Nawaheshimu sana walimu, lakini mwalimu yeyote akimfanyia mtoto wangu kama inavyoonyesha picha hii nitamtafuta kokote alipo tumalizane

Umeongea vzuri sana juu ya malezi.

Sasa fikiria juu ya watoto wa majirani, Ambao hawasikii kwa wazazi wao mpaka wapate viboko.

wanaweza kusikia shuleni bira viboko? Na mind you viboko vingi shuleni sio kwa sababu ya kuto kuelewa darasani mara nyingi ni Mambo madogo madogo mfn: Kuwai shuleni, Kufanya Usafi wa mazingira, Kuvaa vzuri na kuvaa nguo safi, Kutokuoiga kelele darasani, N.k

Unawezaje kudisclipline watoto 200 kutoka buza, Tandale na Kimara bila kutumia kiboko, Ikiwa tu wazazi wao, wano miliki watoto wa3 wanatumia kiboko ndo mtoto anaoga
 
Kanuni zako haziwezi kwenda kinyume na sheria/kanuni kuu ambazo zinatambuliwa na mamlaka.

Ukiwa na kanuni zako zinazokiuka kanuni mama basi hizo kanuni zako ni null and void ab initio.
unakuaje mwalimu halafu huna kanuni zako? Elewa utashi ni nini katika kufundisha mada mbalimbali. Hizo sheria ni general objective rules tu
 
Labda upo huko vijijini ambako wazazi wengi hawana mwamko kuhusu haki za watoto wao.

Yaani umuadhibu mtoto pasipo kufuata utaratibu na muongozo halafu kesho uwepo hapo shuleni?

Lahasha! Hata mwalimu mkuu wako ama afisa elimu kata hatokubali kuwa na wewe hapo shuleni maana mimi nitakuuliza wapi ulisaini maelekezo ya mkuu wa shule/mwalimu mkuu kabla ya kutoa adhabu.

Huna maelezo ya kutosha basi tutakutana mahakamani ili ukajibu tuhuma zako.

Kumbuka ushahidi wa mtoto aliyefanyiwa ukatili wa aina yoyote hauhitaji kuthibitishwa beyond reasonable doubt bali uaminifu tu wa mtoto unazingatiwa.

Ndiyo maana mtoto halazimiki kula kiapo pale anapotoa ushahidi bali atatakiwa kusema tu ukweli.

Mwalimu jirekebishe bado nafasi unayo. Ukishupaza shingo utakuja kukumbuka kauli zangu hizi ukiwa matatani.
 
Wewe ni phalla. Utakuwa tas,a maana kama ungekuwa hata na uwezo wa kuzaa tu usingeongea mapupu kama haya.

Mfano huyo mwanafunzi angefariki kwa kipigo hicho bado ungeongea mashudu kama haya?

Afrika ina watu wenye IQ ndogo sana wakiongozwa na wewe.
Phala ni wewe unayedhani kumtoa MTU ujinga na upumbavu ni KAZI ndogo.
Wazazi ni dhahiri malezi yalishawashinda kutwa kuwasakama walimu kwa tuhuma za kijinga.
 
Nimegundua unatatizo la afya ya Akili, fanya hata ufugaji kama mishe ya pembeni ili ushushe stress... Pole utapona
 
Mkuu, kuwa na wanafunzi 200 sidhani kama ni suala la sera mbovu ya elimu. Ni uzembe tu wa serikali katika kuendesha wizara ya elimu
 
Kama huelewi na hujui misingi ya elimu na dhana nzima ya ujifunzaji na ufundishaji na bora upite kimyakimya usilete ubishi tuta reveal upuuzi na upumbavu wako
 
Shukuru tu kwamba umepata mtoto muelewa, anae kuelewa kirahisi. Mimi pia mtoto wangu nilimchapa mara moja tu akiwa na miaka 5 na sikuwahi kurudia tena.
Ila kuna aina ya watoto viboko ni muhimu, bila fimbo hawaelewi chochote
Cha ajabu watoto wanaoongoza kwa nidhamu na ubunifu hii nchi wanatoka shule na familia ambazo haziongozwi kwa viboko.

