Ndugu zangu upande wa baba wanainua vita kali juu yangu

Ndugu zangu upande wa baba wanainua vita kali juu yangu

Asante sana mku kWa ushauri.

Kuna kitu jirani alinisaidia so nikaenda kwakwe kumshukuru so tukiwa katikati ya mazungumzo nikamskkia shangazi yangu anamuita so ikabidi aende kumsikiliza.alipomaliza kilichomleta ikabidi sasa aanze mada juu yangu alichokiongea ndicho kilichousononesha mayo wangu🥺
Wapotezee fanya kama vile hauna ndugu maisha yaendelee kipenzi changu
 
Habari ya wakati huu JF members, nina imani mnaendelea salama. Kama kichwa cha habari kinavyojieleza, naomba kushare japo kidogo hili swala ninalolipitia.

Mimi na familia yangu(baba, mama, kaka na wadogo zangu) hatukutoka kwenye familia ya yenye uwezo. Maisha tuliyokuwa tunayaishi tangu nikiwa mdogo binafsi nilikuwa siyapendi kabisa na niliapa mimi wala watoto wangu hatutakuja kuishi maisha maisha niliyoyaishi nikiwa mdogo na niliapa kuja kubadilisha historia ya wazazi wangu.

Kwa ufupi tu haikuwa kazi rahisi lakini Mungu ni mwema, nililoliomba kwa miaka mingi limefanikiwa kwa asilimia 92. Ndugu zetu kwa upande wa baba kwanzia baba wadogo, babu, mashangazi walikuwa hawatukubali wala kutuombea mema.

Walituhesabu sisi ni fungu la kukosa, maisha hayakuwa rahisi lakini Mungu mwingi wa rehema amenitumia mimi kubadilisha familia ili nizidi kuongeza Utukufu.

Nitaruka ruka kidogo ili kufikisha ujumbe maana ni ndefu sana, najua hii ni personal life lakini nimeamua kuileta huku sidhani Kama kuna ubaya.

Wazazi wangu walitengana kama miaka 20 na zaidi iliyopita kila mtu akaishi kivyake, hali ya utengano iliunyong’onyeza sana moyo wangu kuna wakati nilikuwa nikienda kumsalimia mama najikuta namkumbuka baba yangu (hapo sijui alipo), nikajiuliza ni kwanini ninaumia hivi juu ya utengano huu wa wazazi wangu, nikajisemea moyoni hapana mimi ndie ninaetakiwa kuirudisha hii familia pamoja tena.

Mungu alivyomwingi wa rehema akanibariki nikafanikiwa kujenga kijumba kidogo kwa ajili ya wazazi wangu (nikamrudisha kwanza baba nyumbani) baada ya baba kurudi vita vya ndugu vikaibuka nilikuwa na maswali mengi sana nikajisemea moyoni badala hawa ndugu wamshukuru Mungu ndugu yao amerudi nyumbani wao wanaanza kumpiga vita.

Maisha yakaendelea wakati Niko endelea kufanya utaratibu na kuzungumza na wazee ili kama kuna mila zifanyike başı mama yetu arudi nyumbani.

Wakati baba yuko nyumbani ugomvi ukawa ni mwingi sana na mashangazi, mara leo limetokea hili kesho lile nikasema ngoja nikate mzizi wa fitna maana ilikuwa inaonekana kama mama angerudi başi Vita ingekuwa kubwa ikabidi nizungushe ukuta kote kupunguza maneno.

Nikajisemea mpaka mtu aje kugonga geti kuanzisha ugomvi basi atakuwa amedhamiria kweli.

Baada ya kumalizana na ujenzi wa ukuta nikamrudisha mama nyumbani so kwa sasa wa naishi kwa upendo na Amani ingawa majaribu ya upande wa ndugu wa baba hayana budi kuja lakini Mungu anamuepusha nayo.

Sasa kwanini nimeleta uzi huu ni kuwa ile vita iliyoanzishwa kwa wazazi imenigeukia mimi. Baba wadogo na mashangazi wananiombea maanguko, magonjwa hatarishi na hata kifo jamani!

Moyo wangu unavuja damu, koşa langu liko wapi? Ninastahili maombi mabaya namna hii? Moyo wangu unamajeraha.

Nimeifupisha naomba kuiwasilisha.
Kimbia mkuu, hao wamepanga kukumaliza.
 
