Kuna level ya dhiki ukipitia huwezi furahia madhila ya mwenzio haijalishi alikukosea kiasi gani.ikawa umefurahi ehh ?
Waswahili wanasema Karma is a Bitch.Hii comment yako imenikumbusha mbali sana.
Kipindi cha mapito magumu nilikutana na ndugu kabisa wa mzee wangu. Nikamwambia hali halisi ya maisha.
Yule mzee alinijibu unakosaje hata mlo mmoja, huoni unajaza dunia tu si bora ungekufa na baba yako tu.
Hii kauli iliniliza kama mtoto mdogo.
Ila Mungu si wa mmoja, hivi karibuni tu kulipitishwa mchango wa kifamilia, mzee kashikwa na tezi dume analia kama mtoto. Watoto wake hakuna hata mmoja mwenye muelekeo.
Nilistopisha ule mchango na nikasimamia operation yake mpaka kutoka kwake hospitali.
Yule mzee anajifanya kasahau kila kitu ila najua nafsi yake inamsuta kila akiniona.
Ameandika habari za Kusikitisha ila Nilipoona Picha la Mwigulu nikakumbuka Bajeti nikaghafirika. [emoji3][emoji3][emoji3]Wewe ni Mh.Mwigulu?
Mara nyingi katika maisha ni nadra sana kwa mtenda kukumbuka mabaya yake.Mzee ameoneshwa na kufunzwa jambo kubwa sana kupitia wewe. Ingawa unasema amejizima data kujifanya hakumbuki ila Moyoni anajuta haswa.
oyaaaNilikuwa naishi na bibi yangu, kwakuwa hatukuwa na chakula ndani ikabidi aniache pekeyangu aende kwa baba zangu wadogo kuomba pesa ya matumizi.
Safari yake ilikuwa ya sikumbili kama sijakosea. Aisee nilishikwa na njaa nikachemsha yale mamchicha mekundu nikala badae nikaenda kwa jirani nikakuta wanatoa vichwa kwenye samaki wadogo kanda ya ziwa tunawaita Furu.
Ikabidi niwaombe vile vichwa, nakumbuka nilidanganya naenda kumpa bata wangu. Nilichemsha vile vichwa nikala nikanywa na supu anagalau nikawa vizuri.
daahMaisha ni safari ndefu sana nikikumbuka ya nyuma namwambia tu Mungu Asante umejua kunifurahisha[emoji120]nishawahi kuzimia na njaa mara mbili
Dah 😕😕Mke wangu kushindia mua tu tena akiwa mjamzito. Mungu atusaidie kwa kweli.
Hakika.Mara nyingi katika maisha ni nadra sana kwa mtenda kukumbuka mabaya yake.
Nilichofanya kwake sio kwa kumdhihaki bali kwa kuwa najua nini maana ya kukosa pale unapohitaji.
Mwenye asili yake haachi, haitokuwa ajabu kesho akiwa na uwezo akaacha kumsaidia mwenye shida na ndio maana tukaambiwa fanya wema uende zako.
Inatakiwa uweke x number zote zisizo pokea simu ukiwa masikini ili siku ukipata tu nawe upokeiSiku Ukipata kaunafuu, wanaanza kukupigia eti "nilikuwa nakusalimia tu"😅 wtf
Mwamba umetisha nimecheka kinoma kushindia mua duuuu????!!!!Mke wangu kushindia mua tu tena akiwa mjamzito. Mungu atusaidie kwa kweli.