Nauliza, Mwalimu Nyerere nchi ilimshinda kuongoza?

Nauliza, Mwalimu Nyerere nchi ilimshinda kuongoza?

Kuna msemo unasema 'huwezi kutumia akili iliyosababisha tatizo kutatua tatizo'..haishangazi kuona kwamba hakuona tatizo kwenye ujamaa wake,ujamaa kwake ulikua dini,alichukia sana mtu kuwa tajiri
Vijana wa sasa hivi hawajui kama mtu alikuwa na hera yake kipindi hicho alitaka kununua gari ilibidi aanzie kwa mwenyekiti wa eneo husika ili aanze kujadiliwa mpaka ngazi ya mkoa kwamba hiyo hera kaipateje pataje
 
Jamaa una akili sana .

Ni ipi tofauti kati ya Communism na socialism.

In socialism people share wealth but in Communism people share poverty.

Hope nimejibu swali lako.
 
Wazanzibar maisha yao hayakuwa magumu sana kwao kwani kwanza walikuwa wachache na pia walikuwa wanasaidiwa sana na ndugu zao waarabu.
Wazanzibar mapinduzi waliyoyafanya na Muungano waliofanya na Tanganyika viliwaingiza kwenye maisha magumu zaidi.
Wazanzibar wasingefanya yale mapinduzi zanzubar ingekuwa mbali sana kwa sasa
Karume aliukataa ujamaa,mtu wa darasa la tatu tu aliona ujamaa haufai,mwenye masters akaingia mkenge,wazanzibar walikua na maisha ya kiutu kuliko tanganyika
 
Kaptula la Marx na shati la Mao vyote vilimpwaya. Ila Baba wa Taifa amesaidia kwa kiasi kikubwa sana kuwa na Tanzania tuliyonayo leo.

RIP Mzee Mchonga.
 
Binafsi namkubali mwamba Kuibadili nchi kutoka umasikini wa 0 ni kazi ngumu sana , Laiti angekata tamaa Tusingekua hapa..

Watu hawakua na elimu ya kutosha, Serikali haina akiba yeyote, Watu walikua na Mindset ya kusaidiwa na serikali...

Alipata tabu sana mwalimu
Watz hawakua masikini wa 0, mentality ya kuitegemea serikali ilitokana na ujamaa
 
Vijana wa sasa hivi hawajui kama mtu alikuwa na hera yake kipindi hicho alitaka kununua gari ilibidi aanzie kwa mwenyekiti wa eneo husika ili aanze kujadiliwa mpaka ngazi ya mkoa kwamba hiyo hera kaipateje pataje
Stori za vijiweni tena vijiwe vya kahawa.
 
Kawawa aliye kuwa PM,akiwa na elimu ya madrsa TU.
Je munajua Kwa nn alipewa hicho cheo akiwa na elimu ndogo sana. Pengine yy ndio baba wwa taifa hili😎
 
Badala ya kila nyumba kuungwanishwa na umeme wa bei nafuu ,wakaletewa mwenge ili uwamulike mpaka huko vijijini na mipakani, sindio vifkra za MKT hizo
 
Kama umezaliwa miaka ya 70 na hujui yaliyotokea basi utakuwa ni baba/babu mpumbavu sana kuwahi kutokea. Kuhusu Mwalimu Nyerere naweza kusema ana mazuri mengi kuliko mabaya. Aliipenda Tanzania na alitaka kila mtanzania afaidi keki ya taifa ila bahati mbaya akawa haambiliki. Kosa lake kuu ni kuamini yeye anajua kila kitu.
 
Nimezaliwa miaka 1970, nimekutana na maisha magumu Sana, kulikuwa hakuna Sabuni, Sukari, Mafuta na hata nguo.

Watu walivaa magunia, kulikuwa hakuna vyakula na wakati tunapata uhuru aliikuta Tanganyika iko vyema kutoka kwa mkoloni nchi ikiwa vizuri.

Je, Uongozi ulimshinda?
Ndio ndio maana aliji ng'atua mmbo yasimchachie
 
Back
Top Bottom