Ndugai: Ujenzi wa bandari ya Bagamoyo uendelee, Dkt. Magufuli alishauriwa vibaya

Ndugai: Ujenzi wa bandari ya Bagamoyo uendelee, Dkt. Magufuli alishauriwa vibaya

Kuna watu fahamu zinaanza kurudi- ile Kinga yako ya kutokushitakiwa ameshauriwa vibaya?
Hapa sio fahamu kurudi bali ni fahamu kuhama. Yaani Bagamoyo iendelezwe kwa sharti bandari Dat, Tanga, Mtwara etc zisiendelezwe na mwekezaji apewe lease 99 years. TZ inafaidika au inaliwa? Au aliyeuidhinisha huo mradi kabla kajipenyeza kwa hiyo kamati na Ndugai wake akijua wanamwogopa bado?
 
Wekeni mkataba wazi acheni uhuni wa presentation,sisi inatusaidia nini hiyo presentation?,mnaahidiana mipesa kutuibia sisi ili mpitishe mikataba ya wizi,huu ni upumbavu wa hali ya juu kabisa!
 
Namshangaa Dr Abas bado anaishi kwenye kivuli cha mzee Magu ashtuke mapema vingnevyo atavuna mabua Kama mihimil mikuu inabadil msimamo akae chonjo

Lakn hapa nawaza tu kidarasa la chekechea B KWEL ILE SAFARI YA WAZIR WA CHINA ILIKUWA YA HERI JAMANI HEBU TUISHI HUMU HUKU TUKITAFAKARI UJIO WA YULE WAZIRI
 
Mkuu Yoda,

Naomba nami nipandie kwenye hoja yako hii ya "kutokuwa na Bunge Huru."

Naomba sasa tushirikiane kuwastua hawa wabunge wa CCM waliomo kwenye Bunge hilo.

Mfadhiri wao mkuu, KAONDOKA; hakuna tena anayewashikilia wasiweze kulifanyia haki taifa hili.

Kitu cha kwanza wanachopaswa kukifanya ni kusafisha takataka zilizoko huko Bungeni kwao kwa kuwaondoa katika ngazi za uongozi wapuuzi kama huyu Ndugai.

Ndugai bila ya mbeleko wa mtu mwingine (kama Magufuli), hana nguvu ya kumuyumbisha mtu yeyote. Huyu wamkatae asiwaongoze, wamwondoe haraka.

Wakishafanya hivyo, hapo ndipo itatakiwa wafanye kazi za wananchi ambao kiuhakika hawakuwachagua kwa hiari zao. Hapo watakuwa wamelifanyia taifa lao haki, na wartastahili kupewa heshima.
Mkuu haya mambo yalikuwa wazi kabisa. Ndungai ni mchumia tumbo tena kilaza wa kutupwa. Magufuli alikuwa anapenda watu kama hawa. Kichwani hamna kitu tumboni kuna tani mbili. Alidhani kina Lissu ni maadui kumbe walikuwa watu wema sana na wanataka kumsaidia afanye vizuri. Ohooo. mbona kila alichoasisi Magufuli kinasambaratika kwa kasi ya ajabu namna hii! Wale waliokuwa wanamsifia mchana kutwa ndiyo wamegeuka wapondaji. Haki watu wangekuwa wanarudi kutoka kaburini Magufuli asingeamini kinachotokea sasa hivi.
 
leo ndio nimeona wanasiasa hawawezi kuiona pepo kwa unafiki wao,huyu huyu ndugai aliwekwa pale na mzee leo anaongea haya kweli
Unga ulipokuwa mashariki, aliufuata kwa mapambio, ikiwemo kutaka kutekeleza harakati za kumwongezea mungu mtu muda. Leo unga unaelekea magharibi, anaufuata.
Kumbuka huyu ni mkuu wa mhimili. Poor Ndugai
 
Ndugai ungeoneka wa maana ungeshauri wkt jiwe lipo. Sasa hv hata fote bado mnagawana fito
 
Hawa si ni ''wachapa kazi '' wa Magufuli lakini? Si ndio alikuwa anawaamini na kusema wana uzalendo? Maskini mzee wa watu hakujua alikuwa amezungungukwa na mbwa mwitu. Alidhani kina Lissu ndiyo maadui zake kumbe walikuwa wazalendo na hawa kina Ndungai ndiyo maadui wa Taifa.

