NATO itaiponza Ukraine. Leo wametangaza kupeleka ndege vita huko Ukraine

NATO itaiponza Ukraine. Leo wametangaza kupeleka ndege vita huko Ukraine

Ni hatar kwa Ukraine au kwa dunia ndugu. Ujiandae ulimwengu unaelekea kubaya zaid na wenye hali mbaya zaid ni sisi maboya. Hatujajiandaa kwa kinachokuja.
Ni hatari kwa Ukraine zaidi maanake kwasasa hata ikitokea vita ya 3 ya dunia uwanja wa vita utakua Ukraine na nchi za karibu. Siso wa huku mbali tutaathirika kibiashara na kiuchumi tu.
 
NATO wanataka kujua uwezo wa mrusi na siraha zake kupitia hii Vita.
Wanapanga pia kumdhoofisha kiuchumi maana ametumia pesa nyingi sana kwa hii vita.

Uwezo wa kumaliza hii vita anao,kuna mawili aachie full mkoko au awapige mdogo mdogo ajiangushe kiuchumi.
Kuhusu kuanguka kiuchumi siyo rahisi. Gesi na mafuta bado anauza sana ulaya marekani na Asia hasa India. Bidhaa za kilimo na viwandani pia. Vyovyote vile atakavyopigana Ukraine na NATO hawatamuweza
 
Baada ya huu mpambano Urusi hata vamia nchi yoyote miaka ya karibuni.Wengi hatufuatilia historia tunabaki kulalama NATO vile NATO hivi.Tunajua kuwa 11% ya Ardhi ya Urus inakopakana Finland ni Ardhi ya Finland Urusi ilibeba kimabavu,mnajua Urusi alipataje kisiwa cha Kalingard ,Mnajua kuwa Urusi anatawala baadhi maeneo ya Georgia baada uvamizi wa 2008.Urusi kwa asili ni mvamizi Sugu
Russia inachofanya ni kwa usalama wake!
 
Hizi nchi za NATO tangu vita imeanza wamekua wakitoa silaha na fedha kwaajili ya Ukraine kupambana na Russia 🇷🇺. Leo wametangaza kupeleka ndege vita za kisasa F 16 lakini tuelewe kuwa Ukraine anazo mig ambazo ni Su version ya mrusi na Russia amekua akizilipua na kupiga miundo mbinu ya Ukraine inayosaidia mashambulizi dhidi yake.

Hawa NATO hawajitokezi waziwazi front lakini wapo..

Lengo la andiko hili kwa wasomaji wenzangu na wafuatiliaji wa vita hapa duniani ni kuelezea udhaifu wa nchi ya Ukraine na mtego wa NATO katika hii vita. Kwanza hawajampa uanachama mpaka leo kama target ya Ukraine na ombi lake la muda mrefu.

NATO wapo mguu nje mguu ndani ni kama hawana uhakika je tutashinda hii vita kwa kumsaidia Ukraine? ( ukweli ni kwamba hawawezi kushinda)

Russia amekua akipigana kiustaarabu sana kwa sababu kiuhalisia wayukreini wengi wana asili ya urusi na hawataki hii vita ila maslahi ya marekani na NATO vita hii inachochewa.

Leo uingereza huyu waziri mkuu mpya ametoa agizo kiwa silaha za uingereza ziidhambulie urusi moja kwa moja. Kwa mtazamo wangu sasa putin atafungua ghala la silaha maana ni kama vita ya NATO na Russia imetangazwa rasmi. Lakini atakeumia hapa ni Ukraine na mwisho wa siku Ukraine atabaki kama alivyo hatapewa uanachama wa NATO na atakua koloni la mrusi totally.
Putin kama ana ghala la silaha angeshalitumia, saivi kakimbilia north korea kupata usaidizi ashaingia nao mkataba eti akishambuliwa yeye na North Korea aingie mzigoni, kaenda na Vietnam hajui kama vietnum uchumi wao uliyumba US ndio anampa maisha saivi, Putin ni big looser


