Nape Nnauye: Tukosoane kwa hoja na lugha za staha. Kutukanwa kwa mama mmoja ni kutukanwa kwa kina mama wote Tanzania

Nape Nnauye: Tukosoane kwa hoja na lugha za staha. Kutukanwa kwa mama mmoja ni kutukanwa kwa kina mama wote Tanzania

CCM wanataka kuhamisha goli, walikuja na hoja ya ubaguzi imebuma, wakaja na hoja ya udini imegoma kupokelewa, sasa wanakuja na hoja ya muuza nchi eti anatukanwa. Huyu mama na Mbarawa wamefanya jambo la kijinga sana na mtu kuitwa mjinga sio tusi. Tibaijuka ni mwanamke mbona anampinga hadharani Samia, DCI Kingai na Nape ni watu wanaonyesha haja kubwa ya kuwepo na katiba mpya kudhibiti wajinga kupewa ofisi za umma.
 
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknoloji ya Habari, Mhe. Nape Nnauye (Mb) amewataka watanzania kutotumia lugha za matusi kukosoa jitihada mbalimbali zinazofanywa nchini na Rais wa Serikali ya Awamu ya Sita, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Waziri Nape ameyasema hayo leo Julai 18 Mkoani Dar es Salaam alipokuwa akizungumza Katika Kongamano la Majadiliano ya Ripoti ya Tume ya Haki Jinai lililohudhuriwa na Wataalamu, Viongozi Wastaafu, Watumishi wa Serikali na Wanafunzi.

Nape amesema kuwa Rais Samia alipowaapisha Viongozi wa Wizara ya Mipango na Uwekezaji amewataka Viongozi hao wawasikilize wakosoaji wote na ikiwezekana wawajumuishe kwenye michakato mbalimbali ya kuboresha mambo mbalimbali katika nchi yetu na kusema kuwa kitendo cha baadhi ya wananchi wakiwemo wanasiasa kutumia lugha zisizofaa wanapotoa maoni yao sio sawa.

“Tukosoane, turekebishe, tutoe maoni bila ya kutukanana. Baba wa Taifa Mwalimu Nyerer alitufundisha tukosoane kwa hoja bila ya kutukanana. Kosoeni, toeni maoni, msidhalilishane na wala msitukanane na hasa inapokuwa ni Rais wa Nchi yetu mana yeye ni sura yetu sote”. Amesema Nape

“Kutukanwa kwa Mama ni kosa na hata kama hajakuzaa moja kwa moja unapomtukana basi ni sawa na kutukanwa kwa wazaza wote, tunao wajibu wa kuwaadhibu wote wanaotukana wazazi wa Nchi hii, kwani wazazi hawa wametulea, wametutunza, wametufikisha hapa tulipo salama na tusisahau kuwa utamaduni wa nchi yetu ni kuheshimiana” Ameongeza Waziri Nape.

Waziri Nape pia amempongeza Rais Samia kwa nia yake ya dhati kutaka kuona haki ikitendeka nchini na kusema kuwa mageuzi anayofanya katika kuboresha na kukusanya maoni ya watanzania kuhusu maboresho ya taasisi zinatoa haki nchini.

“Tunaposhuhulika na Haki Jinai, moyo wa Rais unataka haki. Haki italiinua Taifa letu,” amesema Nape.

Naunga mkono hoja na sitaki Mtu yeyote atukanwe maana matusi hutweza.
Lakini kusema "Hizi ni akili au matope" ni kauli ya kuonyesha uwezo wa chini wa kufikiri na si tusi.
Pia si kweli kwamba nikimaambia Anna Tibaijuka kwamba ana uelewa mdogo basi ndo nimewaambia wanawake wote. Hii dhana ya kulazimisha Samia aonekame Mwakilishi wa wanawake wote duniani imepitishwa na Bunge la CW au la SADC?
 
Naunga mkono hoja na sitaki Mtu yeyote atukanwe maana matusi hutweza.
Lakini kusema "Hizi ni akili au matope" ni kauli ya kuonyesha uwezo wa chini wa kufikiri na si tusi.
Pia si kweli kwamba nikimaambia Anna Tibaijuka kwamba ana uelewa mdogo basi ndo nimewaambia wanawake wote. Hii dhana ya kulazimisha Samia aonekame Mwakilishi wa wanawake wote duniani imepitishwa na Bunge la CW au la SADC?
Kuwakamata watu siyo solution solution ni kukaa chini kama taifa na kushindanana kwa hoja
 
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknoloji ya Habari, Mhe. Nape Nnauye (Mb) amewataka watanzania kutotumia lugha za matusi kukosoa jitihada mbalimbali zinazofanywa nchini na Rais wa Serikali ya Awamu ya Sita, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Waziri Nape ameyasema hayo leo Julai 18 Mkoani Dar es Salaam alipokuwa akizungumza Katika Kongamano la Majadiliano ya Ripoti ya Tume ya Haki Jinai lililohudhuriwa na Wataalamu, Viongozi Wastaafu, Watumishi wa Serikali na Wanafunzi.

Nape amesema kuwa Rais Samia alipowaapisha Viongozi wa Wizara ya Mipango na Uwekezaji amewataka Viongozi hao wawasikilize wakosoaji wote na ikiwezekana wawajumuishe kwenye michakato mbalimbali ya kuboresha mambo mbalimbali katika nchi yetu na kusema kuwa kitendo cha baadhi ya wananchi wakiwemo wanasiasa kutumia lugha zisizofaa wanapotoa maoni yao sio sawa.

“Tukosoane, turekebishe, tutoe maoni bila ya kutukanana. Baba wa Taifa Mwalimu Nyerer alitufundisha tukosoane kwa hoja bila ya kutukanana. Kosoeni, toeni maoni, msidhalilishane na wala msitukanane na hasa inapokuwa ni Rais wa Nchi yetu mana yeye ni sura yetu sote”. Amesema Nape

“Kutukanwa kwa Mama ni kosa na hata kama hajakuzaa moja kwa moja unapomtukana basi ni sawa na kutukanwa kwa wazaza wote, tunao wajibu wa kuwaadhibu wote wanaotukana wazazi wa Nchi hii, kwani wazazi hawa wametulea, wametutunza, wametufikisha hapa tulipo salama na tusisahau kuwa utamaduni wa nchi yetu ni kuheshimiana” Ameongeza Waziri Nape.

Waziri Nape pia amempongeza Rais Samia kwa nia yake ya dhati kutaka kuona haki ikitendeka nchini na kusema kuwa mageuzi anayofanya katika kuboresha na kukusanya maoni ya watanzania kuhusu maboresho ya taasisi zinatoa haki nchini.

“Tunaposhuhulika na Haki Jinai, moyo wa Rais unataka haki. Haki italiinua Taifa letu,” amesema Nape.

Mama mmoja akiuza bandari zetu maana yake akina mama wote wamauza bandari zetu za Tanganyika?
Mama mmoja akileta TOZO basi mama wote wametuletea TOZO,
Mama mmoja akipandisha gharama za bundle la internet basi .......
 
Back
Top Bottom