Nataka kumuoa huyu mlimbwende wa JF

Nataka kumuoa huyu mlimbwende wa JF

Habari wakuu,

Kuna mlimbwende mmoja humu amenivutia sana, nataka msimu ujao wa mavuno, niweze kutangaza ndoa kabisa.

Huyu mrembo ameiteka sana akili yangu, mpaka uwezo wa kufikiri umepungua; nilipo pishana naye tu barabarani, ilikuwa kidogo tu nigongwe na bajaji.

Kupitia huu uzi, anatakiwa ajitambue yeye tayari ni mke mtarajiwa wa equation x, na ajiandae kwa mipangilio ya familia ya kuwa na watoto wengi hapo baadaye.

Najua atapitia huu uzi, jina lake linaishia na h.

Wakuu nipeni baraka zenu.​

Wajomba wa Bwana harusi tupo tayari kukuunga mkono ufanikishe hili. Iwe heri tupu
 
Back
Top Bottom