Nasikitika kusema kwamba, Katiba Mpya tunayoitafuta kwa nguvu nyingi haiwezi kutusaidia

Nasikitika kusema kwamba, Katiba Mpya tunayoitafuta kwa nguvu nyingi haiwezi kutusaidia

Ya zamani imetushinda kuwajibisha viongozi wakikosea. Mpya tutaweza kweli? Cha msingi issue sio katiba. Issue ni tutaweka mfumo gani ambao utafanya kila mtu awajibike na sheria. Lakini mwisho wa siku hata kama tukipata hiyo katiba. Bado kuna swala moja ambalo ni gumu kutatulika "rushwa" kiongozi anaweza kucheza faulo. Lakini marefa( bunge na mahakama) wakapewa rushwa na wakavunga hawajaiona faulo, hata kama wananchi wakiona faulo. Bado kiongozi na timu yake ya jeshi na mahakama wanalindwa na jeshi. So mwisho wa siku wananchi mtabaki kulia tu.
Ndo maana nasema. Cha msingi hii kitu inahitaji ma genius na wana falsafa kuijadili na kutengeneza mfumo utakao kua permanent
Mwisho wa siku solution bado ni moja. Elimu bado ni jambo la msingi. Kwa sababu. Imagine watanzania wote million 55 wakawa na uelewa wa intelijensia ya siasa na elimu ya juu. Hivi nani ataweza kumdamganya nani. Hapa ndo utashuhudia mabadiliko makubwa. Ila kwa style iliyopo. Wajinga bado ni mtaji mkubwa wa wanasiasa. Wakiisha wajinga kila mtu anarudi kwenye umaskini. Kwa sababu hakuna mtu anae elimika anakubali kufanywa mtumwa " educated mind cant be enslaved"
Hii nguvu tunayotumia kupambana na wanyonyaji ni kwa sababu watu wengi hawawezi ku organize na kufikiria kitu kimoja kwa sababu ya elimu. Na wanasiasa wanapenda situation iwe hivo ili wafaidike.
 
Angalau basi kuwe na tume huru ya uchaguzi, hilo nalo lina gharimu nini nchi! Kwani Serikali haijui kuwa tume iliyopo sio huru chini ya mfumo wa vyama vingi?!
 
Ndiyo na ni ukweli kabisa, Katiba tunayojaribu kuitafuta kwa jasho jingi na Energy nyingi, nasikitika kusema, haitatusaidia popote kama nchi.

Kama kuna mtu anapingana na mimi, Embu atusaidie kujibu maswali haya

Ni kweli tumekuwa na katiba isiyokidhi matakwa yetu hususani katika mizania ya kisiasa, kwa maana, katiba iliyopo, ilitungwa chini ya Chama kimoja, hivyo kuvifanya vyama vingine kukosa uhalali wa kulindwa na katiba hii tuliyonayo

Kingine, Katiba hii iliyopo, inamfanya Rais wetu kuwa mfalme, ni kama yeye ni mtu wa kwanza na wa mwisho, kwa lugha ys kiyunani, ni Alfa na Omega, n.k

Sasa basi, Ukisikiliza kwa umakini, wengi wa wanaharakati wetu kwenye majukwaa ya kisiasa na majumkwaa mbalimbali mbali, Utasikia wakisema, Tunataka katiba itakayotuwezesha kuwaajibisha wote wanaovunja katiba

Ni jambo jema, maana mtu yeyote anayediriki kuvunja makubaliano yetu na katiba yetu , ni sawa na matusi kwa watu woote kama taifa

Tumeshuhudia katiba yetu ikivunjwa waziwazi na baadhi ya viongozi wetu,

Bahati mbaya ni kwamba, kuna waliovunja katiba hata kwa wale ambao, katiba hailindi ouvu wao kama ilivyo kwa Maraisi wa nchi, lakini wanapovunja, Hasira zetu tunazielekeza kwa kiongozi mkuu, tunamsagia meno, Wakati huohuo, Katiba yetu mbovu tuliyonayo, ni kumlinda Raisi wa nchi na maovu yote kipindi awapo madarakani, na kwamba Hawezi kushitakiwa kwa kosa lolote awapo madarakani

Na bila shaka, shida yetu inaanzia hapo


Okay, Achilia mbali makosa ya Rais kwa mjibu wa katiba mbovu tuliyonayo kwamba, hatoshitakiwa kwa makosa yoyote aliyotenda akiwa madarakani, Hili tunaweza kusema, lipo juu ya mamlaka ya kawaida ya mwananchi kumwajibisha Raisi wao kwa kuwa katiba inamlinda