Mama Samia kaa chonjo kuna kundi la wezi wanataka kurudi hewani kwa spidi ya mwewe hata arobaini haijaisha

Walifungiwa kwenye banda la mifugo sasa wanatoka kwa kasi kurudi kula mazao shambani

Wanaanza kukunjua mikucha yao mchana kweupe hata bila haya

Mzee Ndugai na uzee ule rushwa hata kweli anafanya decision kuwa mradi mzuri kwa kuangalia presentation ya mchina !!! Nimekubali CCM tunaingiza baadhi ya watu wenye upeo mdogo bungeni Ndugai akiwemo.
 
Watanzania tunapenda kuchonganisha sana, huo ndio ulikuwa msimamo wa Ndugai from day na alishatoa hiyo story yake ya China before.

Nani sahihi kati ya Ndugai na Magufuli wabunge badala ya kuburuzwa ku support au kupinga kitu ambacho awakijui in details wangeomba ushahidi utakaowasaidia na wao kuamua.

Ndugai apeleke proposal ya mradi bungeni ijadiliwe ili maamuzi ya wabunge yawe kutokana na information sahihi sio kutumia opinion zao kulazimisha agenda.
 
Spika wa Bunge ameshauri mradi wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo uendelee kwa sababu Magufuli alishauriwa vibaya, hii ni baada ya kamati ya Bunge ya bajeti kushauri kuwa serikali iangalie kuhusu kuendelea na mradi huo.

Ndugai amesema kuwa mradi huo utakuwa na faida kubwa kwa Watanzania na tukichelewa hatutauta tena.

Magufuli alisema mradi huo ulikuwa ni hasara kwani ulikuwa na masharti magumu ikiwemo ya kuzuia bandari yoyote kuendelezwa, wala TRA kukusanya kodi na kupewa lease kwa miaka 99.




Pia soma: Spika Job Ndugai: Kutokana na masharti ya Mradi wa Bandari Bagamoyo, ni sahihi Serikali kuusitisha

Du! Tujifunze kuweka akiba ya maneno, "mkono wa chuma" kafa leo Ndugai anamgeuka kweli wanafiki ndani ya CCM wapo wengi
 
Ila hasa watu jamani [emoji848]

Kitu inaitwa aibu huwa hawana asee

Kabla jogoo hajawika mara tatu ni raia zimemkana
 
Mama Samia kaa chonjo kuna kundi la wezi eanataka kurudu hewani kwa spidi ya mwewe hata arobaini haijaisha walifungiwa kwenye banda la mifugo sasa wanatoka kwa kasi kurudi kula mazao shambani

Wanaanza kukunjua mikucha yao mchana kweupe hata bila haya

Mzee Ndugai na uzee ule rushwa hata kweli anafanya decision kuwa mradi mzuri kwa kuangalia presentation ya mchina !!! Nimekubali CCM tunaingiza baadhi ya watu wenye upeo mdogo bungeni Ndugai akiwemo.
Ndiyo maana tulikuwa tunalilia uchaguzi huru. Haya ni matokeo ya Magufuli kuokoteza mabaki huku na huko.
 
Du! Tujifunze kuweka akiba ya maneno, "mkono wa chuma" kafa leo Ndugai anamgeuka kweli wanafiki ndani ya CCM wapo wengi
Hao ndio watanzania wala usishangae, we jiulize una marafiki wangapi ambao ‘piga, uwa’ lazima wawepo.

Kama una marafiki ishirini basi mmoja au wawili tu siku nyumba yako ikijaa maji na mafuriko ndio watakufungulia mlango ujibanze na familia yako.

Tuna associates in life but not friends.
 
Ndio maana kwenye maisha yangu kamwe simtumaini wala kumtegemea mwanadamu mwenzangu.
Ina maana Ndugai amepata maono mengine mapya?
 
HApo kwenye bold....inaanzia kwenye familia, mtaani, makazini hadi TAiFA
Ajabu walioshauri mradi usijengwe ndiyo hao hao wanashauri mradi ujengwe.

Hiyo ndiyo rangi halisi yetu wabongo😇
 
Ni ngumu sana kuuwa legacy ya Magufuli na uzuri jamaa alikuwa anasema hadharani watanzania wanajua.


Ndiyo maana mpinga legacy ya Magufuli hatajibiwa na Magufuli wala watoto wa Magufuli mbali atajibiwa na watanzania.


Kama Ndugai anasema Magufuli alishauriwa vibaya itabidi atueleze huo mkataba unasemaje tofauti na aliyosema Magufuli.

Watakaohoji haya ni watanzania.


Ni kama waliojaribu kuuwa legacy ya Nyerere huwa wanatapa upinzani mkali hadi leo wakati Nyerere alishafariki zaidi ya miaka 20 iliyopita.
Watu huwa wanarejea hotuba tu.

Maneno huiishi
 
Back
Top Bottom