Nape Nnauye: Kiroboto ulishindwa akiwepo godfather, utaweza leo?

Jambo usilolijua ni kama usiku wa giza, watu wengi humu JF hawaelewi hata nini kinaendelea kuhusu hii movie.

Ngoja leo hapa JF nifungue code chache.

Sote tunapaswa kujua kuwa kuna vita kubwa sana ya kimaslahi ndani ya CCM kwa sasa baada ya Magufuli kufariki dunia. Vibaraka wote wa JPM wamepangwa kunyofolewa kwenye madaraka ya serikali na chama ili vibaraka wa Hangaya (JK) washike hatamu. Anachokifanya Hangaya ni kutimiza mapatano ya uhuni wa 2015 uliofanywa na JK kupitia genge lake (akiwemo Nape, January, Kinana, Makamba nk) uliohakikisha ufalme haiendi kwa mmasai wala hauendi upinzani kwa kutumia koti la kisukuma (JPM). Alichokifanya JPM baada ya kuingia madarakani kilikuwa kiko kinyume na mapatano ya kupewa urais wa dezo na genge la Msoga, ule ulikuwa ni uasi dhidi ya JK. Huo ndio ukweli wa kwanza.

Ukweli wa pili ni kuwa, Pole Pole ndio mjumbe rasmi wa kuongea mbele ya umma kuwakilisha Sukuma gang. Pole Pole anatumika kutishia, kutikisa kiberiti na kutuma ujumbe dhidi ya utawala wa Msoga gang. Wale wote waliokuwa ndani ya utawala wa JPM na kwa sasa wako kimya, basi mdomo wao wa kusemea ni Pole Pole. Ukiona ngedere mjini basi ujue kuna mtu anamfuga!

Ukweli wa tatu ni kuwa Pole Pole yuko mbioni kufukuzwa, kusimamishwa au kufungwa mdomo kisiasa (kupewa cheo cha kufungwa mdomo kama ubalozi, RAS nk) na utawala wa sasa, na tayari hilo ameshalijua, press yake ya leo ilikuwa ni "Political strategy" ya kuwatisha watawala waogope kuchukua hatua walizozipanga au wakizichukua iwe more advantage kwake kisiasa, hiyo inaitwa Pre emptying approach. Tetesi za kusema leo Pole Pole alikuwa ajivue uanachama wa CCM mbele ya vyombo vya habari zilianzishwa na team ya Pole Pole, kimakusudi na kimkakati ili kutisha na kupima upepo wa watawala wa sasa. Ni mbinu ya kisiasa.

Ukweli wa nne ni kuwa Nape ndio mwanasiasa aliyepangwa rasmi na Msoga gang kujibizana na Pole Pole kwa sasa. Anachokifanya sasa Nape sio bahati mbaya, ni jambo limepangwa na analitekeleza. Muda sio mrefu Nape naye atakuwa na vipindi vya tv na platform za kuongea mitandaoni. Yaani ngedere atajibiwa na ngedere, maana wote wako mjini wanafugwa!

Mwisho kabisa ni kuwa Nape anarudishwa tena serikalini, muda sio mrefu, na huenda akarudishwa wizara ile ile aliyotolewa au kwenda wizara fulani mpya iliyoanzishwa na Magufuli ikihusika na wizara ile ile aliyokuwepo Nape.
 
Yah hii demokrasia ya kurithishana mikoba kama waganga wa jadi haitufai
Hi hivi unajua Watanzania wengi hawajui maana ya democracy.

Democracy ni utawala wa wengi, tatua matatizo ya wengi, weka mazingira watu wapate riziki kodi, tozo sahihi.

Hakikisha umeme, maji upo siku zote, thibiti mfumuko wa bei. Kuna wizara inaitwa ya mipango na fedha.

Hivi wanapanga nini, wanawasaidiaje wengi,vijana, maskini, kuwawezesha kusimama.
 
Kiroboto aka Punda hahahaaaaaaa..
 
Pole pole atulie tu hawawezi watoto mjini waswahili kwa fitina wako vizuri kama kweli magufuli yalimshinda na ndiye Rais na kila kitu hayupo sembuse yeye, ndio maana Nape kamjibu kuwa yeye ni kiroboto tu atulie.
Ukishindana na mwenye power utaumia
 
Serikali ya CCM ni failure, katika mambo critical hutolewa majibu mepesi tu na huwa lazima muyakubali tu!
 

Ni hivi France waliua Wafalme na wazazi, vizazi vyao vyote, watu wao wa karibu wote, wakaanza upya, katibs mpya 1890 huko, kwamba hatutaliwa tena na familia moja,mbili, kumi .

UK waliwapa nguvu walalahoi, wanawake, watumwa. Kupunguza nguvu zao.

US ni wakimbizi watu wa Ireland, Ulaya, Protestant, waliokuwa second class citizens, maskini.

Walitaka uhuru.
 
Ila CCM hawajua kinachoendelea mtaani sio? Wafanye tafiti kuna chuki sana inajengeka...watakuja washangae akitokea mwanasiasa ana nguvu...watashangaa sana watu kama kina Nnape. Just someone to ignite

Sahihi sana
 
Binafsi sioni wa kumlaumu ,Kama biniadamu asilimia kubwa tumeumbiwa roho za chuki na kisasi hasa kwa watu tunaohisi walikuwa chanzo Cha matatizo yetu.

Nape anatema nyongo iliyomkaa kwa miaka kadhaa,hivyo hivyo itakuwa kwa polepole siku dunia ikifanya turn up na kutoa nafuu kwake.
 
Mjinga katudharau watanzania wote kwa hii kauli yake.

Siku zote wanajiona, wanafikiri wamezaliwa kutawala. Katiba mpya itasaidia kuondoa huu upuuzi wa kupendelea wachache, jina la baba yako, unanijua mimi ni nani.

Itawapa fursa vijana wenye akili, maono, wanaolipenda taifa kuweka maslahi ya taifa mbele.

Wanasahau wazee, baba zao, Enzi zile wote waliikuwa ila wazelendo wa ukweli.

Maskini sana wa mali, lakini walijali jamìi,nchi yao, Afrika, amuangalie baba yake, ajifunze.
 
Nape naye alisimamia sakata la Makonda na Clouds hadi akapoteza uwaziri!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…