Upande wa pili kwa kosa hilohilo la kikatiba, Tumeshuhudia Bunge lisilo halali, Ni bunge ambalo wabunge wenginewe waliomo humo bungeni si wabunge halali kwa mjibu wa katiba za vyama vyao pia kwa mjibu wa katiba ya nchi, kwamba hawana uhalali wa kuwa wabunge kwa kuwa, hawatambuliki na vyama vyao na katiba haitambui mtu wa aina hiyo kuwa sehemu ya bunge

Sasa basi

Nionyesheni ni wapi ambapo huyo mkuu wa mhimili huu wa Bunge alipohalalishiwa na katiba hii mbovu tuliyonayo kwamba naye hawezi kuwajibishwa,

Je, sasa, ni nani wa kumwajibisha?
Ni kwa nini tunataka katiba mpya, Je, ni nani atakuwa mbadala wetu wa kusimama na kuwawawjibisha wote wavunja katiba?

Je, katiba hii mbovu ilipokuwa ikivunjwa, ni nani anafahamika ambaye yeye anapaswa kudili na wavunja katiba yetu? Je, alifanya kazi yake?


Na kama alishindwa kuwashughurikia hao waharifu wa kikatiba, Ni kwa vipi anadhani itakuwa rahisi kuwashughurikia kukiwepo katiba mpya?

Ni nani asiyejua kwamba, Watanzania, Watanzania kwao ni wazuri wa kuhamaki mitandaoni pekee ila nje ya hapo ni watu wanafiki na wapole kama maji ya mtungi? na ndiyo maana hata Asiyelindwa na katiba aweza kuvunja katiba na ikawa salama?

Mkinionyesha atakayekuwa zamu ya kuwashughurikia wahalifu wa kikatiba badala yetu, ndipo nitakubali kwamba, Tunataka kweli katiba na tumemaanisha

Katiba haijilimdi, haijipeleki mahakamani, haiandamani na wala haimtishi mvunja katiba, Nionyesheni mlinzi wa katiba

Tanzania hoye?
Umewasilisha mawazo yangu kwa namna ingine kabisa yani kama ulikuepo akilini mwangu.

Ndio maana mimi nilisema katika moja ya uzi wangu...

Thread 'Mifumo imara bila watu waadilifu sio suluhisho, jenga watu kwanza' Mifumo imara bila watu waadilifu sio suluhisho, jenga watu kwanza
 
Angalau basi kuwe na tume huru ya uchaguzi, hilo nalo lina gharimu nini nchi! Kwani Serikali haijui kuwa tume iliyopo sio huru chini ya mfumo wa vyama vingi?!
Ili tume iwe huru inatakiwa iwe na sifa gani ?
 
Watanzania hawajui kuandamana, hawajui kudai haki yao, wao wanaamini tu kwamba, Mungu ndiyo kila kitu.

Hivi kwa nini kweli tunahangaishana kudai katiba?
Ndoma huko kwa mswati,watu wanamtoa kwa nguvu

Ova
 
Katiba ya sasa inaruhusu maandamano na mikutano ya siasa, si ndiyo jamani?

Mbona mambo yakienda kombo, watu hawaandamani nchini?

Mbona wanasiasa wa upinzani hawafanyi mikutano ya kisiasa ya nje wakati katiba inaruhusu?

Ukipata majibu ya hayo maswali, ndo utagundua, chanzo cha matatizo ya Watanzania ni katiba au hilo jibu la maswali ya hapo juu!
 
Katiba ya sasa inaruhusu maandamano na mikutano ya siasa, si ndiyo jamani?

Mbona mambo yakienda kombo, watu hawaandamani nchini?

Mbona wanasiasa wa upinzani hawafanyi mikutano ya kisiasa ya nje wakati katiba inaruhusu?

Ukipata majibu ya hayo maswali, ndo utagundua, chanzo cha matatizo ya Watanzania ni katiba au hilo jibu la maswali ya hapo juu!
Hahaha.

Naunga mkono hoja kwamba tatizo sio katiba.

Tatizo ni watu.

Kwa sababu kuna mengi ambayo wapinzani wanakubali kikatiba lakini hayafanywi.
 
