NECTA yaacha Utaratibu wa Kutangaza Wanafunzi bora na Shule bora kwa Kidato cha 4

NECTA yaacha Utaratibu wa Kutangaza Wanafunzi bora na Shule bora kwa Kidato cha 4

Na ndiko tunakoelekea. Mpango wa MEWAKA (Mafunzo Endelevu kwa Walimu Kazini) utawaimarisha walimu katika eneo hili la lugha na ufundishaji.

Shule binafsi zijiandae miaka kumi ijayo wanaweza kukosa wanafunzi kama ilivyo katika vyuo vya ualimu vya binafsi. Iwapo lugha itakuwa ya Kiingereza Msingi, idadi ya wazazi watakaopeleka watoto wao huko itapungua.
Leo wazazi wengi waliosomesha watoto elimu ya msingi English Medium wanatafuta nafasi katika shule za boarding za serikali kwa sababu wanaamini mtoto akimasta lugha hiyo, ufaulu sekondari ni hakika.
Hebu tuhabarishe zaidi kuhusu hiyo MEWAKA mkuu.
 
Kisa wameona nmepiga one ya 7 ningeweza kuwa hata top ten niwanyooshe watu ndo wamefuta watu wapuuzi sn
 
Afadhali maana shule hii ingeingia top ten za mwisho 😂, headmaster atakuwa amefurahi sana
IMG-20230129-WA0017.jpg
 
Binafsi bado sijashawishiwa na hizo sababu za kusitisha huo utaratibu, nilitamani wauboreshe badala ya kusitisha.

Kwanini, nasema hivyo. Sababu zangu ni hizi hapa.

1. Utaratibu ule uliongeza ushindani na kuchochea uwajibikaji miongoni mwa wamiliki, walimu na wanafunzi.

2. Ulichochea ubora katika utoaji wa elimu.

3. Uliwapa wahusika (serikali, taasisi binafsi, wazazi na wanafunzi) tathmini ya haraka na uhakika kujua walipotokea, walipo na wanapoelekea kielimu kulinganisha na wengine waliofanikiwa au kuanguka.

Kiujumla ule utaratibu ulikuwa unaleta Vibe ya kipekee katika masuala ya elimu.

Imagine zamani ukitamani baadhi ya shule unajua kabisa lazma usome sana ili uzipate

Na shule au mkoa ukiwa wa mwisho, wahusika huwa wanaongeza nguvu ili waepuke hiyo aibu

Tukitoa hii kitu lazma kuwe na kitu kingine cha kuwapa waalimu na wanafunzi ari ya kufanya vizuri

Na hii inawezekana kuonekana kama itaathiri shule za private tu lakini kuna za serikali kama kibaha, mzumbe, ilboru etc ambazo zitaondolewa ule msisimko wake pia
 
Baraza la mitihani NECTA limesitisha utaratibu wa kutangaza shule bora na mwanafunzi bora wa matokeo ya kidato cha nne

Kaimu katibu Mtendaji wa Baraza la mitihani Tanzania NECTA Athumani Salumu Amasi amesema utaratibu huo wa kutangaza shule bora ulikuwa unazitangazia biashara baadhi ya shule

"Unamtaja mtu kwamba ameongoza katika kundi ambalo pamoja na kwamba wamefanya mtihani huo huo lakini hawakusoma katika mazingira yanayofanana, alafu sasa unampa sifa mtu mmoja"

Kuhusu kumtangaza mwanafunzi bora wa mtihani huo amesema hakuna tija katika hilo kwani hauwezi kumtangaza mwanafunzi mmoja katika ya wanafunzi wote Tanzania ambao huenda pia mazingira yao ya kusoma yalikuwa tofauti


Chanzo: EA Radio
Safi
 
Baraza la mitihani NECTA limesitisha utaratibu wa kutangaza shule bora na mwanafunzi bora wa matokeo ya kidato cha nne

Kaimu katibu Mtendaji wa Baraza la mitihani Tanzania NECTA Athumani Salumu Amasi amesema utaratibu huo wa kutangaza shule bora ulikuwa unazitangazia biashara baadhi ya shule

"Unamtaja mtu kwamba ameongoza katika kundi ambalo pamoja na kwamba wamefanya mtihani huo huo lakini hawakusoma katika mazingira yanayofanana, alafu sasa unampa sifa mtu mmoja"

Kuhusu kumtangaza mwanafunzi bora wa mtihani huo amesema hakuna tija katika hilo kwani hauwezi kumtangaza mwanafunzi mmoja katika ya wanafunzi wote Tanzania ambao huenda pia mazingira yao ya kusoma yalikuwa tofauti


Chanzo: EA Radio
Haya ni matokeo ya kuwa na viongozi wenye elimu ya kuungaunga. Shule nyingi zilizokuwa zikishika mkia zina uhusiano na walio madarakani hivyo wamefanya hivyo kwa lengo la ubaguzi hasa udini
 
Kaingia Shekhe pale NECTA kaletewa Mkeka wa TO kaona ni majina ya VATICAN tupu ikabidi apige chini huo utaratibu. Shule zooote za Mwisho ni shule za Dini yake ataanzia wapi kuzitangaza ni ovyo.
Hio utaratibu ulileta hamasa ya watoto kusoma kwa bidii ili watambulike kama TO sidhan kama kulikua na ubaya wowote basi hatuna maono na vitu vya msingi
 
upumbavu tu
kama unatambua watu wanatoka mazingira tofauti kwa nn uweke mtihani mmoja kwa wote

kama vp kila shule ipewe mtihani wake, unatoa mtihani alafu utaki sema ufaulu ukoje
ukweli utabaki shule za serikali ni tia maji tia maji
 
Kaingia Shekhe pale NECTA kaletewa Mkeka wa TO kaona ni majina ya VATICAN tupu ikabidi apige chini huo utaratibu. Shule zooote za Mwisho ni shule za Dini yake ataanzia wapi kuzitangaza ni ovyo.
Hio utaratibu ulileta hamasa ya watoto kusoma kwa bidii ili watambulike kama TO sidhan kama kulikua na ubaya wowote basi hatuna maono na vitu vya msingi
Hahahah ule utaratibu haukuwa Sahihi bhana, watu wanahangaika kupata mitihani ili wapate ufaulu wa juu na kukuza biashara.
 
upumbavu tu
kama unatambua watu wanatoka mazingira tofauti kwa nn uweke mtihani mmoja kwa wote

kama vp kila shule ipewe mtihani wake, unatoa mtihani alafu utaki sema ufaulu ukoje
ukweli utabaki shule za serikali ni tia maji tia maji
Exactly..

Unawapima kwa mtihani sawa then unaogopa kutangaza ranking kisa wanatokea mazingira tofauti..kwanini waweke mtihani mmoja kwa wote sasa?
 
Back
Top Bottom