Natafuta mganga wa kienyeji konki

Natafuta mganga wa kienyeji konki

Basi ngoja niwapatie kisa flani hivi..
Mwaka 2019 niliibiwa simu zangu kama 3 hivi...(kila moja ilikuwa na matumizi yake ikiwemo ya shughuli za dukani).
Basi nikaelekezwa kwenda pale makanya sehemu inaitwa nkwini. Nimefika mzee akaniambia utazipata tu.
Basi akanipigisha kambi kama siku 3 kwake ila usiku wa manane ananiamsha tunatoka nje kuna upande tunasimama halafu kuna maneno anaongea na mimi ananiambia niongee maneno flani.
Basi akaniambia nikanunue mbuzi wale wa rangi za brown na kuku wa nkama sijui. Kwa ajili ya kuniangalia matatizo yangu lakini pia itolewe kama sadaka yani watu waitwe wale na chakula kipikwe.
Basi siku ya mnada wa makanya j5 tukaenda na mwanae ikantoka kama 80 elfu hivi kununua mbuzi na jogoo.
Basi akamchinja yule mbuzi akachukua utumbo wake akawa anaangalia vitu flani.
Kupitia ule utumbo aliniambia anaona msiba kwenye familia yangu ila sio mimi nitakaekufa
Pia anaona nina nyota ya hela na kuna utajiri mkubwa mbeleni (sasa sijawa tajiri ila mtaji upo mahali unakuja na nishauzoom).
Na sijalogwa sema ni matatizo tu madogo madogo ambayo mengine niliyasababisha mimi mwenyewe na kuna jambo akanilataza nisilofanye kwani litaharibu baraka zangu na malaika wanaonilinda watachukia.
Pia aliniambia jambo lingine ambalo sijalitaja nalo likawa vile vile.
Kingine akaniambia mwanaume niliye naye japo ninampenda sana hanifai kabisaa na atanisumbua sana mbeleni.

Haya yote aliyoyasema yalitimia kwa asilimia 100% na simu nilikuja kuzipata na aliyenikaba kwakuwa sura nilimkumbuka ndo alikamatwa (yani aliiba June 2019 akaja kukamatwa October 2019) akalipa gharama zote.

Sema huyu mzee mganga kwa jina la Wandile alikuja kufa na korona mwaka jana mwanzoni.
Ila alikuwa hatarii
So waganga wapo na wana maajabu watu muache ubishi
Huyu mzee alikuwa mganga wa kienyeji au wale wanaosoma dua?
 
Nakumbuka kuna story jamaa aliibiwa godoro boarding..., akaanza kupiga mkwara kwamba aliyeiba asiporudisha godoro ikifika saa tano usiku kwao wataanza kudondoka mmoja mmoja....

Haikupita masaa godoro likarudishwa..., Watu wengi huwa wanajiroga wenyewe huyo unayempa tahadhari kama amesikia kwa bahati mbaya akianza kuwashwa tu, lazima akuombe msamaha
 
Poleni na majukumu ya kila siku
Nimekuja na ID yangu hii sina haja ya kujificha

Moja kwa moja kwenye mada,nahitaji msaada kama kuna mtu anamjua mganga wa uhakika anifanyie kazi yangu, kuna waganga huwa nasikia wanatoa watu mabusha, wanatuma majini au kumpa mtu ugonjwa nahitaji mganga wa hivyo

Hii dunia ina mengi,na ikifika kipindi cha vita unaambiwa usichague silaha,nahitaji jambo langu likamilike kwasababu kuna watu wanaweza kukukosea heshima mpaka wakapitiliza, ukimya na subira ni muhimu lakini kuna watu huwa wanaona kama umezubaa

Nikifanikiwa kazi yangu nitakupa ya shukrani sina hiyana
Watu wa mahubiri hapa sio sehemu yake.

Nawashukuruni naamini nitapata msaada wenu
Mkuu kama mtu kavuka mipaka toa onyo uwenda akajiludi....
akizidi basi peleka makombora kama Urusi nchi Ukraine kudadadeki...
Akuanzae mmalize.

Onyo mjue unae pigana nae yuko vipi isije ngoma ikaludi kwako....
 
Back
Top Bottom