Determinantor
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 59,045
- 94,974
Naunga mkono hoja na sitaki Mtu yeyote atukanwe maana matusi hutweza.Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknoloji ya Habari, Mhe. Nape Nnauye (Mb) amewataka watanzania kutotumia lugha za matusi kukosoa jitihada mbalimbali zinazofanywa nchini na Rais wa Serikali ya Awamu ya Sita, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Waziri Nape ameyasema hayo leo Julai 18 Mkoani Dar es Salaam alipokuwa akizungumza Katika Kongamano la Majadiliano ya Ripoti ya Tume ya Haki Jinai lililohudhuriwa na Wataalamu, Viongozi Wastaafu, Watumishi wa Serikali na Wanafunzi.
Nape amesema kuwa Rais Samia alipowaapisha Viongozi wa Wizara ya Mipango na Uwekezaji amewataka Viongozi hao wawasikilize wakosoaji wote na ikiwezekana wawajumuishe kwenye michakato mbalimbali ya kuboresha mambo mbalimbali katika nchi yetu na kusema kuwa kitendo cha baadhi ya wananchi wakiwemo wanasiasa kutumia lugha zisizofaa wanapotoa maoni yao sio sawa.
“Tukosoane, turekebishe, tutoe maoni bila ya kutukanana. Baba wa Taifa Mwalimu Nyerer alitufundisha tukosoane kwa hoja bila ya kutukanana. Kosoeni, toeni maoni, msidhalilishane na wala msitukanane na hasa inapokuwa ni Rais wa Nchi yetu mana yeye ni sura yetu sote”. Amesema Nape
“Kutukanwa kwa Mama ni kosa na hata kama hajakuzaa moja kwa moja unapomtukana basi ni sawa na kutukanwa kwa wazaza wote, tunao wajibu wa kuwaadhibu wote wanaotukana wazazi wa Nchi hii, kwani wazazi hawa wametulea, wametutunza, wametufikisha hapa tulipo salama na tusisahau kuwa utamaduni wa nchi yetu ni kuheshimiana” Ameongeza Waziri Nape.
Waziri Nape pia amempongeza Rais Samia kwa nia yake ya dhati kutaka kuona haki ikitendeka nchini na kusema kuwa mageuzi anayofanya katika kuboresha na kukusanya maoni ya watanzania kuhusu maboresho ya taasisi zinatoa haki nchini.
“Tunaposhuhulika na Haki Jinai, moyo wa Rais unataka haki. Haki italiinua Taifa letu,” amesema Nape.
1.Tuna raisi mshamba mno kuwahi kutokea- ZZKHakuna tatizo lolote kumkosoa Mama, ila lugha iwe ya staha Heshima kitu cha bure! Kwanini Rais Samia, japo sio lazima apendwe na wote lakini ni lazima aheshimiwe na wote? Akosolewe kwa staha na asitukanwe!
P
Kuwakamata watu siyo solution solution ni kukaa chini kama taifa na kushindanana kwa hojaNaunga mkono hoja na sitaki Mtu yeyote atukanwe maana matusi hutweza.
Lakini kusema "Hizi ni akili au matope" ni kauli ya kuonyesha uwezo wa chini wa kufikiri na si tusi.
Pia si kweli kwamba nikimaambia Anna Tibaijuka kwamba ana uelewa mdogo basi ndo nimewaambia wanawake wote. Hii dhana ya kulazimisha Samia aonekame Mwakilishi wa wanawake wote duniani imepitishwa na Bunge la CW au la SADC?
Lisu ndio mjanja?!!Tukiachana na Nape,Ila jamaa ushamba ulimzidi hadi kimo.
Hilo la ushamba wa yule dhalim halina ubishi.Tukiachana na Nape,Ila jamaa ushamba ulimzidi hadi kimo.
Mama mmoja akiuza bandari zetu maana yake akina mama wote wamauza bandari zetu za Tanganyika?Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknoloji ya Habari, Mhe. Nape Nnauye (Mb) amewataka watanzania kutotumia lugha za matusi kukosoa jitihada mbalimbali zinazofanywa nchini na Rais wa Serikali ya Awamu ya Sita, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Waziri Nape ameyasema hayo leo Julai 18 Mkoani Dar es Salaam alipokuwa akizungumza Katika Kongamano la Majadiliano ya Ripoti ya Tume ya Haki Jinai lililohudhuriwa na Wataalamu, Viongozi Wastaafu, Watumishi wa Serikali na Wanafunzi.
Nape amesema kuwa Rais Samia alipowaapisha Viongozi wa Wizara ya Mipango na Uwekezaji amewataka Viongozi hao wawasikilize wakosoaji wote na ikiwezekana wawajumuishe kwenye michakato mbalimbali ya kuboresha mambo mbalimbali katika nchi yetu na kusema kuwa kitendo cha baadhi ya wananchi wakiwemo wanasiasa kutumia lugha zisizofaa wanapotoa maoni yao sio sawa.
“Tukosoane, turekebishe, tutoe maoni bila ya kutukanana. Baba wa Taifa Mwalimu Nyerer alitufundisha tukosoane kwa hoja bila ya kutukanana. Kosoeni, toeni maoni, msidhalilishane na wala msitukanane na hasa inapokuwa ni Rais wa Nchi yetu mana yeye ni sura yetu sote”. Amesema Nape
“Kutukanwa kwa Mama ni kosa na hata kama hajakuzaa moja kwa moja unapomtukana basi ni sawa na kutukanwa kwa wazaza wote, tunao wajibu wa kuwaadhibu wote wanaotukana wazazi wa Nchi hii, kwani wazazi hawa wametulea, wametutunza, wametufikisha hapa tulipo salama na tusisahau kuwa utamaduni wa nchi yetu ni kuheshimiana” Ameongeza Waziri Nape.
Waziri Nape pia amempongeza Rais Samia kwa nia yake ya dhati kutaka kuona haki ikitendeka nchini na kusema kuwa mageuzi anayofanya katika kuboresha na kukusanya maoni ya watanzania kuhusu maboresho ya taasisi zinatoa haki nchini.
“Tunaposhuhulika na Haki Jinai, moyo wa Rais unataka haki. Haki italiinua Taifa letu,” amesema Nape.
Bora akumbushwe tu ,naona amelewa madaraka na tumbo Lake kama pipaAlimuita Magufuli mshamba, je akitukana wababa wote? Au wakati huo kukosoa kwa staha haikuwa lazima?
Nape anaakili ndogo Hawezi kukumbuka mpaka awekewe tapeHuyu kiribatumbo amesahau kuwa alimuita Magufuli mshamba?
Huyu anastahili maneno magumu zaidi na mambo mengine Raisi anajitafutia tu yy mwenyewe adhabu za kisiasa ,kama hili la DPHivi ni rais huyu tu ndio anatukanwa na wengine hawakuwa wakitukanwa au inaonekana ni vibaya kumtukana rais huyu kwa sababu ni mwanamke?
Bosi wake na yey nape wanafananaNape ni Waziri wa hovyo kabisa kuwahi kutokea, sijui ni ushirikina tu unambeba?
Wote ni vilazaBosi wake na yey nape wanafanana