Ndugu zangu upande wa baba wanainua vita kali juu yangu

Ndugu zangu upande wa baba wanainua vita kali juu yangu

Nimerudia kusoma uzi mara tatu nione sehem ndugu zako walipokufanyia ubaya sijaona, punguza kuwafikiria watu vibaya umejihami kiasi kwamba kila mtu unamuona mbaya
Sawa mkuu hakuna shida.asante
 
Pole mrembo...yasikuathiri. Cha msingi puuzia maneno utakaoletewa. Usiongeze neno kwa yale yatakayoletwa kwako na wala usijenge uadui kwa maneno yatakayoletwa kwako na nduguzo.

Kama uliweza kuwaleta pamoja watu waliotengana miaka 20 basi unaweza kuwaleta pamoja shangazi na baba zako.
Nafikiri niwapuuzie tu mkuu.kuwaleta pamoja sidhani Kama itatokea
 
Pole mkuu kuna ndugu jau sana nina experience inaendana na yako nakuelewa vzuri. Me washajaribu hadi kunitenganisha na familia yangu kimkakati kabisa, washasema sana sitatotoboa Mungu si Asumani sahv napigwa vizinga hatari na kusomewa mashtaka ya watoto wao eti niwasaidie kuwashauri.

Ndo ile nakuheshimu sana na kama una shida ntakusaidia kama naweza ila tofauti na hapo tutaonana misibani na kwenye sherehe, funga vioo. Plus kuna mtu apo kasema usiulize wala kutaka kujua wanakusemaje, yes 100%.. what u dont know, can't hurt yo feelings.
Asante sana.
Ninashukuru kwa ushuhuda pia
 
Watu kama wewe huwa hawana maisha marefu bro... Anytime anything can happen!!!
Mzee wangu aliwahi nipa somo kwamba "watu wa aina tatu huwa hawana maisha marefu hapa dunian...... Kuwa mwelevu kweny kundi la wajinga (wewe upo hapa), migogoro ya ardhi na mwsho kabisa akasema kutembea na mke wa mtu


Anyway kuwa makini bro... Allah akutangulie🚶🚶
I’m a woman mkuu.

Mimi nitakuwa wa kwanza kuwa na maisha marefu.

Hallelujah.

Nakushukuru sana kwa comment yako mkuu
 
Kwanza pole sana Mkuu, ndio Walimwengu walivyo na ushauri wangu ni huu.
1. Acha kuwa na roho ya huruma wazingatie watu wanaokuhusu
2. Wakali mwingine punguza sana hofu ya mambo mabaya kukutokea
3. Ishi vizuri kwa kuzingatia kanuni za imani yako.
4. Punguza kuwaogopa maana unaitengenezea akili yako hali kuwaona ni kama adui zako.
5. Imani yako ifuate kwa asilimia zote iwe ni Kanisani au Msikitini
6. Wapende Baba na Mama yako maana has ndio miungu yako hapa duniani hao ndugu wa Baba yako achana nao ikiwezekana wapige marufuku na wakizidi kukughasi wachukulie hatua za kisheria.
Nikutakie wakati mzuri japo kuna mambo mengi hujafunguka na ndio maana nimeshindwa kutokea ushauri wa moja kwa moja
 
Habari ya wakati huu JF members, nina imani mnaendelea salama. Kama kichwa cha habari kinavyojieleza, naomba kushare japo kidogo hili swala ninalolipitia.

Mimi na familia yangu(baba, mama, kaka na wadogo zangu) hatukutoka kwenye familia ya yenye uwezo. Maisha tuliyokuwa tunayaishi tangu nikiwa mdogo binafsi nilikuwa siyapendi kabisa na niliapa mimi wala watoto wangu hatutakuja kuishi maisha maisha niliyoyaishi nikiwa mdogo na niliapa kuja kubadilisha historia ya wazazi wangu.

