Narudia tena, Mafundi gereji msipojiongeza mtaishia kutengeneza gari za mwaka 90

Narudia tena, Mafundi gereji msipojiongeza mtaishia kutengeneza gari za mwaka 90

Mafundi aina zote ni makanjanja na wengi wajinga wasiotaka kujiongeza maisha yao yote
Unakuta mechanics ana garage miaka 30 ila spanner ni zile zile ufundi ule ule na wizi kwenda mbele kwa baadhi

Yaani hawataki kujiongeza hata kuwa na vifaa vya maana
Garage inatakiwa iwe na kila kitu na kuenda na wakati

Wengine ni wajenzi nao hivyo hivyo mjenzi hana hata gari la kubebea vifaa vyake na hata akihitaji kitu
Hawa nao ni masikini tu wasiotaka kujiendeleza

Tatizo wana ujuzi ila hawataki kujipeleka mbele
Utasikia ooh hela hakuna, miaka 30 unasema hela hakuna

Yaani wote hali moja ni njaa tu na wizi na uongo ndio linawafanya wengi wasiendelee na ukiwaambia wanakushangaa
Wanakushangaa kwa kuwa wengi ni wajinga waliokimbilia ufundi. Wizi wizi na ujanja ujanja tu
 
Upo sahihi kabisa mkuu
Unakuta mtu ni fundi cherehani anapata tender mpaka za shule kushona sare na wafanyakazi wake wengi ni wa msimu ila sasa jichanganye umpelekee vitambaa akutengenezee utajuta

Hela amekula na utazungushwa mwezi

Ukienda kwa carpenters nao ndio kabisa unauziwa kochi kalijaza maboksi ukilikalia siku Tatu tu umemezwa na kochi

Ukanjanja kila mahali ndio maana hakuna wanaoendelea huku wakisema ooh foreigners wanatajirika kwa ndagu na kuiba na kujuana na wakubwa

Mtu anafeli maisha hajui anafeli wapi halafu kutwa kwa mganga
Inatakiwa shule wafundishwe sana maisha badala ya kukaririshwa tu

Ndio maana hata viongozi unakutwa vichwa boga
"ooh foreigners wanatajirika kwa ndagu na kuiba na kujuana na wakubwa"[emoji118] wahindi ni waaminifu sana acha tu watoboe. Hawaangalii muonekano na kukuzidishia bei kama wabongo wengi wanavyofanya
 
kumbe na wewe ni poyoyo tu, hapo kuna uchambuzi gani. Km watu wenyewe ndiyo km nyie unategemea nini. Hamuwezi kuelewa profession yoyote, mna udumavu wa akili kutokana na lishe mlizotumia utotoni
[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]
 
Ahsante sana kaka. Ni Wazungu hao bila shaka, hawataki janja janja

Bosch ni wazungu makao makuu ujerumani,,, ni brand kubwa sana maana ni garage ambazo zipo dunia nzima..

Ila bei zake sio za kitoto...maana wateja wao ni mabalozi, na makampuni makubwa.

Wale tuliozoea Zile service za elfu 50 ama laki moja..

Bosch sio kwa ajili yetu
 
Siyo mafundi tu; binafsi hapa Tanzania naona Kada zote hufanya kazi zao kwa kubahatisha..

Hata hawa Madaktari wetu, wengi wanabahatisha kwenye kutibu wagonjwa..

Wanasiasa ndiyo usiseme, na Uchawi wanatumia ili kufanikisha siasa zao Uchwara..

Tanzania ni maeneo machache sana wanazingatia Professionalism kwa asilimia 100%..

Nadiriki kusema Ikulu yetu pamoja na Wizara na Ofisi zote za Umma ndiyo Vinara wa kufanya mambo Kikanjanja kanjanja..
[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]Umenikumbusha kituko fulani kuna siku miguu yangu ilikuwa ina maumivu chini ya unyayo yaani inanipa ganzi na kuna alama fulani za makovu zinatokea kwa chini hasa hasa msimu wa baridi sasa nikaenda hospitaliali uswahilini kumuonyesha dokta akanicheki akashindwa kujua tatizo langu ila akajiongeza tu"akaniambia hizi zitakuwa fangasi tu nakuandikia dawa za fangasi" sikubishana nae na kwa vile nilikuwa natumia Bima sikuleta complain nikaondoka na dawa alizonipa nikasepa.
Baada ya siku kadhaa nikaenda kwa specialist wa ngozi TMJ akanicheki akaniambia haya ni makovu ambayo yalisababisha na miba kukuchoma mara kwa mara miaka ya nyuma sasa yameacha makovu ambayo mizizi yake iko kwa ndani na kuitibu kwake ni hadi ufanyiwe operation unyayoni,nikakumbuka ni kweli utotoni nilikuwa mtundu sana nilikuwa nakimbia maporini kufukuza kuku bila kuvaa viatu pekupeku na miba zilikuwa zinanichoma mara kwa mara baada ya hapo nikasepa sikutaka kufanya operation.
 
