Napendekeza Rais aliyechaguliwa akifia Madarakani, makamu wake ashikilie nafasi hiyo kwa siku 90 tu kisha uitishwe uchaguzi

wanaongea kwa uhuru gani wakati police wanawaita kujieleza?
Waache Polisi wafanye kazi yao. Enzi za yule mwehu 2015-21 ulikuwa husikii mtu kukamatwa na Polisi bali WASIOJULIKANA!! Na baada ya hapo ni kwenye viroba baharini
 
Utaratibu huu ulikuwepo kabla ya mwaka 1992. Tulipobadilisha Katiba kukubali Mfumo wa Vyama Vingi ndipo utaratibu wa sasa ukawekwa. Marekani na nchi zingine zenye watu wenye akili wanatumia mfumo huu. Kuturudisha nyuma, HAPANA!!!
 
L
Leo mnamuona Nyerere ni mjinga? Aliyetunga hiyo katiba?
 
Mimi napendekeza Usultani tu, Rais wa milele na akitangulia anashika madaraka mrithi ataemchaguwa yeye akiwa hai.
 
Mimi siungi mkono hoja, ila ningependa uteuzi wa Mgombea mwenza uwe serious, siyo huu wa kuokoteza okoteza tu. Mgombea Mwenza awe anatokana na wale waliogombea kwenye primary na wakapata kura nyingi. Ina maana kuwa wazenji wawe wanajitokeza kuwania primary siyo wake kusubiri kuteuliwa kuwa wagombea wenza. Kwenye Uchaguzi wa 2015, nadhani huenda hata Amina (pamoja na mapungufu yake) alistahili zaidi ya huyu.

Halafu rais aliyechaguliwa akifariki angali madarakani basi Makamu wa Rais anamalizia serikali iliyoachwa na marehemu, siyo aruke na kusema kuwa anaunda serikali yake awamu mpya ilhali siyo yeye aliyekuwa amechaguliwa. Kwa mfano, Marekani wakati Kennedy anauwawa mwaka 1963, Johnosn aliendeleza serikali ya Kennedy hadi baada ya uchaguzi mwaka 1964 ndipo akaunda serikali yake.
 
Kwa utaratibu huu, naomba nikuhakkishie kuwa kwa mwaka mmoja unaweza ukaitisha hata chaguzi nne; kwa hiyo hutakaa ukae na Rais kwa sabbabu kwa mwaka kuna siku 360
Au divetaizi ile ya kipindi kile cha CORONA umeisahau?
 

Imepita bila kupingwa!
Iwekwe kwenye KATIBA MPYA.
 
Ahahahahaaaa naona Dp world imewatoa tongotongo watu.

Katiba ni mbaya kwa sehemu kubwa. Hasa mamlaka hayo mkuu wa nchi. Imeumba mungumutu fulani hivi
 
Huwa tunachagua mgombe na mgombea mweza wa urais pamoja
 
Manmaaeee, wagalatia mtaongea lugha zote kkenge nyie
 
Mnalo. Bado mnaye mpaka 2030
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…