Ni biashara ipi ndogo sana uliifanya ikakufikisha kwenye mafanikio makubwa?

Ni biashara ipi ndogo sana uliifanya ikakufikisha kwenye mafanikio makubwa?

Hii inalipa mkuu Mimi KWA mwez tu Napata faida sio chini ya million 1 . Kitu cha kuzingatia uwe na mtaji na hakikisha wateja hawaondoki na machenji ili wachina wakija kufungua wakutee mifuko Mingi . Mfano Mimi jana tu jumamos wamefunga mifuko 5 (Sawa na 45000) na hii ni makusanyo ya siku 2 tu haya jana nimeingiza mifuko 4 leo nimewambia wafungue 36000 . Kwahiyo jana na leo tu faida nimeingiza 81000.

Tahadhari ili ufaidi hii biashara hakikisha wewe au msimamizi wako hachez kabisa kamari akicheza tu ndugu yangu umeumia


Na hapa ni KWA kuwa mzunguko umekuwa mdogo zaman nilikuwa naweza kuuza hata mifuko zaidi ya 10 KWA siku
Uko sahihi kabisa.

Location matters
 
WALIOFANYA YA PHOTOGRAPHY NA PHOTOSHOOT NAOMBA MUONGOZO JAMAN WAKUU
enzi zangu kwenye 2010 nilimuwa na camera yangu nikon nilinunua around 1.8m kwa jamaa yngu toka south
kazi yangu kubwa ilikuwa ikifika jioni natafuta kumbi za harusi iwe diamond jubilee au kokote kule nampa mlinzi 10k yake

naingia napiga watu picha na picha moja nlikuwa nauza kuanzia elf 3 mpka 5 kutokana na size nilikua na mashine ya kusafishia hapo hapo nikitoka hapo naweza kuondoka na hata laki kama faida sjui sku hizi wnafanyaje japo kuna sku unaweza kupta ndogo au kukosa kazi kabisa kama wenye shughul wakiwa wakuda
 
Biashara ya dawa ina faida kubwa sana! Faida yake huwa ni mara 2 au zaidi yani ukiuziwa dawa yoyote mfano labda 1000 ujue aliyekuuzia kapata faida ya 1000 na kuendelea! Mfano zile baby test kwa jumla zinauwa 100/= ila ukiend duka la dawa unauziwa 1000!! Ila changamoto ya hii biashara mjini haina mzunguko! Vijijini inalipa sanaaa!
 
enzi zangu kwenye 2010 nilimuwa na camera yangu nikon nilinunua around 1.8m kwa jamaa yngu toka south
kazi yangu kubwa ilikuwa ikifika jioni natafuta kumbi za harusi iwe diamond jubilee au kokote kule nampa mlinzi 10k yake

naingia napiga watu picha na picha moja nlikuwa nauza kuanzia elf 3 mpka 5 kutokana na size nilikua na mashine ya kusafishia hapo hapo nikitoka hapo naweza kuondoka na hata laki kama faida sjui sku hizi wnafanyaje japo kuna sku unaweza kupta ndogo au kukosa kazi kabisa kama wenye shughul wakiwa wakuda

Ubarikiwe brother kwa ku share nasi
 
Premier bet buku saba unapata ukiuza laki moja.....sasa ivi raia hawana ela mie nilikua nauza laki nne per day mpaka tano wikiend sasa ndio balaa nagonga laki nane mpaka 1M.......nilikua na mashine mbili moja ya vibosile kuanzia mkeka wa buku kumi na kuendelea hawa walikua balaa mtu anakuja na laki tatu anatoa mkeka mmoja tu mashine nyingine ya hawa wenzangu na mie mikeka ya jero buku mpaka buku tisa.....

Nilikua nafunga kijiji balaa pale mtaani nikikosekana masaa tu natafutwa kwenye simu na wafanya biashara wa lile eneo huwa wananiambia nasie tunauza vinywaji na vyakula sana kupitia wewe mimi mwenyewe sikuwahi kuwaza kabisa kama kuwa kwangu pale ni faida kwa wengine......