Kwa ufupi tu haikuwa kazi rahisi lakini Mungu ni mwema, nililoliomba kwa miaka mingi limefanikiwa kwa asilimia 92. Ndugu zetu kwa upande wa baba kwanzia baba wadogo, babu, mashangazi walikuwa hawatukubali wala kutuombea mema.

Walituhesabu sisi ni fungu la kukosa, maisha hayakuwa rahisi lakini Mungu mwingi wa rehema amenitumia mimi kubadilisha familia ili nizidi kuongeza Utukufu.

Nitaruka ruka kidogo ili kufikisha ujumbe maana ni ndefu sana, najua hii ni personal life lakini nimeamua kuileta huku sidhani Kama kuna ubaya.

Wazazi wangu walitengana kama miaka 20 na zaidi iliyopita kila mtu akaishi kivyake, hali ya utengano iliunyong’onyeza sana moyo wangu kuna wakati nilikuwa nikienda kumsalimia mama najikuta namkumbuka baba yangu (hapo sijui alipo), nikajiuliza ni kwanini ninaumia hivi juu ya utengano huu wa wazazi wangu, nikajisemea moyoni hapana mimi ndie ninaetakiwa kuirudisha hii familia pamoja tena.

Mungu alivyomwingi wa rehema akanibariki nikafanikiwa kujenga kijumba kidogo kwa ajili ya wazazi wangu (nikamrudisha kwanza baba nyumbani) baada ya baba kurudi vita vya ndugu vikaibuka nilikuwa na maswali mengi sana nikajisemea moyoni badala hawa ndugu wamshukuru Mungu ndugu yao amerudi nyumbani wao wanaanza kumpiga vita.

Maisha yakaendelea wakati Niko endelea kufanya utaratibu na kuzungumza na wazee ili kama kuna mila zifanyike başı mama yetu arudi nyumbani.

Wakati baba yuko nyumbani ugomvi ukawa ni mwingi sana na mashangazi, mara leo limetokea hili kesho lile nikasema ngoja nikate mzizi wa fitna maana ilikuwa inaonekana kama mama angerudi başi Vita ingekuwa kubwa ikabidi nizungushe ukuta kote kupunguza maneno.

Nikajisemea mpaka mtu aje kugonga geti kuanzisha ugomvi basi atakuwa amedhamiria kweli.

Baada ya kumalizana na ujenzi wa ukuta nikamrudisha mama nyumbani so kwa sasa wa naishi kwa upendo na Amani ingawa majaribu ya upande wa ndugu wa baba hayana budi kuja lakini Mungu anamuepusha nayo.

Sasa kwanini nimeleta uzi huu ni kuwa ile vita iliyoanzishwa kwa wazazi imenigeukia mimi. Baba wadogo na mashangazi wananiombea maanguko, magonjwa hatarishi na hata kifo jamani!

Moyo wangu unavuja damu, koşa langu liko wapi? Ninastahili maombi mabaya namna hii? Moyo wangu unamajeraha.

Nimeifupisha naomba kuiwasilisha.
Kumbe wanakuombea, Mimi nikajua labda kuna mtu amekukata mkono au Miguu hapo lingekuwa suala lingine, ndugu yangu kuombewa mabaya siyo wewe peke yako unayepitia hiyo Hali.


Wewe mtegemee Mungu na endelea kufanya lililo HAKI , pengine Mungu amekubariki basi usitumie pia uwezo wako kuadhibu wengine maana huwa ina backfire, ugomvi WA wazazi achana nao wanajijua wenyewe, huenda kuna namna wazazi wako au Baba alikwaruzana na ndugu zake , sasa badala ya yeye kurudi kwa ndugu zake kuomba msamaha analazimisha ionekane kuwa anaonewa, hiyo haipedezi na ugomvi hautokoma.


Vita ya wazazi waachie wenyewe usichochee Moto, unachoweza kufanya ni kuwaunganisha kupitia viongozi wa Imani either Masheikh au wachungaji waone namna gani ya kuondoa tofauti zao ili maisha yaendelee.


Maisha ni mafupi Sana kuendelea kuishi kwa chuki .
 
