Nape: CHADEMA wamepewa fedha na wazungu kuvuruga mchakato wa katiba

Nape: CHADEMA wamepewa fedha na wazungu kuvuruga mchakato wa katiba

Sasa nyie ndo wenye dola iweje mje mlalamike kwenye mkutano wa hadhara badala ya kuwachukulia hatua ilihali mna taarifa muhim kama hizo.

Mi naona hizo ni stori za kutunga tu,Mmeumbuka maana mchakato huo mnataka kuhodhi kwani wakwenu peke yenu? Kila kitu tulikiona bungeni, Tusubiri 2015,Tatizo lenu CCM mnatuona sisi mazezeta hatujui kitu kinachoendelea
 
Kwa hiyo CHADEMA walipewa hela ili waingize ajenda ya katiba mpya kwenye ilani yao ya uchaguzi, Kisha wakapewa hela ili Waisukume ajenda hiyo japo wao hawakushinda uchaguzi, Basi wakafanikiwa kuisukuma kwa ufanisi mkubwa, na sasa wamepewa hela ili waivuruge, na sasa washaanza kuivuruga?

Pengine mwenye majibu ya maswali haya anisaidie na mimi nipate kufahamu; CHADEMA walianza kupewa hela toka walipokuwa wakiandaa ilani ambapo katiba mpya ilikuwa ndani yake au wamepewa juzi tu walivyotoka bungeni? Ikiwa walipewa toka mwanzo; aliekuwa kawapa awali ndo huyo huyo kawapa juzi au ni mtu wengine!

Kama majibu hayapo; Rejea dalili za CHAMA kinachoelekea kufa kwa maelezo zaidi kuhusu anachoongea Nape..
 
Yaani kuna watu mpaka leo wanachukulia kauli za Nape seriously? Really?
 
Mkuu, kwa kuwa Nape ni kiongozi wa chama tawala, kauli yake si ya kubeza hata kidogo. huwezi jua ana ushahidi kiasi gani katika hilo. sote tutafakari kwa pamoja

Sasa wao si wangekwenda mahakamani sasa wanalalama nini?
 
Huyu jamaa ni punguani sana, huyu haaminiki, alikuwa wapi kutueleza kabla ya tukio kutokea? hawa wanatafuta pakujifichia,

siasa za Tanzania ni za kijinga sana na ni za watu wajinga waliobaka siasa, sio kila mtu anafaa kuwa mwanasiasa bhana, Kila

likitokea tukio lazima suala fulani litafutwe ili kuwapoteza watanzania, na baadhi ya watanzania wamekuwa ni bendera tu

wanapelekeshwa na wanasiasa uchwara, Lazima siasa zetu zibadilike, Nape, Mwigulu na wengine kama hawa lazima waelewe

kuwa hii nchi si yao peke yao.

CCM ndo ina serikali, polisi, jeshi, usalama, magereza, Takukuru nk. nijuavyo siasa za Tanzania kama ingekuwa kweli ungeona

hivi vyombo, Mbona Kinana alienda China akakaa muda mrefu? mbona Mwigulu alienda China akaja na Bomu la Arusha? kwani

hivyo vyombo havikujua? Shame on him!!! wala chadema msijibu chochote huyu ni sisimizi, lengo lao wanataka kuwagawa

wapinzani ambao tayari wameungana kwa swala hili.
 
Tunaomba awe waz basi..hizo pesa wanatoa wap.!?

Nape mwenyewe anasema amesikia CDM wamepewa fedha na wafadhili wao ili kuvuruga mchakato wa katiba mpya. Kwa maana nyingine Nape hana uhakika na analosema, ni mambo ya kusikia mitaani (umbeya). Kama anaamini anachokisema ni ukweli basi aseme hao wafadhili ni akina nani na wa nchi gani, walitoa kiasi gani, nani alipokea hizo fedha ndani ya CDM, ikaingia akaunti ya nani, akaunti namba gani na benki ipi? Nape akishathibitisha hayo, vielelezo viende kwenye vyombo vya dola kwa hatua zaidi. Tofauti na hayo Nape atakuwa kiongozi mp.u.m.ba.v.u kwa sababu anapotosha umma kwa siasa za kipuuzi.
 
