Ndoto tunazoota na tafsiri zake

Ndoto tunazoota na tafsiri zake

Hii si ndoto ni script... tunasubiri matangazo toka kwa wadhamini! Muhimu nikukumbushe kwamba ukiona choo ukiwa ndotoni usikitumie, ni mtego!
 
Ndoto zina maana kubwa sana kama ukifuatilia,vilevile ni maonyo na mafunzo.Kuna kitu unamfanyiya wife wako sio kizuli na kinawaletea mgogoro,akichoka ataondoka zake,Mtoto atakuachia,hiyo mwanamke utakayekuja kuwa naye atamtesa sana mwanao pamoja na wewe kishirikina
 
Chamsingi kinachonekana umeshinda lile balaa hata kama ni ndoto mbaya ila umeshinda..na imekuwa hivi baada ya kutaja jina laYesu na kumtupia yule mchawi kwenye miba.
 
😛😛😛😛atakuja mtaalam wa ndoto akwambie,maana yake ni kwamba unakaribia kupanda cheo kazini,na kupata mtoto wa pili tena mwenye ulbinism.mambo ya ndoto na tafsiri yanavuruga.ndio maana huwa nakausha tu.ndoto pekee inayonivurugaga nikiota nimebanwa na tumbo jirani na kichaka.
 
Usiku wa kuamkia leo nimeota ndoto ambayo nimeshindwa kuitafsiri kabisa, picha linaanza ilikua usiku, niko mimi, wife na mwanangu mdogo wa miaka miwili maeneo ya Kamata DSM kama unatokea Posta kuelekea mataa ya Kamata.

Baada ya kuvuka reli kabla ya mataa nakutana na mdada amevaa jezi ya yanga ile ya njano.....ananiuliza nimuelekeze mtaa wenye mafundi...nami namuelekeza mtaa wa Makamba, tukaendelea mbele na wife,wkt huo mwanang nimembeba kifuani nikiwa nimemkumbatia(ndo style nnayopenda kumbeba tukiwa matembezini)...
bro katka vitu mungu huzitumia kutuma ujumbe ni ndoto. pia shetani hutumia hio hio nafas kukutisha. kwa ndoto km hizo inahusiana tu na ulozi wa kawaida
 
Habari wana JF, pamoja na shughuli zote salamu muipokee.

Kiukweli nimekua na mfululizo wa ndoto za kutisha, naota majoka ya kila aina makubwa ya kila rangi hadi kufikia kukata tamaa hadi ndotoni

Msaada hapa wataalam wenye experience na hizi mambo.
Nawasilisha[emoji29]
 
Mpendwa katika Bwana biblia inasema,, 🤦🤔 ahh nimesahau sijui ni kifungu gani? 😜 Ila Mkuu Usijali Sana inaonekana kuna adui zako pembeni sio watu wazuri na hiyo ndoto umeota unapambana nao wameshindwa kwa jina la YESU, Cha msingi zidisha tu maombi, sala kwako na familia yako🙏🤪🏃🏃
 
- Ndoto haina maana yeyote maana inatengenezwa na akili (subconscious) yako mwenyewe.

- Subconsciously inawezekana una ile wanasaikolojia wanaita GUILT CONSCIENCE. [emoji1][emoji1]

- Achana na makandokando, kama unamawazo au umeshafanya matendo ya usaliti muombe Mungu akuongoze, la sivyo wasiwasi wako wa kuitenganisha familia utatimia.
Mmh
 
Habari wana JF, pamoja na shughuli zote salamu muipokee.

Kiukweli nimekua na mfululizo wa ndoto za kutisha, naota majoka ya kila aina makubwa ya kila rangi hadi kufikia kukata tamaa hadi ndotoni

Msaada hapa wataalam wenye experience na hizi mambo.
Nawasilisha[emoji29]
Unaota ukiwa wapi,yaani eneo gani? Nyumbani,kazini...ni

Na unaota wanafanyaje hao nyoka,wanakufukuza au?
Ni rangi zipi unaziona kwa hao nyoka?
Na mwisho wa ndoto ukoje?

Tuanzie hapa kabla ya kutafsiri na kujua ujumbe!

JESUS IS LORD[emoji120]
 
Back
Top Bottom