Wafungie vioo wanakusaidia nin kwenye maisha yako?
Huyu jamaa atakuwa mtu wa kusikiliza sana na kufuatilia mambo ya nyumbani kwao kama sio kijijini kwao. Kwa hiyo kila kinachosemwa anachukua. Hivi ukifunga vioo ukadeal tu na wazazi wako na hao wazazi ukawaachia wenyewe mambo ya kijijini kwao, utasikia wapi hizo shida?

Ndio tunavyofanya wengine, ujinga ujinga wa kijijini hauna nafasi na hakuna kuruhusu informers. Watasema wee wanakuta no reactions kwa sababu sina habari kabisa. Sasa shida kama hizi zinawakuta watu wapo mjini, lakini sikio lipo kijijini
 
Kwanza pole sana Mkuu, ndio Walimwengu walivyo na ushauri wangu ni huu.
1. Acha kuwa na roho ya huruma wazingatie watu wanaokuhusu
2. Wakali mwingine punguza sana hofu ya mambo mabaya kukutokea
3. Ishi vizuri kwa kuzingatia kanuni za imani yako.
4. Punguza kuwaogopa maana unaitengenezea akili yako hali kuwaona ni kama adui zako.
5. Imani yako ifuate kwa asilimia zote iwe ni Kanisani au Msikitini
6. Wapende Baba na Mama yako maana has ndio miungu yako hapa duniani hao ndugu wa Baba yako achana nao ikiwezekana wapige marufuku na wakizidi kukughasi wachukulie hatua za kisheria.
Nikutakie wakati mzuri japo kuna mambo mengi hujafunguka na ndio maana nimeshindwa kutokea ushauri wa moja kwa moja
Chakorii zingatia hii.
 
Halafu jingine Chakorii inaonekana unapenda sana vita vya maneno kwa sababu umejipata nakushauri kama Kaka/Mdogo wako achana nao usijibizane nao maana wao wapo wengi na wewe uko pekee yako huwawezi watakuvuruga sana na utajikuta unafanya mambo yatakayo kugharimu wewe mwenyewe. Wapotezee kabisa na usijibizane nao. Control your tongue 😝
 
Huyu jamaa atakuwa mtu wa kusikiliza sana na kufuatilia mambo ya nyumbani kwao kama sio kijijini kwao. Kwa hiyo kila kinachosemwa anachukua. Hivi ukifunga vioo ukadeal tu na wazazi wako na hao wazazi ukawaachia wenyewe mambo ya kijijini kwao, utasikia wapi hizo shida?

Ndio tunavyofanya wengine, ujinga ujinga wa kijijini hauna nafasi na hakuna kuruhusu informers. Watasema wee wanakuta no reactions kwa sababu sina habari kabisa. Sasa shida kama hizi zinawakuta watu wapo mjini, lakini sikio lipo kijijini
Anaonekana anapenda sana maneno na majibizano huyu kwa sababu ameshakuwa somebody na hii itam cost yeye mwenyewe
 
Kuna muda ndugu huwa wanazingua kinoma yani !
Hapo huna kosa lolote ukute wanavoona wivu tu kwani walifurahia anguko na utengano wa wazazi wako na hawapendi mafanikio yako!
Ubarikiwe sana hakuna kipindi huwa napata amani kama kipindi ambapo nawajali wazazi!

Cc Smart911
 
Kuna muda ndugu huwa wanazingua kinoma yani !
Hapo huna kosa lolote ukute wanavoona wivu tu kwani walifurahia anguko na utengano wa wazazi wako na hawapendi mafanikio yako!
Ubarikiwe sana hakuna kipindi huwa napata amani kama kipindi ambapo nawajali wazazi!

Cc Smart911
Huyu kayakanyaga Mwenyewe kwa sababu ianonekana anapenda kurushiana nao maneno lazima wamvuruge tu. Mpaka anakuja humu washamvuruga abadirike aache kujibizana nao hiyo ndio last solution's
 
Asante sana mku kWa ushauri.

Kuna kitu jirani alinisaidia so nikaenda kwakwe kumshukuru so tukiwa katikati ya mazungumzo nikamskkia shangazi yangu anamuita so ikabidi aende kumsikiliza.alipomaliza kilichomleta ikabidi sasa aanze mada juu yangu alichokiongea ndicho kilichousononesha mayo wangu🥺
Manyanza sio maneno ya kuambiwa mkuu.nimemsikia mwenyewe kwa masikio yangu sijasimuliwa na akawataja ndugu zake wengine ambao wako pamoja nae.

Naweza kusema kuwa ni Mungu ndie aliyesababisha nimsikie kwa kinywa chake maana nisingeamini kama ningesimuliwa na mtu.