Duh kumbe fedha toka ughaibuni ndizo zinarusha chopper angani?

Pamoja na anti-money laundering measures zote hizo pesa zinaingiaje hapa nchini? Serikali si izi freeze kama kweli zinakuja kwa nia ya kuharibu mchakato wa katiba.
...hapo mkuu umenena. labda anataka kutuambia Dr alikuja nazo kwenye magunia kama yale madawa ya kulevya ya "Masogange" akapita nayo airport na anazitunza nyumbani kwake?
Kama hayo yanafanyika na serikali inashindwa kudhibiti basi wawaachie serikali wanaoweza kudhibiti fedha haramu.
 
Huyu Nape na yeye alishafilisika kisiasa! Kabla ya kutoa tuhuma hizi anapaswa kututhibitishia tuhuma za nyuma alizowahi kuzitoa dhidi ya Cdm! Na Kama hawezi sisi tunamuona Kama Vuvuzela!
 
Katiba ilikuwa ni agenda ya wapinzani.

Serikali na dola ni vya CCM, so ingeweza kuzuia fedha haramu kuingia nchini.

Vyombo vya Dola havijui km kuna adui mkubwa nje mwenye nia ya kuleta machafuko nchini? Nape wasaidie kuwajua.

Msajili wa Vyama vya siasa anaielea CHADEMA na kumletea usumbufu aliyemteua? Si akifutilie mbali kutokana na tuhuma zoooote za Nape, Wassira, Lukuvi na Mwigulu?

Nchi wakoloni wetu...Membe anasubiri nini kuwasulubu mabalozi wa nchi hizo hapa nchini kwa kutuletea balaa kubwa?

My take:
Imefika wakati CHADEMA kupitia Lissu waandae na kuwasilisha muswada wa kusema uongo (Ant-Lie Bill) Bunge lijalo ili kukomesha akina Nape na wale wanaokana mashtaka halafu ushahidi ukathibitisha.
 
~ Adai ndio chanzo cha kupigana bungeni
~ Asema ndizo walizotumia kuzunguka na helkopta nchini.
~ Aeleza yaliyotokea sio bahati mbaya, Chadema waliyapanga
~ Ashukuru bunge kuendelea kuonyeshwa "live" ili wananchi waone ujinga wao.
~ Awatuhumu kuweka masilahi yao mbele badala ya nchi.
~ Asisitiza CCM kuendelea kuheshimu uamuzi wa wananchi juu ya katiba.
~ Aonyesha madai ya Chadema kitakwimu yasivyojali wakulima na wafanyakazi.


Katibu wa NEC ya CCM itikadi na Uenezi Nape Nnauye amesema kinachowasumbua Chadema mpaka wanafanya yote waliyoyafanya hasa ngumi na vurugu bungeni ni namna watakavyoeleza kwa waliowapa pesa za kuvuruga mchakato wa katiba nchini kwani wanatakiwa kupeleka mrejesho jinsi walivyofanikiwa na jinsi walivyotumia mabilioni hayo.

Nape ameyasema hayo kwenye mkutano mkubwa wa hadhara mjini Kahama kwenye ikiwa ni sehemu ya ziara ya wilaya zote za mikoa ya kanda ya ziwa ya Shinyanga, Simiyu na Mara ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndg. Abralhaman Kinana.

"Wenzetu hawa nasikia wamepewa mabilioni toka nje kwa kisingizio cha kushiriki mchakato wa katiba, na kama ilivyo kwa vibaraka wengine katika bara la Afrika lengo la mapesa hayo sio kuwawezesha kushiriki bali kuanzisha fujo na vurugu ili mchakato usimalizike salama iwe ajenda 2015 kwani kimsingi hawana ajenda mpya" alisisitiza Nape.

