Natabiri dunia lazima ivute pumzi muda mchache ujao ni kiama Iran

Hakuna anayesaidia bhana wale wanamtumia messages za mbinu za medani..hakuna kitu pale.

USA yupo bega kwa bega na Israel yaani ukisema mmpige Israel tu mwamba anakaa mbele yake ..hutoboi.
kwa macho ya nyama na damu utwaona USA, ila kwa macho ya rohoni, Israeli hupiganiwa na Mungu Mwenyenzi Yehova YHWH.

Israeli haijaanza kupigana leo. Iliingia Kaanani kwa vita ikitokea utumwani Misri. Mungu aliwashindia vita
 
sisi watu wa ulimwengu wa kiroho huwa tunaunga mkono.
haya ni majira ya ushindi tu kwa Israel.
ni kama yalivyo majira ya shetani kwa Tanzania ya sasa. asilimia 50 ya Tanzania iko mikononi mwao sasa hivi ninavyoandika
 
Ilo ndo watu wanashindwa kuelewa USA inamsandia Israel wanasaahau USA ndo viongozi wote top ni Waisrael Trump na kibri chake bado anaikubali sana Israel
Mbaya zaidi wanasayansi wakubwa karibu duniani kote haijalishi ni raia wa USA, CANADA, GERMAN, FRANCE nk. Ukitrace route zao utakuta wanadamu ya kiyahudi hapo ndio shida inapoanzia.
 
Hiyo mistari uliyo quote ya biblia kuhusu Israel ilipachikwa ni US na magharibi ili israel ionekane hivyo unavyoitazama wewe lakini na wakiristo wengi duniani waliaminishwa hivyo lakini utashangaa hao mayahudi dini yao si ukiristo na kitabu cha biblia wanakiona na kukichukulia kama gazeti la udaku tu, Mayahudi dini yao ni Judaism ambayo wao hawaamini katika yesu, nabii yesu wanamtukana na kumtemea mate.

Ulioandika hapo juu ni upuuzi mtupu, Taifa la israel lilisimikwa ni nchi za magharibi na US 1948 ata baba yako kiumri ni mkubwa kuliko nchi ya israel ujuwe kwamba hiyo ni nchi bandia walinyanganywa ardhi Wapalestina na kupewa hao mazayuni ambao hawana hata asili ya kuwepo hapo mashariki ya kati, Muda umefika wataitema tu. usiandikie mate
 
Mimi siamini bado kama hao ni taifa takatifu la Mungu!

Kwa kuwatazama tu hawana sifa kabisa!labda tuwapime DNA yao tuifananishe na ya mfalme suleiman!!
 
Aliyesema kuwa atakaye laani Israel naye atalaaniwa ni nani? Tunaaminishwa na watu weupe kila kitu! Mauaji yanayoendelea Mashariki ya Kati yanatakiwa kukemewa na kila mtu mwenye akili timamu na asiyekuwa na upendeleo wowote!!! Huwezi kuua watu kwa kisingizio cha kulipa kisasi ama huwezi kuua watu kwa kisingizio cha udini ama huwezi kuangamiza watu kwa kisingizio cha kumtafuta mtu!! Dunia inaendelea kushuhudia mauaji ya viongozi mbalimbali wasiokubaliana na sera za Kimagharibi!! Sera ambazo unachofanyiwa chochote unachofanyiwa unyamaze na ikiwezekana upate muda wa kuwasifu na kuwakaribisha kuchukua Rasilimali zaidi za kwako (Afrika) na uwaoneshe sehemu zingine ambazo hawazijui ili wao wakuletee net, kukupatia mkopo, kukupatia sila ili muuane wenyewe, kutoa mafunzo ya kukamatana wenyewe na kukualika ukawatembeleee!! Dunia Sasa watu wanaanza kuwa na uelewa wa hila mbalimbali za mabeberu ambazo hazina faida kwa wananchi wetu na mabeberu Bado wanaona kuwa watu Bado wapo mwaka 1950!!! Sisi Waafrika tumeachiwa kuaminishwa dini na kupewa misaada zaidi ili kuendelea kusambaza hizo Imani wakati wao wanakula Bata na kutuua!! Hivyo ni jukumu letu kukemewa kila aina ya uoevu maana haya makundi ya kidini Bado ni mapandikizi yao ya kuhofisha serikali zilizopo madarakani ili ziombe misaada ya ulinzi ambapo watapatiwa kwa masharti ambayo kwa mwenye akili ya kawaida tu anaona haki haijatendeka na kila anayesema kuhusu kurekebisha anaonekana kuwa ni msaliti na astahili kuawa ambapo hasira za wengine wenye kuona uporaji unavyofanyika na kusababisha madhara zaidi ya kuua wenye kuelezea ama kukemea uhalifu huo wa wizi wa Rasilimali za Afrika!! Endelea kuamini wao ni Bora maana ndiyo ulivyoaminishwa hivyo Toka ukiwa mdogo na akili imeganda hivyo!!! Misaada wanayopatiwa na Wamarekani kupigana na Hamas, Hezbollah, nk inatoka mbinguni!!! Na majeshi zaidi yatashuka kutoka mbinguni kuwasaidia wao maana Israeli ni Taifa pekee lenye Wayahudi ama vizazi vya Manabii kwa mujibu wa vitabu vitakatifu lakini ikiwa sivyo hivyo Tutashuhudia maangamizi zaidi kwa pande zote zinazopigana maana upiganaji wa Sasa ni wa Kitekinolojia zaidi sio wa uso kwa uso!!!
 
