NCCR Mageuzi yamsimamisha James Mbatia kufanya shughuli za Chama

NCCR Mageuzi yamsimamisha James Mbatia kufanya shughuli za Chama

Bora huko nccr viongozi wapo huru kumuhukumu mwenyekiti wa chama. Upande wa pili mwenyekiti huwa haguswi hata pale anapotoa boko mchana kweupe. Na anapojitokeza wa kujaribu kufuata sheria za chama dhidi ya kiongozi wa chama basi anakiona cha mtema kuni. RIP Chacha Wangwe.
Hakuna mtu ambaye amewahi kunajisi chama kama Magufuli.

Ebu fikiria, wagombea wa ubunge 75% waliopitishwa wajumbe, aliwakata majina yao, na kupachika ya kwake. Fikiria mahali kama Shinyanga, Masele aliyepata kura 360 za wajumbe, alikatwa jina lake, akampachika Katambi aliyepata kura 3. Wote kimya kabisa ndani ya CCM. Hakuna aliyejaribu hata kunyanyua pua kuhoji. Ukisikia udiktetamwingine wote ni uchwara, udikteta hasa, tazama matendo ya marehemu Magufuli. Ukinyanyua pua kuhoji tu, umeuawa, kutekwa au kupotezwa, ikiwa bahati yako nzuri sana unusurike kama Lisu au Mdude.
 
Alie zaidi ya Mbatia ni katiba ya chama chao, tofauti na chama fulani cha upinzani ambacho mwenyekiti ndo yupo juu zaidi ya katiba ya chama chake, ndo maana anaamua lolote atakalo dhidi ya chama na hakuna wa kumuuliza.

Tupe uzoefu wako wa mwenyekiti wa CCM, maana hapa nilipo nachekea kwenye shati.
 
Doh!!namuona mzee wa mama Tanzania Akiunga juhudi mkono
Huyo hawamuwezi! Akishirikiana na Marando, Selasini na nduguye Lamwai nk, walimng'oa Mrema na maguvu yake. Kisha, akaja kung'oka Marando, Selasini mwenyewe na kumwachia chama. Nina imani, hao waliotangaza mapinduzi, watang'oka wao!
 
hawa watu wanajitambua sio yule mbowe kigando kang'ang'ania cheo cha mwenyekiti ,safi nssr
 
Halmashauri Kuu ya Chama cha NCCR Mageuzi imemsimamisha Mwenyekiti wake, James Mbatia kufanya shughuli zote kisiasa za chama hicho mpaka pale atakapoitwa kwenye mkutano mkuu kujieleza.

View attachment 2232853

=======

Halmashauri Kuu ya Chama cha NCCR-Mageuzi imemsimamisha Mwenyekiti wa Chama hicho, James Mbatia na makamu Mwenyekiti Bara, Angelina Mtahiwa kutojihusisha na shuhhuli zozote za chama hadi mkutano Mkuu utakapoitishwa ili wajieleze kuhusiana na tuhuma inazowakubali.

Uwamuzi huo umefanyika leo Jumamosi Mei 21, 2022 kutokana na tuhuma mbalimbali ikiwemo kugombanisha viongozi na kulazimisha kujiuzulu.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu na Mwenyekiti wa azimio hilo, Joseph Selasini amesema pamoja na kusimamishwa kwa viongozi hao pia wamelivunja Baraza la Wadhamini la NCCR na kuteua wajumbe wapya ambao watasajiliwa kwa mujibu wa taratibu zitakazowekwa.

Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini, Sisty Nyahoza amesema walipokea barua kutoka NCCR-Mageuzi kuwa kuna mabadiliko ya wajumbe wa bodi ya wadhamini.

Amesema pamoja na mabadiliko hayo kulikuwa na ajenda nyingine ambayo ni kusimamishwa kwa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti Bara kutokana na maazimio hayo wanasubiri barua rasmi ili kutoa taarifa.

"Tuna orodha yetu tutaenda kuangalia kama mlivyoona wajumbe wapo na akidi imetimia hivyo tunangoja barua rasmi kisha tutaenda kupitia na katiba yao," amesema Nyahoza.

Pia soma > Mgogoro NCCR Mageuzi: Timu Mbatia wachukua ofisi, wasema umefanyika uhaini ndani ya chama,
DaaAAh wamemtimua
 
Katiba yenu inasema ukiwa rais outomatiki unakuwa m/kiti wa chama, chukua mfano kama mkishindwa uchaguzi mala tano mfululizo itakuwaje??
Nioneshe hicho kifungu cha katiba, kinachosema ukiwa raisi unakuwa outomatiki mwenyekiti wa chama. Na kama hauna basi kubali kuwa wewe ni chawa kama chawa wengine waliokubali kutumiwa kama daraja na wajanja wachache, kwa masilahi ya matumbo yao na familia zao.
 
Chadema kwani Mbowe ndio mwanzilishi?

Magufuli alipokuwa akiajisi Chama CCM ilimfanya nini? Au dawa ndio kumuwekea sumu na kusingizia moyo?
Hayo ya sumu unayajua ww. Ila huku muda wako ukifika utake usitake lazima upishe wengine. Hiyo ndio demokrasia ya kweli.
 
Nioneshe hicho kifungu cha katiba, kinachosema ukiwa raisi unakuwa outomatiki mwenyekiti wa chama. Na kama hauna basi kubali kuwa wewe ni chawa kama chawa wengine waliokubali kutumiwa kama daraja na wajanja wachache, kwa masilahi ya matumbo yao na familia zao.
Kwani wewe haufahamu kuwa kila rais mpya wa ccm anakuwa m/kiti wa chama pia??
 
Kwani wewe haufahamu kuwa kila rais mpya wa ccm anakuwa m/kiti wa chama pia??
Unapojadiliana na mtu mwenye akili kama mimi unatakiwa utumie akili yako mwenyewe ili twende sawa, sio utumie akili uliyopandikizwa na mwenyekiti kwa masilahi yake na familia yake. Nimekuomba unioneshe kifungu cha katiba ya ccm kinachosema kuwa mtu akiwa raisi wa JMT anatakiwa pia awe mwenyekiti wa chama chao, umekosa kunionesha, badala yake unaendelea kubwabwaja bila evidence. Hilo ulilozungumzia hapa ni swala la mazoea wala halipo kwenye katiba ya chama. Kama ilivyokuwa imezoeleka mwanzo kwamba raisi wa JMT akitoka bara basi awamu inayofata atatoka zenji. Haya yalikuwa ni mazoea tu wala sio katiba ndio maana uliona utaratibu huo uligeuka mwaka 2005 baada ya kutoka hayati Mkapa bara akaingia Kikwete bara na Kikwete pia akamuachia hayati Magu ambae nae alikuwa m'bara. Kwahiyo swala la mazoea ambalo halipo kikatiba wenye chama wakiamua kupindua meza kama walivyopindua kwenye swala la uraisi wa bara na zenji hakuna atakaepingana nao.
 
Mbowe amefanya kazi nzuri sana kwa miaka mingi ila sasa anapoendelea kukaa madarakani kwa miaka mingi wengi tunamchoka.

Suala la maslahi yake kifedha yupo vizuri sana kupata ndani ya chama mkuu, hili linajulikana.

Chama sasa apewe kijana wa kazi John Heche ili ccm wapotezwe kabisa.
Usiwe na matarajio makubwa sana na mtu kabla hujamwona kwenye hiyo nafasi.Heche unaweza kumwona mzuri kumbe nikwasababu hajakaa kwenye hiyo nafasi.
 
Back
Top Bottom