Nadhani hapa, kinachofanya katiba yetu iwe ngumu kupatikana, ni pale inapoonekana inadaiwa na wanasiasa badala ya wanaharakati huru wasioegemea chama chochote

Siasa zetu zimechafuka mno mkuu, Kwa tulipofikia, Ni rahisi kwa jambo mhimu kama hili, CCM na vyama vingine visivyoamini katika Chadema, basi ni rahisi kuona hilo ni jambo la chadema kama ambavyo Chadema hupuuza kila kilichojema kinachoanzishwa na CCM

Kupatikana kwa katiba hii tunayoihitaji sana, ni aidher, Chadema wanyamaze, kuzaliwe makundi mengine kabisa yasiyoshabihiana na chadema wala CCM, naamini ni rahisi kusikilizwa

Inawezekana ukawa na ushauri wa msingi kuwa cdm wanyamaze. Tuje kwenye uhalisia, je ni mara moja au 2 umewahi kusikia mtu akifanya madai stahiki ya kundi lao na kuambiwa kuwa anatumika? Makundi ya dhahiri ndani ya nchi hii ni wakulima, wafanyakazi na wafanyabiashara, je makundi haya umewahi kuyaona yakimudu kutetea maslahi yao, zaidi ya kuwataka wanasiasa wawatetee?

Hayo niliyokutajia ni makundi ya wazi kabisa ambayo ndio wanaoendesha nchi hii. Je makundi haya yana umoja wowote wa wazi, au wana platform ya pamoja ya kuongelea mambo ya utawala wa nchi hii, zaidi ya kila kundi kuongelea maslahi yao, ambayo hata hayo maslahi ya makundi yao huyapata kwa shida? Je kuna dalili yoyote ya makundi hayo kudai katiba ya nchi? Je kwa hili hii ya wanasiasa kudai katiba mpya, makundi hayo yanaonyesha kuwa hayaitaki katiba mpya? Tusitake kupotoshwa na ccm kuwa katiba mpya iachwe idaiwe na makundi ambayo, hata madai yao yanasubiri wanasiasa ndio wawasaidie kuyadai.
 
Ndio hapo tunapofeli kuwa na katiba yetu, Tunataka hata hao wasiokuwa na elimu wajue umhimu wa kuwa na katiba inayogusa maisha yao na wajue kwamba wanawajibu wa kuipigania na kuitetea

Katiba inshitaji makundi yote na siyo mashabiki wa Chadema wala nani

Hayo makundi wasio mashabiki wa cdm unayajuaje? Ni lini hayo makundi yataanza kuidai hiyo katiba mpya? Katiba hii ya mwaka 1977 hayo makundi yote ndio yaliidai mpaka ikatengenezwa? Acha upotoshaji usio na msingi wowote.
 
Mimi pia huwa nashangaa jinsi watu wanavyoweka mkazo kwenye katiba mpya zaidi ya ubora wa elimu yetu.
Tungekuwa na elimu ya viwango stahili suala la katiba lingekuwa agenda ya wananchi karibia wote na sio sasa ambapo wenye shida nayo ni wanasiasa, wanaharakati na wasomi tu.
Tungekuwa na elimu bora watanzania wasingeruhusu kuvunjwa kwa katiba, kuchezewa uchaguzi na mihimili mingine ya serikali kama ilivyokuwa miaka kadhaa iliyopita.
Tunachohitaji haswa na elimu ya bora kwa ujumla na ya uraia ili tusije hata tukipata katiba mpya watu wakaendelea kuivunja maana watu ni walewale na uelewa ni ule ule na tabia zilizile.

Uko sahihi kabisa kwenye hii nadharia yako, hiyo elimu kuhusu katiba nani anapaswa kuitoa? Ni lini unategemea watu watoe hiyo elimu ya katiba na wapi, zaidi ya hawa hawa wanasiasa? Na je, kuna mtu yoyote amekukataza ww ama wanaoamini kwenye hii nadharia yako kutoa elimu ya katiba? Ama hii kutoa elimu ya katiba ni dhana yako, lakini unataka watu wengine ndio waitekeleze?
 
Hoja ni nzuri ila kwa mtazamo wangu hakuna katiba yoyote Duniani ambayo hujilinda au kijitete yenyewe. Je katiba ni nini ni mkataba baina ya mtawala na mtawaliwa. Kwa ukweli huu basi mtu yeyote atakaevunja mkataba huu anaweza kuhoji kwa njia mbalimbali. Kwa upande wa serikali itakupeleka mahakamani na utafungwa. Kwa mwananchi njia zipo nyingi ikiwemo ya kwenda mahakamani, kuandamana na kupiga kelele. Na kelele hizi ndizo unazosikia, njia moja ikishindikana wananchi watatafuta njia njingine hadi wafike mwisho hadi kutokutii serikali iliyo madarakani kama Arab springs. Hiki kilio sio cha kufumbia macho au kukitolea utatuzi wenye kebehi kwani wananchi watatufanya nini ni hatari. Majeshi hayataweza kuzuia nguvu ya umma, serikali isitoe kisingizio cha kujenga uchumi this is cheap politics zenye dalili za kudharau mwananchi ni hatari sana.