Walipekwaje Misri kuwa watumwa?
watoto wa Yakobo (Israeli) walimuuza mwenzao Yusufu baada ya kumuonea wivu. walimuuza Misri. Baadaye Yusufu Akaja kuwa mtu mkubwa sana huko Misri, na njaa ikatokea Israeli wakaenda kuhenea chakula Misri na kukuta Yusufu ndiye waziri mkuu wa Misri yeye akawatambua, ambapo aliwaita waende kuishi huko Misri ndipo baadaye (baada ya Yusufu kufa) wakaanza kutumikishwa kikatili na Farao. (SOMA KITABU CHA MWANZO)

Baadaye Musa anapewa jukumu la kuwatoa Misri utumwani na kuwapelekwa kwenye nchi ambayo Mungu alikuwa amemuonesha Ibrahimu (miaka kibao nyuma) ambayo ndio Kaanani.

...
 
Alafu eti wewe unaelewaje .... anapotumia maneno kama."huwenda"..labda,.....ktk utabiri wake?
 
Huwezi kufundisha mbuzi kucheza mziki....watu wengi ni wajinga mno wao hushabikia Israel wakijua ndo Israel ya musa...hutaweza kuwafundisha wakaelewa maana hawajafunuliwa na Mungu
 
ISRAEL ni taifa teule na takatifu mbele za Mungu ila waisrael halisi makabila 10 walichukuliwa utumwani na hawajarudi waliobakia ndo hao asili ya Ethiopia ila uwaonao akina Netanyahu ni wahuni tu waliletwa pale na mawakala wa shetani wala sio waisrael
 
Rabishiiii
 
Jana umeTABIRI kuwa baada ya masaa machache ni KIAMA huko Iran.

Ndugu yangu TumainiEl unajua Pombe huwa zinaleta maono HEWA.
 
kwa macho ya nyama na damu utwaona USA, ila kwa macho ya rohoni, Israeli hupiganiwa na Mungu Mwenyenzi Yehova YHWH.

Israeli halijaanza kupigana leo. Iliingia Kaanani kwa vita ikitokea utumwani Misri. Mungu aliwashindia vita

Tofautisha kati ya Uyahudi na Israeli. Uyahudi ni Ukafiri, Israeli ya leo ni makafiri na wana lana ya nabii Daudi, Suleyman na wengine katika Mayahudi.
 
Huu ni mwisho utawala wa kidikteta wa Iran.
Sababu kajitengenezea yeye mwenyewe.
Kuanzia sasa Israeli imepata ruhusa na sababu ya kuipiga na kuisambaratisha katika kabisa katika siku na muda wowote ule

Huu sio mpango wa Leo au kesho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…