathimin yeye mwenyewe sio kila mtu anaweza kuwa mfanyabiashara ndo maana unaweza mpa mtu hata 100M ikafa yote.
Kabla ya kuingia kwenye biashara aangalie hayo mambo uliyomfafanulia hapo juu.
Uko sahihi mkuu
 
Habarii wana JF natumai wote mko salama.

Mimi ni mfanyabiashara wa mchele hapa Dar es Salaam
Nauza jumla na rejareja.

Ila nasikitika toka nifungue hiii baishara yangu nimepitia changamoto nying sana mpka leo na nimekuwa mtu ambaye sikatii tamaa nikijipa moyo kwamba ndo napata experience maana ndo mara yang ya kwanza hii biashara.

Lakini changamoto amabyo imenipelekea kuandika huu uzii ni hapa ambayo nimetumia njia zote nimeshindwa biashara naiendesha kwa hasara sipatii faida hata kidg na basi ikipatikana inakuwa ni ndgo sana..

Hiyo changamoto ni kwamba kila nikileta mchele kweny store yang wateja wanarukaruka kwamb mchele wanaona siyo mzurii najitahidii kugradee jambo amablo linapelekea faida yang yote kuishia huko ilimradii tu niwateke wateja kwa vitu vizurii lakini wapi nimejikuta napoteza mtaji wang nusu nzima mpka sasa.

Na kingine mimi nipo mbagala dar es salaam nzima wanasifia mbagala kuuza mchele bei rahisii ni kwelii huku bei ni rahissiii jana nimetoka nimeenda sehem nyingine nimekuta mchele naouza mimi huku 1400 wao wanauza 1600
Sasa niko nawaza nifunge hapa flemu nikatafute sehem nyingine niendelezee baishara hiii hii ya mchele au nitafutee tu biashra nyingine nifanye naomba mnisadie sana.

Ushaurii wenu unahitajika hii biashara hemu imagine miezii saba sasa haijawah kunipa faida hata kidg nimevumilia nimechoka nahisii napoteza tu kila siku.

Maduka ya mchele sasa yamejaa kila kona kila mtu anauza mchele, na wakulima hawajkaa mbalii kila mkoa unalima mchelee.

Miaka yotee huu mwezii wa tisaa michele inapanda bei ila mwaka huu mpka mchele wa 1300 ninao mimi ofisini afu baishara haiendii kabisa yaniii

Nitafute eneo linginee au nibadilishe baishara msaada wenuu wakuu
Tafuta sehemu nyingine kama vile amabayo ni ya kishua kidogo.
 
Jaribu kumix mchele kama wengine huenda bei ukaenda nao sawa, wanatuchanganyia super na Chenga kidogo halafu inaandikwa super *****
 
Back
Top Bottom