Sasa kwa mtazamo huo ndio kataa ndoa wanapata point tatu, wanaona kwenye ndoa anayenufaika ni mwanamke for the sake of children, ninaamini kama sheria itabadilishwa ikasema mwanamke na mwanaume wakitalakiana mali zitakazogawanywa ni zile walizochuma pamoja, hata spidi ya wanawake kutaka kuolewa itapungua.
Nasema hivyo kwa sababu sheria imetengenezwa kumlinda mwanamke tu haijawa fair pande zote, yaani jambo likienda kwenye sheria inaonekana mwanamke ana haki na mwanaume hana katika hiyo sheria, lakini tunaona wanawake wanawabambikia wanaume watoto ndani ya ndoa, kuna sheria inasema lolote juu ya hilo, au ni mwanaume anatumia sheria yake na mwanamke anakosa nguvu, Mwanamke akizaa na mwanaume mwingine ndani ya ndoa mnasema kitanda hakizai haramu, ila mwanaume akizaa na mwanamke mwingine kachepuka