Napingana na viboko lakini kama lengo ni hilo ambalo huwa mnashikilia "kufundisha", basi sio kwa namna hiyo kwenye picha

Nimebahatika kusoma shule zenye viboko na zisizo na viboko, wengi kati ya walimu wanaotumia viboko hata darasani hawaeleweki!
 
Niliwahi pigwa fimbo zaidi ya 40 mixer mateke na ngumi staff zima imenizunguka utadhani nimeiba library au majengo ya shule alafu kosa lenyew ni utoro kipindi nipo sec😥

Kuna mwalimu alinipiga teke la tumbo mpka nilitapika,kipindi nipo shule ya msingi😥
 
Wewe ni phalla. Utakuwa tas,a maana kama ungekuwa hata na uwezo wa kuzaa tu usingeongea mapupu kama haya.

Mfano huyo mwanafunzi angefariki kwa kipigo hicho bado ungeongea mashudu kama haya?

Afrika ina watu wenye IQ ndogo sana wakiongozwa na wewe.
mbona unawahi kumtukana mwenzio chief 🤔sidhani kama viboko vitano vnaweza muua mwanafunzi
 
Kwa hiyo kwamba alikuwa hana akili
Unajua Magufuli nae alikuwa mwalimu ?
Mkuu, ndio maana basi alikuwa anawapa kichapo sana watoto wake wasipofanya vizuri darasani. Sasa walimu kama Magufuli hawatakiwi kabisa, wana mental issues. Si unaona mentality ya "kuchapa watu bila huruma" aliileta hadi kwenye uraisi? Akamchapa na Ben Saanane. Anaweza kuwa alifanya vizuri katika baadhi ya sehemu,lakini kwenye hili la kuchapa alikuwa na tatizo la afya ya akili
 
Tuonyeshe hao watoto wanaoongooza kwa ubunifu bongo hii ambao hawajawahi kuchapwa viboko.
Wamebuni nini?
 
Kumbe hujanielewa mkuu.

Licha ya wazazi wakatili kutumia viboko dhidi ya watoto wao lakini haijasaidia kuwafanya watoto wawe wasikivu badala yake wamezidi kuwa watukutu.

Tumekuwa tukishuhudia kila siku watoto wanavyokuwa watukutu huko mashuleni licha ya kupewa adhabu za viboko lakini hawabadiliki isipokuwa wanazidi kuwa sugu.

Hata huko mashuleni wanaoadhibiwa kila siku kwasababu ya utoro, kuchelewa kuwahi shule ama sababu nyingine yoyote ni wale wale wa siku zote. Kama viboko vinasaidia kwanini hao watoto wasibadilike?

Kumbuka huwa tunatembelea mashuleni kuongea na walimu pamoja na wanafunzi juu ya mambo mbalimbali ndipo walimu wanapolalamika kwamba watoto ni watukutu licha ya kupewa adhabu ya viboko.

Viboko ni utumwa sio kila kitu cha kuiga. Wakoloni walitumia viboko kama adhabu ya kutweza utu wetu Waafrika lakini hata baada ya kuondoka bado sisi tumeikumbatia bila kujua tunajitweza utu wetu wenyewe.
 
Kama huelewi na hujui misingi ya elimu na dhana nzima ya ujifunzaji na ufundishaji na bora upite kimyakimya usilete ubishi tuta reveal upuuzi na upumbavu wako
Misingi ya elimu ni ipi? Dhana nzima ya kujifunza na ufundishaji ni ipi? Tafuta angle nyingine ya kuhalalisha viboko lakini sio uisingizie elimu!

Unafundisha shule ambazo msingi wake ni viboko ndio maana kwako huo ni msingi na dhana ya ufundishaji lakini shule ambazo zinahitaji ubunifu na kipaji cha mwanafunzi kwa ushirikiano na mwalimu, hizo dhana zinaishia kuwa dhana tu
 
kwanza we ni mwalimu au ngumbaru? Wapi ambako hakuna makabrasha ya haki za wato?
 
Mimi niliwahi pigwa usku kisa Nimegoma kulala🤔can u imagine that mzee 😂kum@nyko
zako mwalimu kali popote mpaka Leo bado nachelewa Kulala kwenye maisha yangu
 
Kuna sehemu nilisoma mwanafunzi auwawa Kwa kupigwa Fimbo na mwalimu wake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…