Mkuu Nehemia alikuwa na backup ya JK hila alianzishiwa mziki na Tibaijuka kuhusu kuongeza kodi.
Alikuwa akikutana na mziki huo anazindua mradi anamualika JK anamuonyesha migorofa aliyojenga. JK anasifia Dar imependeza asikii wala aambiwi kwa huyo mtu.
Sasa kama wewe waziri utafanya nini wakati boss anasifia?
Likaja sakata la escrow likaindoka na Tibaijuka, ardhi akaingia Lukuvi kitu cha kwanza alipiga stop rent hike na kukagua miradi yao.
Jamaa wazushi hao wakaleta hadithi za miradi yao ya Anna na Sifu kuuza nyumba zote, sijui wameingia mkataba na mabenki gani kuuza mortage za 18% plus. Na watu humu kumsifia jamaa ana miakili wakati common sense says ni hadithi tupu.
Kwa ufupi you understand how the government used to work kipindi cha Magufuli. Ila mawaziri walijaribu hasa Tibaijuka na hata Lukuvi.
Alipoingia Magufuli kwakuwa yeye ni mtu wa kufuatilia baada ya kuona hayo madeni yenyewe serikali ndio inalipa sasa ana faida gani ndio maana akamtimua bila ya kujali miradi iliyo njiani.
Huko ATCL upuuzi unaondelea ndio usiseme kama ilivyo kwa JK na NHC, ATCL na Magufuli ndio ovyo kweli kweli.