Nilikuwa nawapanda wote
 
Huyu kayakanyaga Mwenyewe kwa sababu ianonekana anapenda kurushiana nao maneno lazima wamvuruge tu. Mpaka anakuja humu washamvuruga abadirike aache kujibizana nao hiyo ndio last solution's
Sasa ndugu yangu naona unaanza kunibandikia maneno kinywani.ikikupendeza uache kuniwekea maneno kinywani si ndio mkuu.shukrani sana
 
Pole kama umekwazika na sio dhamiraĺ yangu kufanya hivyo.
Sijakwazika mkuu isipokuwa niliona unavyoandika ni kama tunaishi wote kila siku so ukawa unajua fika Napenda kurushiana maneno.

naona ulikuwa umeng’anga’ana na tuhuma tu mkuu

Nashukuru kwa ushauri pia
 
Habari ya wakati huu JF members, nina imani mnaendelea salama. Kama kichwa cha habari kinavyojieleza, naomba kushare japo kidogo hili swala ninalolipitia.

Mimi na familia yangu(baba, mama, kaka na wadogo zangu) hatukutoka kwenye familia ya yenye uwezo. Maisha tuliyokuwa tunayaishi tangu nikiwa mdogo binafsi nilikuwa siyapendi kabisa na niliapa mimi wala watoto wangu hatutakuja kuishi maisha maisha niliyoyaishi nikiwa mdogo na niliapa kuja kubadilisha historia ya wazazi wangu.

Kwa ufupi tu haikuwa kazi rahisi lakini Mungu ni mwema, nililoliomba kwa miaka mingi limefanikiwa kwa asilimia 92. Ndugu zetu kwa upande wa baba kwanzia baba wadogo, babu, mashangazi walikuwa hawatukubali wala kutuombea mema.

Walituhesabu sisi ni fungu la kukosa, maisha hayakuwa rahisi lakini Mungu mwingi wa rehema amenitumia mimi kubadilisha familia ili nizidi kuongeza Utukufu.

Nitaruka ruka kidogo ili kufikisha ujumbe maana ni ndefu sana, najua hii ni personal life lakini nimeamua kuileta huku sidhani Kama kuna ubaya.

Wazazi wangu walitengana kama miaka 20 na zaidi iliyopita kila mtu akaishi kivyake, hali ya utengano iliunyong’onyeza sana moyo wangu kuna wakati nilikuwa nikienda kumsalimia mama najikuta namkumbuka baba yangu (hapo sijui alipo), nikajiuliza ni kwanini ninaumia hivi juu ya utengano huu wa wazazi wangu, nikajisemea moyoni hapana mimi ndie ninaetakiwa kuirudisha hii familia pamoja tena.

Mungu alivyomwingi wa rehema akanibariki nikafanikiwa kujenga kijumba kidogo kwa ajili ya wazazi wangu (nikamrudisha kwanza baba nyumbani) baada ya baba kurudi vita vya ndugu vikaibuka nilikuwa na maswali mengi sana nikajisemea moyoni badala hawa ndugu wamshukuru Mungu ndugu yao amerudi nyumbani wao wanaanza kumpiga vita.

Maisha yakaendelea wakati Niko endelea kufanya utaratibu na kuzungumza na wazee ili kama kuna mila zifanyike başı mama yetu arudi nyumbani.

Wakati baba yuko nyumbani ugomvi ukawa ni mwingi sana na mashangazi, mara leo limetokea hili kesho lile nikasema ngoja nikate mzizi wa fitna maana ilikuwa inaonekana kama mama angerudi başi Vita ingekuwa kubwa ikabidi nizungushe ukuta kote kupunguza maneno.

Nikajisemea mpaka mtu aje kugonga geti kuanzisha ugomvi basi atakuwa amedhamiria kweli.

Baada ya kumalizana na ujenzi wa ukuta nikamrudisha mama nyumbani so kwa sasa wa naishi kwa upendo na Amani ingawa majaribu ya upande wa ndugu wa baba hayana budi kuja lakini Mungu anamuepusha nayo.

Sasa kwanini nimeleta uzi huu ni kuwa ile vita iliyoanzishwa kwa wazazi imenigeukia mimi. Baba wadogo na mashangazi wananiombea maanguko, magonjwa hatarishi na hata kifo jamani!

Moyo wangu unavuja damu, koşa langu liko wapi? Ninastahili maombi mabaya namna hii? Moyo wangu unamajeraha.

Nimeifupisha naomba kuiwasilisha.




Hapo mkuu, hakuna VITA yoyote Ila kilichopo ni hao ndugu zako kuwa negative na wewe kuwa negative


Kuhusu kukuombea mabaya.

