Nguvu nilizowekeza kwenye ujana wangu nakula Matunda yake sasa

Nguvu nilizowekeza kwenye ujana wangu nakula Matunda yake sasa

Salaam kwenu wote,

Mimi ni mgeni humu ila ningependa kushare kisa kidogo cha maisha ya ujana wangu. Nimezaliwa 1953.

Kusema kweli mwenyezi Mungu alinijalia sana mimi, kwenye elimu ya darasani nilikuwa vizuri sana nikafanikiwa kumaliza chuo mwaka X kipindi hicho. Bahati nzuri nikapata kazi yangu kwenye kampuni Y, nilifanya kwa miaka 3 kabla ya kuhamishwa kupelekwa kwenye kituo kingine. ambapo nilipata mshahara na marupu marupu matamu kweli. Nilitumikia hiyo nafasi kwa miaka 35.

Mpaka nilivyostaafu rasmi 2016, namshukuru Mungu sana kwa kunijaalia akili ya kuona mbele, na kuweza kupanga hatma ya maisha yangu.

Niliweza kujiingiza kwenye kuwekeza kwenye vitega uchumi mbalimbali ambavyo ndo vinanilea sasa hivi.

Nawashauri vijana mtakaosoma hiki kisa tafadhali tafadhali tumieni muda wenu vizuri, msije mkajuta baadae mkiona mzee ni masikini jua haikuja hivi hivi, likewise mkiona mzee ni tajiri jua ni tu watu walijitoa haswa haswa,

Zingatia: Tumieni ujana wenu vizuri, narudia tena tumieni ujana wenu
Vizuri, narudia tumieni ujana wenu vizuri. Msije Mkajuta kwenye uzee wenu, maana muda utakuwa umekutupa mkono na ndipo maradhi yatakavyoanza kukushambulia.

Kwangu mimi navyoona umri wa kuweka nguvu ni (25-55) hapa ndo inabidi ufanye uwekezaji mkubwa na uchakarike sana.

Lakini kumbukeni pia kumtanguliza Mungu kwenye kila mfanyacho ili azidi kuwabariki. Mimi namshukuru Mungu wanangu 4 wapo vizuri kila mtu yupo kwao na famili zao. Mimi nalea wajukuu tu wakija likizo. Hivyo ni faraja sana kwangu.

Namshukuru Mungu kwa kunijaalia uzee mzuri, japo haikuwa rahisi mpaka kufikia hapa nilipo.

Muwe na Jumapili njema [emoji114][emoji114][emoji114][emoji114][emoji114]
Umezaliwa 1953 na umestaafu 2016, kwa hiyo ulidanganya umri wa kuzaliwa maana ulitakiwa ustaafu 2013 (miaka 60 ).
 
Watu wanauliza maswali mengi ili,kumfanya mtoa mada aonekane muongo,chukueni hiyo point itatusaidia badae ni ukweli usio pingika
Uko sahihi, watu wanachambua sana, kumbe lengo la mtoa mada ni kutukumbusha yatupassyo kufanya kabla ya uzee.

Watu wanahoji mpaka umri, ina maana wameshindwa kuona hekima iliyo katika andiko, wanatafuta kasoro pekee. Kupanga nj kuchagua.
 
Maisha ni bahati tu ndugu

Kwa umri wako naamini umeona na kukutana na watu hawa:

01).watu wenye elimu kuliko wewe
02).watu wenye juhudi kuliko wewe
03).watu wenye imani kuliko wewe
04).watu makini na wenye mipango mizuri kuliko wewe

lakini wote hao wewe umewazidi mafanikio ..unafikiri ni kwanini?

Wewe una bahati kuliko wao.

Juhudi na mipango mizuri ina nafasi lakini kwa kiasi kidogo tu

Watu wanafanya each and every thing kwa usahihi lakini mafanikio tu ndio hakuna

Kwa kuwa hatujui ikiwa tuna bahati au la basi tuendelee kujituma na kuamini kama ulivoshauri.
 
Vijana vya sasa hivi vya ajabu sana.
Eti hiki nacho kinajiona kizee.
Aya babu tutafata ushahuri wako.
Ila maisha ya sasa hivi sio kama ya zamani.sasa unatakiwa kushikilia bomba haswa.

Hata hizo kazi unazosema umepata sasa hivi hazipatikani .
Kupata kazi sasa hivi imekuwa kazi mzee
 
Salaam kwenu wote,

Mimi ni mgeni humu ila ningependa kushare kisa kidogo cha maisha ya ujana wangu. Nimezaliwa 1953.

Kusema kweli mwenyezi Mungu alinijalia sana mimi, kwenye elimu ya darasani nilikuwa vizuri sana nikafanikiwa kumaliza chuo mwaka X kipindi hicho. Bahati nzuri nikapata kazi yangu kwenye kampuni Y, nilifanya kwa miaka 3 kabla ya kuhamishwa kupelekwa kwenye kituo kingine. ambapo nilipata mshahara na marupu marupu matamu kweli. Nilitumikia hiyo nafasi kwa miaka 35.