Kuna Nissan Dualis ya teacher mmoja hivi alikopa ndo akanunua, ilienda kufia gereji ... Gari ilikuwa na shida ya usukani kumbe ilihitajika matengenenezo madogo tu pamoja na kuweka fluid, fundi kafumua usukani wote, mfumo wote wa umeme ukapiga shoti...
Teacher hakuongea kitu alinyooka moja kwa moja polisi... Sikujua kiliendelea nn
Dah yaani mtu anafungua usukani hajadisconnect battery.

Balaa tu la Airbag kudeploy ikuue au ikuvunje shingo halitoshi watu kujifunza.

Hapo bado mtu hajachomoa wire za immobilizer. Maana unaweza ukaja kurudishia, ulikuwa unafanya kazi ya 20k likazaliwa tatizo la 500k.
 
Tatizo la mafundi kukubali ukweli ni mgumu sana. Halafu wanapata pesa kwa kukadilra ndio maana wamelizika.

Mifumo ya magari sasa imebadilika ndio maana Nissan zinawashinda na kundandia kusema kimeo kumbe nyie ni vimeo.

Swala la vifaa ndio kabisa yani na mkuta fundi anatumia nyundo kuondoa kitu kwenye matairi mpaka unachoka.

Magari yanayo toka yanatumia electronic na umeme mwingi sana kuliko mlivozoea gari zenu 90.

Kila siku mnaunguza magari ya watu.
Jiwe lililotupwa gizani limekupata. Kitu gani hao mafundi vimeo wamekuharibia mkuu?
 
Mafundi sioni shida yao bali shida ipo kwawamiliki.mtu unaona kabisa sehemu unayo peleka gariyako hata hapajajengewa atlist uziotu.sasa katika halihio unategemea nini? huduma yaaina gani?.kifupi mabosi hela hawana ndio Mana mnapeleka chini yamwembe🤣🤣 Sasa mtu una ki i.s.t unataka kisigongwe nyundo? kwauspacio gani kilionao?😃😃

Mana ukikipeleka kwenye garage zamaana unakiacha ukouko kwasababu umezoea kutoa elfu kumi natano yasevis🤣🤣.garage zamaana nikwaajiri ya range, Ford,landcrz,benz,vw,nanyingine zaulaya.

Hayo mengine nikugonga nyundotu hamna chanisani Wala nini zote gari zakawaidatu msiogope zikila nyundo ndio stahikizao mana huwezi kununua kitendea kazi chagarama halafu mtu anakuja kulialia eti halingumu bosi😂😂 hatakama niwewe hutaipiga nyundo gariyake huyo mtu😃😃nazani mmeelewa?
 
Uko sahihi kabisa mafundi wengi ni kubahatisha tu kwa gari nyingi za sasa ni kutumia diagnostic computer mtu ana force afumue ata engine wakati haviusiani ndo hivyo hakuna namna.
Diagnostic mashine inadeal na management systems tu. Sensors, electrical actuators na modules(hii ni sehemu ndogo sana kwenye gari. Kuna vitu vingi sana bado havihitaji Diagnosis.

Mtu anakuja gari inagonga chini, anataka umfanyie diagnosis na mashine. Duh!
 
Nimependa analysis yako, umesema vyema.
Madaktari wa Tanzania ndiyo makanjanja +++.

Ukijumlisha na vimeo walio huko "mahabara' zao utachoka kabisa.

Majibu ya vipimo vingi ni full kukisia au kuhisi.

Kila ukipima mkojo matokeo ni UTI na daktari fasta anakuandikia azuma, cipro au ceftriazone.

Ni bora serikali iajiri madaktari wa kihindi au wakyuba kuliko hawa wakwetu
 
Back
Top Bottom