 
Ukraine imekubali nchi yake kuwa uwanja wa majaribio.
Unaishi dunia ipi wewe?
Ukraine alivamiwa na russia kwa mabomu kila upande wa nchi yao, miji na majengo yakavurugwa kote sasa kuna ubaya gani kujilinda? Ukraine siye alienza vita na kama wewe kuvamiwa nyumbani kwako nyumba yk ikapigwa moto sasa unaposema Ukraine ni uwanja wa majaribio unakuwa hufahamiki, Ukraine anatafuta usaidizi kujilinda ingekuwa si usaidizi leo Ukarine ingekuwa bendera za russia zinapepea Kyiv
 
Kuhusu kuanguka kiuchumi siyo rahisi. Gesi na mafuta bado anauza sana ulaya marekani na Asia hasa India. Bidhaa za kilimo na viwandani pia. Vyovyote vile atakavyopigana Ukraine na NATO hawatamuweza
Vita inamaliza Pesa,Hao wanajeshi wa kukodi anawalipa kiasi gani? Uchumi wake lazima upungue.Achilia mbali vikwazo. Alivyowekewa na EU.
 
Amesema wapi? Maana zelenskey mpaka jana anatoa shukurani sana kwa kupata hizo F16 ili zikamnyooshe mtu
Ukitaka kuelewa kinachpendelea duniani usiwe mshabiki! Hanyosheki mtu!
Haya fuatilia kwenye link hii usikie Zelensiky anasemaje!
 
Umetumia neno kubwa sana kusema I am a fool, isipokuwa nitasema tu kuwa wewe ni mjinga na mpumbavu sana ambaye bado una sumbululiwa na kuamini cold war politics kama Putin ambaye bado anataka kuipata USSR tena, na hata huelewei kuwa chini ya makubaliano ya Budapest Memorandum baada ya kuanguka USSR, nchi za Urusi, Uingereza na Marekani zilipewa jukumu kulinda usalama wa Ukraine kusudi iachie silaha za Nyuklia ilizokuwa nazo.

Wakati Putin anavamia na kujimegea Crimea, Ukraine haikuwa na jeshi kabisa na ilikuwa ni nchi neutral ikiamini yale makubaliano ya Budapest Memorandum. Uingereza na Marekani wanatekeleza makubaliano hayo kwa kuisadia Ukraine, wakati Urusi ndiye aliyevunja makubaliano hayo kwa kuanzisha uvamizi.
Na Marekani alipoanzisha vita kule Iraq akiwa na wapambe wake wakubwa wa nato,alikuwa anatelekeza makubaliano ya wapi? Sema umechagua upande unaoupenda. Unafikiri Murikans(American) wakubali Russia aweke military base kule Latin America na Caribbean chanel.? 🤔
 
2008 Urusi aliivamia Georgia na hakukua na vita Ukraine
Georgia imeingiaje hapo? Tunazungumzia Ukraine. Kama unafahamu hii vitu na kama ulivyotoa story Yako. Sema nini kimetokea kuanzia 2008 onwards na hata kupelekea mapinduzi ya Rais wa Ukraine. Kama hujui sema tutakusaidia. Ama kapitie Tena interview mbalimbali za Putin, deliberations mbalimbali za NATO na EU
 
Ni hatari kwa Ukraine zaidi maanake kwasasa hata ikitokea vita ya 3 ya dunia uwanja wa vita utakua Ukraine na nchi za karibu. Siso wa huku mbali tutaathirika kibiashara na kiuchumi tu.
Bila mafuta, pesa za mikopo, bila misaada, bila ARV na codom, bila internet, unaiona nchi ikiathirika kibiashara na kiuchumi tu? Mkuu huku hali inaweza kuwa mbaya kuliko walio vitani.
 
Baada ya huu mpambano Urusi hata vamia nchi yoyote miaka ya karibuni.Wengi hatufuatilia historia tunabaki kulalama NATO vile NATO hivi.Tunajua kuwa 11% ya Ardhi ya Urus inakopakana Finland ni Ardhi ya Finland Urusi ilibeba kimabavu,mnajua Urusi alipataje kisiwa cha Kalingard ,Mnajua kuwa Urusi anatawala baadhi maeneo ya Georgia baada uvamizi wa 2008.Urusi kwa asili ni mvamizi Sugu
Unajua marekani aliipataje guantanamo?
 