Katika kitu kinapaswa kutoacha kupigiwa kelele ni haya madai ya katiba mpya. Hakuna hata kushiriki uchaguzi wowote mpaka katiba mpya yenye kutenda haki ipatikane. Inatakiwa hata hao viongozi watakaochaguliwa bila katiba mpya kususiwa, mfano sasa hivi watu hawajitokezi kwa wingi tena kupiga kura, maana hawana imani tena na mwenendo wa uchaguzi. Kwahiyo tunatakiwa tuende mbali zaidi hadi kususia hao viongozi ikibidi hata kuwazomea.
 
Wakina mbowe wanataka katiba mpya itakayo waingiza madarakani.
CCm wanataka katiba hii hii itakayo waacha madarakani? Huu ujinga wa kuona katiba kama nyaraka ya uchaguzi mtauacha lini?
 
Shida yetu kuu iko hapo chief, hata tukipata katiba nzuri kiasi gani, kama hatuna ujasiri wa kukabiliana na wavunja katiba, Tunapoteza muda tu

Ni hivi boss, tunaitaka hiyo katiba mpya ambayo pia itaendelea kuvunjwa. Lakini iko siku watu watasimama kudai katiba hiyo itekelezwe. Kwasasa tuipate hiyo unayoamini haitatekelezwa, kisha kutakuwa na kizazi cha kuhakikisha katiba hiyo inatekelezwa.
 
Katiba ya sasa inaruhusu maandamano na mikutano ya siasa, si ndiyo jamani?

Mbona mambo yakienda kombo, watu hawaandamani nchini?

Mbona wanasiasa wa upinzani hawafanyi mikutano ya kisiasa ya nje wakati katiba inaruhusu?

Ukipata majibu ya hayo maswali, ndo utagundua, chanzo cha matatizo ya Watanzania ni katiba au hilo jibu la maswali ya hapo juu!
Kwa maswali yako Chief, hapa tatizo siyo katiba, Tatizo ni Sisi watanzania
 
Ngoja leo tusikilize hoja za madai ya katiba,pengine tunaweza tukapata pa kuanzia
 
Na huu ndo unatakiwa kuwa msimamo wa taifa katiba ni hitaji la nchi sio hisani ya kiongozi fulani kuamua kitu hata nicha kijinga basi Kiko sawa hapana
Nadhani pia, utaratibu wa upatika aji wa katiba ukifanikiwa, kuwekwe kipengele kingine kitakachoondoa sauti ya Raisi kwamba, Wananchi watakapoona Katiba yao inamapungufu na wanataka katiba iundwe upya tena, kusihitajike sauti ya Raisi kuamua iandikwe au la, Ni kuachwe kipengele cha kupiga kura kuanzishwa katiba nyingine, wananchi watapiga kura, na hizo kura zikifikia kiwango kitakachoruhusiwa kuandikwa katiba zikitimia, mtu yeyote asiseme eti achwe ajenge sjui nini ndio aone katiba kama itaandikwa
 
Naunga mkono hili wazo japo bado nataka katiba mpya. Kama tumeshindwa kumuwajibisha kiongozi anaevunja katiba ya zamani basi hata mpya ikija itavunjwa tu na hakuna kitakachotokea
Nani wa kuwawajibishwa hao wanaivunja katiba sasa?

Watu wengi mnashindwa kulijibu hili swali ndio maana hamuoni umuhimu wa katiba mpya.
 
Tatizo sio katiba. Hata katiba itungwe na malaika. Viongozi wakiamua kuwa play wanawaplay tu. Cha msingi ni kutafuta njia ya kumbananisha kiongozi akivunja katiba. Hili jambo liko very complicated na linahitaji ufikiriaji wa hali ya juu na kwa kina. Pia linahitaji mwanafalsafa ambaye si mlafi wa hela itakayoweza kumbadilisha mawazo.
Ukifanikiwa kutenganisha mihimili ya nchi hakuna ujinga utaendelea.

Kwa katiba ya sasa Raisi anachagua majaji.

Sasa unategemea nini hapo?
 
Back
Top Bottom