Kwanza unabidi kujua hakuna jambo lolote linaweza kukupata baya linalotokana na maombi mabaya.

Nini ufanye.

Hakikisha unakuwa positive usimchuke MTU yeyote , maana unavyowachukia watu maana yake wewe ndo utaishi maisha magumu ,na ukiwaombea mabaya hayo mabaya yatakupata wewe.

Mbinu za kutumia.

Wapende wazazi wako wote na ndugu zako na wasaidie unapoweza , na pia wana ukoo wako ambao unahisi wapo negative tumia kanuni inaitwa "Love from a distance" wapende Ila kaa nao mbali.

Kuhusu kurogwa.!

Kurogwa ni level ndogo Sana kiroho na uchawi hauna nguvu yoyote.

Unafanyaje usirogwe.?

Hakikisha unakuwa innocence , (Unyong'ofu ) usikubali kuwa na kinyongo ,chuki, wivu, n.k

Na mwisho.

Jifunze kufanya Gratitude jambo lolote linalokutokea shukuru ukishukuru unakuwa unaruhusu nguvu chanya au nishati chanya kuyatawala maisha yako.

Zingatia Detachment and Attachment unapoona jambo linakuumiza lisamehe na lishukuru detachment na litaondoka na utakuwa na Amani Sana.

Maombi Prayer /rituals
Unapoomba waombee watu wote kuanzia hao unaohisi hawakupendi waombee Amani na maisha yenye Afya na Mungu awajaze hekima hii itakusaidia Sana.


Elimu, Exposure

Fahamu na. elewa watu wengi hasa watu weusi hawajawa civilized hivyo habari mbaya zako ndo habari nzuri kwao na hii sio kwako ni nchi nzima Hi yo unapofanya mambo mazuri jitahidi MTU asijue ikiwemo wazazi wako.


All the best.
 
Sijakwazika mkuu isipokuwa niliona unavyoandika ni kama tunaishi wote kila siku so ukawa unajua fika Napenda kurushiana maneno.

naona ulikuwa umeng’anga’ana na tuhuma tu mkuu

Nashukuru kwa ushauri pia
Leo jumatatu kuna Mwanasaikolojia TBC Taifa ana kipindi kuanzia saa 4 na robo usiku mpaka saa 6 msikilize utapata namna ya kudili na hii situation yako
 
Hapo mkuu, hakuna VITA yoyote Ila kilichopo ni hao ndugu zako kuwa negative na wewe kuwa negative


Kuhusu kukuombea mabaya.

Kwanza unabidi kujua hakuna jambo lolote linaweza kukupata baya linalotokana na maombi mabaya.

Nini ufanye.

Hakikisha unakuwa positive usimchuke MTU yeyote , maana unavyowachukia watu maana yake wewe ndo utaishi maisha magumu ,na ukiwaombea mabaya hayo mabaya yatakupata wewe.

Mbinu za kutumia.

Wapende wazazi wako wote na ndugu zako na wasaidie unapoweza , na pia wana ukoo wako ambao unahisi wapo negative tumia kanuni inaitwa "Love from a distance" wapende Ila kaa nao mbali.

Kuhusu kurogwa.!

Kurogwa ni level ndogo Sana kiroho na uchawi hauna nguvu yoyote.

Unafanyaje usirogwe.?

Hakikisha unakuwa innocence , (Unyong'ofu ) usikubali kuwa na kinyongo ,chuki, wivu, n.k

Na mwisho.

Jifunze kufanya Gratitude jambo lolote linalokutokea shukuru ukishukuru unakuwa unaruhusu nguvu chanya au nishati chanya kuyatawala maisha yako.

Zingatia Detachment and Attachment unapoona jambo linakuumiza lisamehe na lishukuru detachment na litaondoka na utakuwa na Amani Sana.

Maombi Prayer /rituals
Unapoomba waombee watu wote kuanzia hao unaohisi hawakupendi waombee Amani na maisha yenye Afya na Mungu awajaze hekima hii itakusaidia Sana.


Elimu, Exposure

Fahamu na. elewa watu wengi hasa watu weusi hawajawa civilized hivyo habari mbaya zako ndo habari nzuri kwao na hii sio kwako ni nchi nzima Hi yo unapofanya mambo mazuri jitahidi MTU asijue ikiwemo wazazi wako.


All the best.
Mkuu nilikuwa ninasubiria comment yako sana.

Ninakushukuru mno.
Nitafanya kilichosahihi.ubarikiwe🫶🫶🫶
 
Back
Top Bottom