Habari ya wakati huu JF members, nina imani mnaendelea salama. Kama kichwa cha habari kinavyojieleza, naomba kushare japo kidogo hili swala ninalolipitia.

Mimi na familia yangu(baba, mama, kaka na wadogo zangu) hatukutoka kwenye familia ya yenye uwezo. Maisha tuliyokuwa tunayaishi tangu nikiwa mdogo binafsi nilikuwa siyapendi kabisa na niliapa mimi wala watoto wangu hatutakuja kuishi maisha maisha niliyoyaishi nikiwa mdogo na niliapa kuja kubadilisha historia ya wazazi wangu.

Kwa ufupi tu haikuwa kazi rahisi lakini Mungu ni mwema, nililoliomba kwa miaka mingi limefanikiwa kwa asilimia 92. Ndugu zetu kwa upande wa baba kwanzia baba wadogo, babu, mashangazi walikuwa hawatukubali wala kutuombea mema.

Walituhesabu sisi ni fungu la kukosa, maisha hayakuwa rahisi lakini Mungu mwingi wa rehema amenitumia mimi kubadilisha familia ili nizidi kuongeza Utukufu.

Nitaruka ruka kidogo ili kufikisha ujumbe maana ni ndefu sana, najua hii ni personal life lakini nimeamua kuileta huku sidhani Kama kuna ubaya.

Wazazi wangu walitengana kama miaka 20 na zaidi iliyopita kila mtu akaishi kivyake, hali ya utengano iliunyong’onyeza sana moyo wangu kuna wakati nilikuwa nikienda kumsalimia mama najikuta namkumbuka baba yangu (hapo sijui alipo), nikajiuliza ni kwanini ninaumia hivi juu ya utengano huu wa wazazi wangu, nikajisemea moyoni hapana mimi ndie ninaetakiwa kuirudisha hii familia pamoja tena.

Mungu alivyomwingi wa rehema akanibariki nikafanikiwa kujenga kijumba kidogo kwa ajili ya wazazi wangu (nikamrudisha kwanza baba nyumbani) baada ya baba kurudi vita vya ndugu vikaibuka nilikuwa na maswali mengi sana nikajisemea moyoni badala hawa ndugu wamshukuru Mungu ndugu yao amerudi nyumbani wao wanaanza kumpiga vita.

Maisha yakaendelea wakati Niko endelea kufanya utaratibu na kuzungumza na wazee ili kama kuna mila zifanyike başı mama yetu arudi nyumbani.

Wakati baba yuko nyumbani ugomvi ukawa ni mwingi sana na mashangazi, mara leo limetokea hili kesho lile nikasema ngoja nikate mzizi wa fitna maana ilikuwa inaonekana kama mama angerudi başi Vita ingekuwa kubwa ikabidi nizungushe ukuta kote kupunguza maneno.

Nikajisemea mpaka mtu aje kugonga geti kuanzisha ugomvi basi atakuwa amedhamiria kweli.

Baada ya kumalizana na ujenzi wa ukuta nikamrudisha mama nyumbani so kwa sasa wa naishi kwa upendo na Amani ingawa majaribu ya upande wa ndugu wa baba hayana budi kuja lakini Mungu anamuepusha nayo.

Sasa kwanini nimeleta uzi huu ni kuwa ile vita iliyoanzishwa kwa wazazi imenigeukia mimi. Baba wadogo na mashangazi wananiombea maanguko, magonjwa hatarishi na hata kifo jamani!

Moyo wangu unavuja damu, koşa langu liko wapi? Ninastahili maombi mabaya namna hii? Moyo wangu unamajeraha.

Nimeifupisha naomba kuiwasilisha.
Sasa kwanini nimeleta uzi huu ni kuwa ile vita iliyoanzishwa kwa wazazi imenigeukia mimi. Baba wadogo na mashangazi wananiombea maanguko, magonjwa hatarishi na hata kifo jamani!
[emoji3064][emoji3064][emoji848][emoji848][emoji2827][emoji2827]
 
Back
Top Bottom