Nauli hizi za SGR nani atapanda? Kutoka Dar - Moro Tsh 24,000?

Nauli hizi za SGR nani atapanda? Kutoka Dar - Moro Tsh 24,000?

Wakati mwingine watanzania tuwe na uwezo wa kujua kwamba kinachowekezwa kikiwa ni ghali, na huduma itakayotolewa nayo itakuwa ghali.

Uwekezaji uliofanywa kwenye SGR ni mkubwa mno kwa ivo ni lazima tukubaliane kwamba na huduma itakayotolewa itakuwa ni ghali pia.
 
Kwa mahesabu hayo kutoka Dar hadi Mwanza kwa SGR nauli itakuwa 500,000
Ni sawa tu. Maana tofauti kati ya treni ya Umeme na ndege ni mwendokasi na njia inayotumika. Maana wanaotakiwa kupanda hizo treni ni wale wenye haja ama sababu ya kwenda kwa kasi kuliko mabasi, Kama huna haraka hakuna sababu za kupanda treni hizo.
 
Hizo bei sio kubwa endapo muda utazingatiwa
Maaan kama una haraka n nzur sana sasa hzo naul znafkia za ndege?
Kwa umeme upi kwa kuendesha hayo mabehewa used kwa haraka angalau ndani ya lisaa hadi Moro?
 
😂😂😂sasa apo na haiendi kigoma apo waha wangejuta na bei
 
Hi project ya sgr haikufanyiwa feasibility study au upembuza ya sanifu, haiwezakani hiyo nauli izidi ya basi, wakati tulikua tunahitaji mbadala wa bei ya chini wa kutumia mabasi na maroli.
Imagine SGR ya Kenya nauli kutoka mombasa hadi Nairobi 600km ni sh 1000 ya Kenya sawa sawa na 19,000 ya Tz itakua je kutoka Dar - Moro 180km iwe shilling 34,000 kwa hiyo itakua na comparative advantage kwetu.
 
Wakati mwingine watanzania tuwe na uwezo wa kujua kwamba kinachowekezwa kikiwa ni ghali, na huduma itakayotolewa nayo itakuwa ghali.

Uwekezaji uliofanywa kwenye SGR ni mkubwa mno kwa ivo ni lazima tukubaliane kwamba na huduma itakayotolewa itakuwa ni ghali pia.
dhana potofu
 
Hata kama ni mapendekezo sidhani kama mlifikiria au kuwaza kwa kinagaubaga, huko Anatorglo mnaenda kupaka mafuta ili kung'arisha hiyo nauli na si vinginevyo.

Ukute mmeshaandaa wazungumzaji wenu wa kutetea hiyo nauli na hapo ndiyo watakuwa wengi ukumbini.

--

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imepokea maombi kutoka Shirika la Reli Tanzania (TRC) kuhusu nauli za abiria kwa treni ya njia ya Reli ya Kisasa – ‘Standard Gauge Railway’ (SGR) zitakavyotumika kwa huduma ya usafiri wa treni za abiria.

Kwa mujibu wa Kifungu Na. 21 cha Sheria Na. 3 ya LATRA, 2019 Mamlaka inapaswa kukusanya maoni ya wadau kabla ya kufikia uamuzi wa kuridhia viwango vya nauli kwa huduma zinazodhibitiwa na Mamlaka ikiwemo nauli za treni.

Katika kulitekeleza hilo, Mamlaka imeandaa mkutano wa kupokea maoni ya wadau wa usafirishaji, ikiwa ni pamoja na watoa huduma, watumiaji wa huduma na wananchi kwa ujumla. Mkutano utafanyika tarehe 19 Disemba 2022 jijini Dar es salaam katika Ukumbi wa Anatorglo.

Nauli zinazopendekezwa na TRC ni Kama ifatavyo:

View attachment 2440636

View attachment 2440637

Kutokana na umuhimu wa mkutano huo, LATRA inawaalika wadau wa sekta ya reli na wananchi kwa ujumla kushiriki katika mkutano huo wa kukusanya maoni ya wadau.

Vilevile, wadau wanaweza kuwasilisha maoni yao kwa Mkurugenzi Mkuu kwa maandishi kupitia LATRA Makao Makuu, Mtaa wa Tambuka Reli, Dodoma au ofisi za LATRA zilizopo Makao Makuu ya kila mkoa Tanzania Bara kabla ya tarehe 3 Januari 2023.

Aidha, maoni ya wadau yanaweza kutumwa kwa barua pepe kupitia anuani hizi: info@latra.go.tz na dg@latra.go.tz

Imetolewa na:
Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano – LATRA
06 Disemba, 2022​
They are willingly killing it before it stars. Sijajua lakin wametumia uhalisia wa wateja wao au walitumia mere papers. We must balance the papers and the reality of the fields
 
Naisubiria na Bwawa la Nyerere likamilike niyakumbuke maneno ya wanasiasa yalivyo matamu kama asali ila matendo machungu kama shubiri. Wakati wanaanzisha hizo harakati ilisemekana SGR ikikamilika bei yake itakuwa nafuu sana hata kushinda nauli za mabasi, Hilo limetoka tusubirie umeme kwa sababu huo tuambiwa unit moja haitozidi 150tsh tofauti na Sasa inauzwa karibia 380tsh ili tuweze kuzalisha bidhaa viwandani kwa gharama nafuu. Tulitolewa mpk na mfano baadhi ya nchi km marekani wao unit moja mpk inamfikia mlaji hifiki hata 100 ya kitanzania ndio maana wanazalisha bidhaa kwa gharama nafuu
Achana na wanasiasa Gharama ya Umeme unaolipia inatokana na gharama za uzalishaji (au in our case gharama za kununua kutoka kwa madalali n.k.) sasa kama gharama ya uzalishaji itapungua common sense inakwambia nini ?

Tupende kuangalia tatizo lipo wapi na sio outcome zitakuwa vipi..., kama kila mwaka ukilima shamba kuna wezi wanakuja kuiba kabla haujavuna tatizo sio wewe kupanda / kulima tatizo ni hao wezi na jinsi ya kuwazuia wasikuibie..., Hence tatizo sio Bwawa kuisha na kuongeza double capacity ya sasa tatizo ni walamba asali
 
Wagogo wakisoma nauli ya Bahi naona wote watahamia Chadema safari hii
 
Tatizo la tanzania tunatukuza Umasikini mno.

Binafsi naona bei iko sawa, kuna watu wanakereka na muda mrefu kutumika barabarani yaani km 450 masaa 7-9
Wakati kwa treni unaweza kutumia masaa 4
Na pia ni adventure

Kikifanyika kitu utasikia sisi wanyonge itakuwaje
Unajua hii ni train ?; Unajua ni kiasi cha kuongezea behewa tu, kwahio hao watu hata mkitaka mkodi behewa kwa milioni tano ili msafiri peke yenu / peke yako nadhani its possible ?

Shida unaangalia mambo kwa mafungu na sio kwa ujumla..., hao masikini / wanyonge unaowaita huenda kwa kuweza kutoka moro na matenga yao ya nyanya kwa bei nafuu ikakusaidia wewe na familia yako kiafya kwa kupata chakula kwa bei nzuri zaidi na fresh zaidi ili uendelee kupanda train kwa kujinafasi..., Pia hio Train imefadhiliwa na kodi za hao hao pia so called wanyonge
 
Back
Top Bottom