Nataka nizalishe kuku wa kienyeji laki moja ndani ya miaka mitatu

Nataka nizalishe kuku wa kienyeji laki moja ndani ya miaka mitatu

Nimefikisha kuku 2000 mpaka sasa. Japo nilipata changamoto hapo kati, ila safari ndo imeiva hivi sasa. Nimetenga tray 10 kila siku za kuhudumia kuku wote. Mpaka ndoto yangu itimie.

Karibu tule vijogoo vya kuchoma na mayai ya kuchemsha kwa mama mkuu
allah akutangulie wasichokijua ni kuwa mpka kufika hiyo idadi hao kuku watakuwa wanajihudumia wenyewe.
 
umempa ukweli mchungu kulisha kuku laki1 kisa kuna mashine ya kukoboa karibu kijana analeta masikhara uyu
Mashine ya kusaga haiwezi kulisha hao kuku nafahamu. Ila hatua nilifikia saizi, nina soko la mayai kila siku tray 10 sawa na sh 120, 000

Nayaona matumaini japo sehemu ya kufugia inaelekea ukingoni. Hesabu niliyonayo ni kuuza uzao wa kuku 1500 yaani kila baada ya miezi 4 natoa kuku 12, 000 sawa na mil 150.

Biashara inaanza mwaka huu mwishoni
 
Mashine ya kusaga haiwezi kulisha hao kuku nafahamu. Ila hatua nilifikia saizi, nina soko la mayai kila siku tray 10 sawa na sh 120, 000

Nayaona matumaini japo sehemu ya kufugia inaelekea ukingoni. Hesabu niliyonayo ni kuuza uzao wa kuku 1500 yaani kila baada ya miezi 4 natoa kuku 12, 000 sawa na mil 150.

Biashara inaanza mwaka huu mwishoni
upo wapi mkuu nije kupata shamba darasa
 
Mashine ya kusaga haiwezi kulisha hao kuku nafahamu. Ila hatua nilifikia saizi, nina soko la mayai kila siku tray 10 sawa na sh 120, 000

Nayaona matumaini japo sehemu ya kufugia inaelekea ukingoni. Hesabu niliyonayo ni kuuza uzao wa kuku 1500 yaani kila baada ya miezi 4 natoa kuku 12, 000 sawa na mil 150.

Biashara inaanza mwaka huu mwishoni
hongera sana
 
Endelea kujifurahisha na kufurahisha wengine, ila kiuhalisia ni kwamba Huwezi kuwa na kuku laki moja

Unawajua kuku laki 1 au unawaskia tu? Hiyo mashine unayosema ipo ya kusaga haina uwezo wa kuhudumia kuku laki 1 Kwa siku

Ni vizuri kama umeamua kukimbia Dar na kurudisha mpira Kwa goal kipa ila kama ndo umerudi na mawazo hayo basi muda sio mrefu utarudi Dar pamoja na kuku wa Mama

Kuanza na kuku 15 saizi unawaza kuwa na kuku laki 1, unadhani wafugaji wenzio walio kwenye tasnia kabla yako hawajui hayo madawa na chanjo?

Huwajui kuku vizuri wewe, Kwa sasa we furahia tu hao vifaranga 70 Kwa sababu wapo ndani ya uwezo wako na ata wafike 500 still wanaweza wakawa ndani ya uwezo wako

ila ukitaka kujua kuwa inawezekana unawaza ukiwa umeshiba sana au Una njaa sana basi Piga hesabu ya gharama ya kulisha kuku 5000 tu ndio utajua kuwa unaota ndoto ukiwa ndani ya Maji

Anyway, All the best mkuu
Mimi siamini kwenye kufeli huwa naamini kwenye kujifunza. Pia nafahamu kuwa kila kitu hakipo kwaajili ya kila mtu. Nilikua na malengo ya kufikisha kuku laki moja lakini nimeamua kuishia kwenye kuku 2000.

Pia huwa siogopi kuzifuata ndoto kubwa. Kadri ninavyozidi kusogea na mradi wangu, ndivyo ninavyozidi kuyaelewa mengi sana kuhusu ufugaji wa kuku wa kienyeji.

Nilipofikia sasa, mdondo sio ugonjwa wa kutisha kwangu maana nina tiba kabisa
 
Namaanisha kibiashara. Kuku wa kienyeji anatumia miezi sita kuwa mkubwa wa kulika wakati chotara anatumia miezi mitatu hadi minne. Kibiashara ilo gape la muda lina maana kubwa sana.