Nilisoma chuo miaka mitatu kupitia ile biashara nilimaliza 2015 kizaazaa alipoingia huyu bwana wateja wakaanza kupungua mdogo mdogo mwishowe hakuna kabisa umeuza sana laki tena wikiendi kufika 2017 mwishoni nikafunga rasmi biashara........
Mkuu naona sasa premier betting wana mawakala wana fremu vilivyopakwa rangi na kubrandiwa na vi machine fulani vya ku touch vya kubeti.. taratibu zikoje kwa wakala wa namna ile?
 
Nilianza biashara ya kukopesha pesa. Nilikuwa na milion moja na nusu mwaka 2018 leo nina mtaji wa milioni 35. Kuna maelezo marefu kidogo ni jinsi gani nilifanikiwa hapa. Nikipata muda naweza kuelezea.

Pia mwaka 2014 nilifungua library ya movie nilikuwa na laptop moja tuu yenye hdd ya gb 160. Leo nina desktop tano na jumla ya terabyte 48. Studio inalaza 300,000/= kwa wiki. Mfanyakazi anajilipa mwenyewe, analipa kodi, umeme na kununua movie.

Haya mafanikio ni matamu sana kuyasoma na kufurahi ila haikuwa rahisi kabisa. Natamani nielezee kwaundani. Ila niseme jambo moja.. Biashara yoyote ile ilimradi iwe halali ukiifanya kwa moyo na kujituma utafanikiwa sana sana...

Haya mawazo yasiwachanganye watu. mtu afanye anachoweza kwa moyo mmoja atafanikiwa tuu piga ua.
 
Nilianza biashara ya kukopesha pesa. Nilikuwa na milion moja na nusu mwaka 2018 leo nina mtaji wa milioni 35. Kuna maelezo marefu kidogo ni jinsi gani nilifanikiwa hapa. Nikipata muda naweza kuelezea.
Pia mwaka 2014 nilifungua library ya movie nilikuwa na laptop moja tuu yenye hdd ya gb 160. Leo nina desktop tano na jumla ya terabyte 48. Studio inalaza 300,000/= kwa wiki. Mfanyakazi anajilipa mwenyewe, analipa kodi, umeme na kununua movie.
Haya mafanikio ni matamu sana kuyasoma na kufurahi ila haikuwa rahisi kabisa. Natamani nielezee kwaundani. Ila niseme jambo moja.. Biashara yoyote ile ilimradi iwe halali ukiifanya kwa moyo na kujituma utafanikiwa sana sana...
Haya mawazo yasiwachanganye watu. mtu afanye anachoweza kwa moyo mmoja atafanikiwa tuu piga ua.
Mkuu ichanganue hii ya movie library
 
Mimi nafanya ya chips, sijaanza muda mrefu, nimemuweka wife asimamie kama biashara yake, kwa siki analaza sio chini ya 20, weekend kama jumapili analaza hata 60
Anahongwa na mabwana huyo, shituka Mkuu. Kuna mtu alileta uzi humu USHUHUDA wa jinsi anavyowala wake za watu kwa hongo ya 200,000 na 250,000. Fuatilia huko kwenye chipsi zenu.
 
Mkuu naona sasa premier betting wana mawakala wana fremu vilivyopakwa rangi na kubrandiwa na vi machine fulani vya ku touch vya kubeti.. taratibu zikoje kwa wakala wa namna ile?
Nimetoka huko muda sana miaka zaidi ya minne sina lolote ninalolifahamu....
 
Hii inalipa mkuu Mimi KWA mwez tu Napata faida sio chini ya million 1 . Kitu cha kuzingatia uwe na mtaji na hakikisha wateja hawaondoki na machenji ili wachina wakija kufungua wakutee mifuko Mingi . Mfano Mimi jana tu jumamos wamefunga mifuko 5 (Sawa na 45000) na hii ni makusanyo ya siku 2 tu haya jana nimeingiza mifuko 4 leo nimewambia wafungue 36000 . Kwahiyo jana na leo tu faida nimeingiza 81000.

Tahadhari ili ufaidi hii biashara hakikisha wewe au msimamizi wako hachez kabisa kamari akicheza tu ndugu yangu umeumia


Na hapa ni KWA kuwa mzunguko umekuwa mdogo zaman nilikuwa naweza kuuza hata mifuko zaidi ya 10 KWA siku
Kulipata hilo dubu ni bei gani?
 
Back
Top Bottom