Watu wanaonea huruma nchi za NATO kwenye vita ya 3, vita ikianza China haiwezi kuingia kichwa kichwa, labda Iran , kitakachotokea Rusia atapiga bomu la nyuklia Ukraine na Ukraine ataipiga Rusia kwa msasa wa USA, kwa madhara yatakayotokea kwa pande 2 , wananchi wa Russia na Ukraine wataungana kufanya maandamano ili kuondoa Putin na Zelensky madaraka. Kuna uwezekano pale Ukraine mzigo wa nyukilia utakuwa umeshafika, kila siku Rusia analalamika kuwa NATO wanatengeneza silaha za kibiolojia. Vita ya 3 ya dunia yatabaki maatifa ya Africa, Amerika ya kidini, Asia na Australia, ila Iran lazima aliwe kichwa. Rusia atateketea, Nato atayeketea.
Siijui kesho yangu itakuaje
Ila nnaloweza kukwambia ukraine haitakaa itumie nyuklia dhidi ya russia na tuseme ikaja ikatokea basi huko nato nakwenyewe kutakua hamkani haswaaaa
Russia hana haja ya kutumia nyuklia ukraine sababu anaetumia nyuklia ni mtu anaeshindwa au aloshindwa kama ilivyokua kwa us pale Nagasaki na Hiroshika ila Russia mboba kwake majambo yanaenda vyema kila leo anakwapua maeneo ya Ukraine
Ukraine bado ile tottaly kusarenda ila kashashindwa big time
 
Bila mafuta, pesa za mikopo, bila misaada, bila ARV na codom, bila internet, unaiona nchi ikiathirika kibiashara na kiuchumi tu? Mkuu huku hali inaweza kuwa mbaya kuliko walio vitani.
Na wao bila dhahabu , almasi , Tanzanite, coal , gas , kahawa , mbao , samaki , nyama , n.k wata survive vipi? Tunaishi kwa kutegemeana mkuu
 
Vita inamaliza Pesa,Hao wanajeshi wa kukodi anawalipa kiasi gani? Uchumi wake lazima upungue.Achilia mbali vikwazo. Alivyowekewa na EU.
Ripoti ya world Bank mwaka huu imesema uchumi wa urusi umezidi kuimarika. Hawa world Bank ni tool ya wamarekani kiuchumi ndio wanaripoti hivyo.
 
Siyo anapigana kistaarabu Bali huo uwezo hana Kama tulivyodanganywa, hata kutawala anga la Ukraine hawezi, Vita vya ardhini vimekuwa vigumu kwake, huko baharini meli amepeleka mbali baada ya kuzamishwa na Ukraine.
Msituone wote hatuna akili ya kung'amua Mambo wakati ukweli uko bayana.
Sasa unaona unauwezo wa kupambanua mambo kwa hili uloandika hapo
Kama hana udhibiti wa anga ukraine anaomba mifumo ya ulinzi wa anga kumdhibiti nani
Na ndege za f16 alizoahidiwa jana kupelekewa ukraine zinapelekwa zikalinde anga lanani
Hamjajua kupembua mambo bado akili zenu hazijakomaa
 
Putin kama ana ghala la silaha angeshalitumia, saivi kakimbilia north korea kupata usaidizi ashaingia nao mkataba eti akishambuliwa yeye na North Korea aingie mzigoni, kaenda na Vietnam hajui kama vietnum uchumi wao uliyumba US ndio anampa maisha saivi, Putin ni big looser
Russia anazalishq silaha mwenyewe na chuma anachimba mwenyewe. Ameingiza vifaru vipya elfu hamsini na bado viwanda vina endelea kuzalisha
 
Mbona hutaji sababu za Ukraine kuvamiwa kwamba kavunja mkataba walioingia na Russia Kwa kutegemea silaha za msaada zitamsaidia kwahyo anachezea mboko tu
Kwenye mkataba kuna kipengele kinasema ukikivunja unavamiwa? Ioneshe....rejea sababu iliyotolewa na Rais Putin wakati anatoa kibali ya wanajeshi wake kuivamia Ukraine. Hakuna sehemu alitaja kuwa Ukraine imevunja mkataba.
 
Back
Top Bottom