Akifafanua juu ya suala la pesa kutoka nje Nape alisema mara tu baada ya rasimu ya kwanza kutoka Katibu Mkuu wa Chadema Dk. Wilbroad Slaa alikwenda nje ya nchi na akakaa kwa muda na aliporudi tu, ndio Chadema wakapanga kuanza kuzunguka na helkopta.

"Babu atwambie alifuata nini nje? Na pesa za kuzunguka na misafara miwili tofauti ya helkopta walitoa wapi? Na watwambie kama walisharudisha mrejesho kwa wafadhili wao" alisema Nape

Nape alisisiza kuwa yote yaliyotokea bungeni si mambo yaliyotokea kwa bahati mbaya isipokuwa ni mambo yaliyopangwa na Chadema katika mkakati wa kutimiza moja ya malengo yao.Alisema ilikua ni lazima watafute mahali pa kufanya kituko bungeni ili iwe mjadala na ili wapate sababu na picha za kuonyesha kwa waliowapa pesa kuwa wanapambana.

"Hili walilofanya Chadema bungeni ni jambo walilopanga katika mkakati wao wa 'civil disobidiency' ...machafuko ya umma dhidi ya dola, mkakati ambao unaratibiwa kutoka nje na baadhi ya wale waliokuwa wakoloni katika nchi zetu za Afrika. Lengo ni kusababisha machafuko na nchi kutotawalika" alisema Nape.

Nape alisema ndio maana CCM ilisisitiza lazima bunge liendelee kuonyeshwa na televisheni ili kuonyesha yanayoendelea bungeni kuwawezesha wananchi kuona kinachofanywa na wawakilishi wao.
"bila shaka wananchi mmeona kilichotokea bungeni kwa macho yenu, sina haja ya kuwaeleza. Mmeona wabunge wa upinzani walichofanya,uchaguzi ujao tupunguze idadi ya wau wasio na maadili bungeni ili kodi zetu zitumike vizuri,kwani tuliwatuma wakajadili maendeleo yetu wao wamegeuza bunge uwanja wa masumbwi.

Aidha Nape akifafanua hoja ya upinzani bungeni juu ya idadi ya wabunge wa bunge maalum la katiba alisema upinzani hawana hoja ya msingi bali wanasukumwa na ubinafsi na ulafi wa madaraka.

"Hoja iliyowafanya wapigane bungeni haina mashiko, wanataka idadi iongezwe ya wabunge wa bunge la katiba kutoka 357 mpaka 792. Hivi nani anabeba mzigo huu wa kuwalipa hawa wabunge kama sio mwananchi wa kawaida? Halafu mnajiita watetezi wa wanyonge? Hawaoni aibu?" alihoji Nape.

Akiendelea kufafanua Nape anasema,"Katika hali ya kawaida tungetegemea wajenge hoja ya kundi kubwa katika jamii ya kitanzania ambao ni wakulima na wafanyakazi ndio wawe na uwakilishi mkubwa kwenye hilo bunge kama tunataka katiba kweli ya wananchi lakini badala yake wao wanapendekeza wawakilishi kutoka vyama vya siasa ukiacha wabunge waliopo sasa wawe 72 na wakulima wawe 10 tu! Wanataka katiba ya vyama vya siasa badala ya katiba ya nchi kwa ajili ya wananchi. Wanataka wafugaji wawe 10 tu na wafanyakazi 40. Kwa uwiano wa kawaida asilimia 80% wa wananchi wa nchi hii ni wakulima, tungetegemea wangependekeza idadi yao kuwa kubwa lakini wao wanawapuuza wakulima na wafugaji kwa kudai wawe kumi tu"!

Nape alimalizia kuwa siku za vyama kama Chadema zinahesabika maana hii ya katiba ndio ilikuwa karata yao ya mwisho.