Kuku wa kienyeji ukiwafuga kibiashara (sio free range) wana gharama sana halafu soko lake ni gumu kutokana na bei ambayo inajumuisha gharama za kuwatunza

Kuku wa mayai wana faida sana ila unapaswa kuwa na mtaji wa kutosha kuwalisha miezi sita kabla hawajaanza kutaga

Wanyama wana mzunguko mzuri kwa wawekezaji wanaotaka faida ya haraka maana wakifika kuanzia wiki nne wanakuwa tayari kuuzwa ingawa faida yao si kubwa sana

Kwa ushauri wangu kama mdau wa sekta hii kufuga kuku laki moja wa kienyeji sio jambo zuri unless uwe na soko zuri la kimkataba kabisa. Ngumu sana kukuta watu wanaonunua kuku kwa wingi kama wale wa mikutano au harusi kutumia kuku wa kienyeji. Wa nyama wanamzunguko mkubwa sana na ni nafuu. Kienyeji tunakula kwenye matukio muhimu tu
Soko ni kubwa sana la kuku wa kienyeji. Kinachofanya lisionekane, ni uhaba wa wafugaji wa kuku hawa. Ila wanatafutwa sana
 
The failure is the success

Lengo lake ni kufikisha kuku 100,000

Let say ndani miaka 3 amefikisha kuku 1,000 au 10,000 kwa kutumia hikohiko kidogo alichoanza nacho

Sawa anaweza kuwa amefeli kufikia lengo lake lakini maisha yake hayatakuwa sawa na jinsi yalivyo Sasa

Kila la kheri ndugu, utekelezaji mwema

Usisahau kuleta mrejesho.

Sent from my Infinix X653 using JamiiForums mobile app
Ulichokisema ni kweli kabisa. Hatua niliyofikia saizi, kwakweli nafurahi mwenyewe. Maana sioni mlima wa kuwalisha. Nauza mayai yao wenyewe maana soko ni zuri alafu nanunua mahitaji. Nakua busy sana maana kila kitu nafanya mwenyewe.

Naiona nuru mbele yangu
 
Simamia kwenye chanjo kuna ugonjwa unaitwa mdondo huo ukipita bandani kama kuku wako hawajachanjwa wanapukutisha banda nzima.
Mdondo sio tishio tena kwangu maana nina dawa ya kutibu kabisa. Hata ndui haifui dafu. Nimejifunza mengi kwa muda mchache sana nilioishi na kuku
 
Nakutakia kila lakheri katika ufugaji ila anza nao taratibu ujue mbivu na mbichi za hiyo biashara. Mimi ni mfugaji wa kuku wa nyama na mayai. Nionavyo mie kwenye mazao ya ufugaji kuku, wenye faida sana ni kuku wa mayai wanafuatia broiler lisha hawa kuku chotora kisha wa mwisho wa kienyeji
Raha ya hawa kuku wa kienyeji hawako complicated sana kuanzia kula, na nature yao kwa ujumla. Inanipa urahisi maana hata dawaza magonjwa hatarishi, hivi sasa nazifahamu
 
Nimecheka sana.Vijana wanatoka shule wakiwa na motivated na mitandao.Mwambie ajaribu kuku 100 kwanza,ndiyo ataelewa Somo ni kwa nini watu hatufugi Kuku wa kienyeji kwa idadi ya broiler
Nitafika tu hata kwa mbinde
 
Mimi siamini kwenye kufeli huwa naamini kwenye kujifunza. Pia nafahamu kuwa kila kitu hakipo kwaajili ya kila mtu. Nilikua na malengo ya kufikisha kuku laki moja lakini nimeamua kuishia kwenye kuku 2000.

Pia huwa siogopi kuzifuata ndoto kubwa. Kadri ninavyozidi kusogea na mradi wangu, ndivyo ninavyozidi kuyaelewa mengi sana kuhusu ufugaji wa kuku wa kienyeji.

Nilipofikia sasa, mdondo sio ugonjwa wa kutisha kwangu maana nina tiba kabisa
Hongera sana mkuu, wewe ni mfano wa kuigwa, uliamua kusimamia ndoto zako pamoja na changamoto ulizopata humu kutoka kwetu sie wachangiaji

Ata kwa hao 2000 sio haba ni wengi sana mkuu, ukilinganisha na Idadi uliyoanza nayo ya kuku 15, hivo unastahili hongera za dhati kabisa

Kama hutojali mkuu, tunaomba ushee nasi picha za kuku zako ili uzidi Ku inspire kundi kubwa la vijana ambao wanaamini kufuga ni kazi ngumu sana

utakuwa umetusaidia sana ukishea picha ili tuone Aina ya mabanda ambayo unafugia, system unayotumia kulelea vifaranga wako na vingine ambavyo utaona inafaa

Bila kusahau kutujuza ndugu zako hiyo dawa ya Mdondo uliyosema ushaijua, maana wengine tunaskiaga kuwa Mdondo hauna dawa, utawaokoa sana wafugaji wenzio mkuu
 
Hongera sana mkuu.
Kwa jamii ya wafugaji tukiona mtu mwenye ndoto kama zako huwa tunafurahi sanaaaaa.

Yan hapo najiona kama ndo mm vile nafuga kuku chotara katika kale ka pori kanguu.

Mungu akutangulie na akuepushe na kila baya katika ndoto hiyo,ukapate kufanikiwa zaid na zaid
 
kuku wa kienyeji wa umri wa miezi 4 ana thamani ye Elfu 15. Mbuzi wa Miezi 4 ana Thamani ya 80k. Kupanga ni kuchagua!
 
Back
Top Bottom