Mpaka nilivyostaafu rasmi 2016, namshukuru Mungu sana kwa kunijaalia akili ya kuona mbele, na kuweza kupanga hatma ya maisha yangu.

Niliweza kujiingiza kwenye kuwekeza kwenye vitega uchumi mbalimbali ambavyo ndo vinanilea sasa hivi.

Nawashauri vijana mtakaosoma hiki kisa tafadhali tafadhali tumieni muda wenu vizuri, msije mkajuta baadae mkiona mzee ni masikini jua haikuja hivi hivi, likewise mkiona mzee ni tajiri jua ni tu watu walijitoa haswa haswa,

Zingatia: Tumieni ujana wenu vizuri, narudia tena tumieni ujana wenu
Vizuri, narudia tumieni ujana wenu vizuri. Msije Mkajuta kwenye uzee wenu, maana muda utakuwa umekutupa mkono na ndipo maradhi yatakavyoanza kukushambulia.

Kwangu mimi navyoona umri wa kuweka nguvu ni (25-55) hapa ndo inabidi ufanye uwekezaji mkubwa na uchakarike sana.

Lakini kumbukeni pia kumtanguliza Mungu kwenye kila mfanyacho ili azidi kuwabariki. Mimi namshukuru Mungu wanangu 4 wapo vizuri kila mtu yupo kwao na famili zao. Mimi nalea wajukuu tu wakija likizo. Hivyo ni faraja sana kwangu.

Namshukuru Mungu kwa kunijaalia uzee mzuri, japo haikuwa rahisi mpaka kufikia hapa nilipo.

Muwe na Jumapili njema 👐👐👐👐👐
Be blessed father,nazingatia hilo
 
Mzee ungeelekeza vizuri namna ulivyoanza kuwekeza na sehemu ulizowekeza uzi wako ungekuwa na manufaa sana Kwa wasomaji, ila Kwa style hii uliyokuja nayo uzi wako umejaa majigambo na mipasho.

Uwe na j.pili njema nawe pia
Watu wana hasira na hii life[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Uko sahihi, watu wanachambua sana, kumbe lengo la mtoa mada ni kutukumbusha yatupassyo kufanya kabla ya uzee.

Watu wanahoji mpaka umri, ina maana wameshindwa kuona hekima iliyo katika andiko, wanatafuta kasoro pekee. Kupanga nj kuchagua.
Kama alidanganya umri maana yake hata andiko lake inaweza kuwa chai ya rangi tu
 
Nilikuwa nakula (30-40)% inayobakia na investvau na save basi hamna kipya

Sikuwa mtu wa anasa kabisa
Eeh sasa imagine ulipwe zaidi ya million 1 kwa mwezi kwa miaka 35. Hata uwe mtu wa bia kila siku lazma utastaafu na hela tu.

Sisi hata hizo fursa za kazi hatuna sikuhizi. Unajikuta unaenda kufanya kitu ambacho kila mtu anafanya sababu ya easy entry.
 
Wala hilo andiko hajafafanua vizuri. Alitakiwa atueleweshe amewekeza nini.
Mkuu, hapa jf ukitaka kila mtu atoe uhalisia wa maisha yake hutampata hata mmoja. Wewe angalia alichoandika, chukua kile kinachokusaidia kifanyie kazi kwa njia zako.

Hata kama atakueleza njia alizopita katika kuwekeza haita kuwa na maana kwako kwa vile kila mmoja ana njia zake za kufanikiwa.
 
Eeh sasa imagine ulipwe zaidi ya million 1 kwa mwezi kwa miaka 35. Hata uwe mtu wa bia kila siku lazma utastaafu na hela tu.

Sisi hata hizo fursa za kazi hatuna sikuhizi. Unajikuta unaenda kufanya kitu ambacho kila mtu anafanya sababu ya easy entry.
Kwenye 1m *35 yrs kuna ukakasi😅
Ila cha msingi nimeona ni kujitahidi ku invest tukiwa vijana na nguvu kubwa, ili uzeeni tupate ahueni.
 
Kweli kabisa.na kwa kipindi icho kaz ni uhakika sio kama saiv mtu anasoma na kupata kazi ni kazi.
Sahizi kusoma ni jambo moja na kufanikiwa ni jambo jingine 😀! Zamani ilikuwa rahisi tu unamaliza chuo ushapangiwa kazi wewe ni kula mshahara tu. Unajipangia aina ya maisha unayotaka.

Sahizi maisha ndio yanakupangia uishi yanavyotaka. Yakiamua uteseke unateseka balaa na hamna kitu utafanya. 🤣
 
Back
Top Bottom