Amevitahadharisha vyama vingine vya siasa kama CUF, NCCR mageuzi na wengine kuwa wenzao wamepewa mapesa wao wanawaunga mkono kwa ajenda iliyojificha. Na kwa kuwa hili la kuvuruga katiba ndio karata yao ya mwisho basi tutarajie anguko baya sana kwa Chadema na huo ndio utakuwa mwisho wao!


kwa bahati mbaya nape ni kijana mwenzetu lakini anatuaibisha, anazungumza kama vuvuzela ambalo hata kichaa anaweza kulipuliza. nape atuambie je yale maoni waliyotoa upinzani hayana mantiki, arudie kusoma kwa makini kisha ajibu kila hoja liyotolewa, asilete siasa nyepesi
 
Nape mwenyewe anasema amesikia CDM wamepewa fedha na wafadhili wao ili kuvuruga mchakato wa katiba mpya. Kwa maana nyingine Nape hana uhakika na analosema, ni mambo ya kusikia mitaani (umbeya). Kama anaamini anachokisema ni ukweli basi aseme hao wafadhili ni akina nani na wa nchi gani, walitoa kiasi gani, nani alipokea hizo fedha ndani ya CDM, ikaingia akaunti ya nani, akaunti namba gani na benki ipi? Nape akishathibitisha hayo, vielelezo viende kwenye vyombo vya dola kwa hatua zaidi. Tofauti na hayo Nape atakuwa kiongozi mp.u.m.ba.v.u kwa sababu anapotosha umma kwa siasa za kipuuzi.

Muacheni Jamani Nape aendelee kukiua chama chake kwa kuaniaki madhaifu ya Serikali inayoongozwa na chama chake! Kwasababu hii itakua kashfa kwa serikali watu kuingiza mafwedha na kufadhili vyama vya siasa bila ya Serikali ambayo ndo mmiliki wa taasisi zote za kibenki Na kifedha kufahamu! Hii inaonesha ata Kule Hazina kuu hakuna usawa!
 
serekali ya ccm ...ipo wapi kuchukua hatua...! wanaidhalilisha ccm kweli...
 
mkuu, Nape ni kiongozi wa chama tawala ambacho kina mikono mirefu. hivyo kauli ya Nape si ya kupuuzwa wala kuingiziwa mizaha. watanzania tutafakari kwa pamoja na hawa wanasiasa uchwara ambao wanazoea kutumiwa kuvuruga nchi yetu tuwakatae kabisa
...hiyo mikono mirefu si ingezikamata hizo pesa haramu? au serikali ni dhaifu?
 
Nape ni vuvuzela wa ccm. Hana jpya hapa. Maneno ya Nape yangetolewa na karani tu wa John Mnyika, saa hii angekuwa central kuutoa ushahidi, lakini kwa kuwa yametolewa na Vuvuzela wa ccm, hakuna anayemwona kwani hiyo ndio sera yao.
Kwa nini Usalama wa Taifa wanajifedhehesha hivi? Yaani mabilioni yaingizwe nchini, sijui kwa mabox au kwenye account gani lakini mshindwe kuuliza walizipata wapi? Mpaka Nape amewaamsha lakini bado hamjachukua hatua?? Kweli dunia mhhhh.
Afadhali Nape hakusema Dr. Slaa alikwenda kuuza kitu huko amesema alienda kuomba msaada, Mwenye kiti wa ccm anazunguka kwenda kuomba Neti za kuzuia nzi wale wakubwa akaambiwa ati ni za kuzuia mbu. Jamani, namwonea huruma.
Pita mitaani, watu wamezifanya za kuzuia kuku wasiliwe na mwewe. Dah!
Pole sana Nape.
CCm mnawalinda wauza Sembe, waziri anasema, Hakuna mbunge wa ccm atakayepona wakitajwa! Maajabu gani haya??
nji hii.
 
Huyu Nape akili mbovu tu kama za Ritz na post yake ya uongo jana kuwa Dr. Slaa anakwepa kodi.
Hovyo kabisa mtu mzima tena mwanaume unakuwa mmbeya! Kwahiyo ndio CDM walimroga Ndugai akawa mpuuzi na kutoa maamuzi ya kijinga kama yale? Aisee....Ndio maana alifeli Civics huyu.

mbona maneno yako hayana mtiririko unaoeleweka. unarukaruka tu! mara hili mara lile. subiri viroba vimalizike kichwani ndiyo uchangie
 
Back
Top Bottom