Ni changamoto zipi umewahi kupitia ukiwa katika hali ya umasikini?

Nimekuwa katika mazingira ya shida na tabu mnooooo aiseee, maisha ya kuuza sambusa ili ule, maisha ya kuuza karanga ili ndo ule, maisha kwenda kufanya kazi Bakery ili upate mikate iliyoungua ndo ukale nyumbani na wazazi aiseeee

Maisha yale yakushindia maembe asubuh mchana, usiku, maisha ya Kula wali bila mboga maisha ya kulalia mabati unaweka nguo nguo juu ndo godoro lako wazeee umasikini nimeuishi saaaaana jamani aiseeee namshukuru mungu sana kwa kidog hiki anachonipa sasa hivi japo njaa siku moja moja nalalanayo bado ila namshukuru sana muumba maana yeye ndo mpangaji wa yote hayo
 
Niliwahi pitia changamoto ya ukata kiasi kwamba niliweza kumaliza siku mbili bila kutia kitu mdomoni,yaani 48hrs bila kula kitu.
Nilikonda sana kiasi kwamba ambaye alikuwa akinifahamu hakuwa na uwezo wa kunitambua tena

Niliishi maisha ya shida sana kiasi kwamba mlo tu kwangu ilikuwa ni kama anasa.Niliweza kuka mlo mmoja tena si ya kwamba hadi nishibe ,ni ile kukazia tu ili njaa isinisumbue.
Wakati mwingine niliamua kufunga na kusali tu,mana chakula nakipata kwa shida mno.Nilikuwa napita kwenye baadhi ya miji ya watu nakuta maembe mabichi kwenye baadhi ya miti iliyo kuwa njiani ,mie najichumia kama mawili hivi na huo ndo unakuwa mlo wangu wa siku nzima .

Nguo zangu zote nilizipunguza mana zilikuwa hazinitoshi tena.
Jambo moja nililoweza kugundua ni kwamba ,pale mwanadam anapokuwa na njaa na ndipo uhalisia wake unapokuwepo.Ukiwa na njaa hauwezi kuogopa kitu,huwezi kuwaza ujinga hata kidogo,fikra zinaimarika na utawaza vitu positive sana

Mungu ni mwema bado pumzi ipo na anatubariki kila kuitwa leo,kwa mwanadamu mapito ni lazima.
 
Ni mipango tu imekosewa na kizazi chake kilichotangulia, kitu chochote kikikosa msingi mzuri kitabomoka au kuyumba mbele ya safari hata kwa dhoruba kidogo, hao wazee unaosema awapelekee utakuta hawakuwa na uchungu wa kulinda ukoo wao katika swala la uchumi ili mbele ya safari ukoo uwe wenye kubarikiwa Sasa akijipendekeza kupeleka hicho Cha shida anachopata ndo kwanza wanaweza kumtumbikiza shimboni kwa wivu, watu wanaojua maana ya kulinda jina la familia wazee huwa wanahakikisha wanajenga msingi kwaajili ya kizazi Cha mbele na hata jina la familia linalundwa sana hata mwanafamilia akikwama hawezi kuyumba sana kimaisha maana anakuwa na msingi mzuri na wale walioharibika tabia unakuta ukoo unawawajibisha ili walinde kizazi kizuri na jina la ukoo, Sasa huyu anatakiwa arudi Kijijini kupata sapoti ya wazee ili ainuke Tena na siyo kuwapa asichonacho.
 
Ni vingi visa, ila nakumbuka mvua ina nyesha asubuhi had jioni na ndani hakuna chakula, mama alinipa mfuko wa sulphate kisha akasema nenda mwembe fulani ukaangue maembe ulete tulalie..

Nimetembea ndani ya mvua, nimekwea ule mwembe kunanyesha, nimevuna maembe robo kiloba kisha nikarejea nyumbani bado kunanyesha, tukajikusanya pamoja kama vile chakula tayari, kila mmoja anavuta embe anakula likiisha unarejea kwenye mfuko kuchukua lingine


Baada ya hapo mama akasem kunyweni maji mlale..
R.I.P hero Mom
Na hiki ni moja ya visanga/episode katika safar ya ufukara
 
Wanawake wengine wajanja, wakiona Maisha magumu, wanazoea nyumba zenye unafuu ukifika pale unasaidia kazikazi, wakipika chakula unakula na mtoto, kama kunachochote kitu unapewa unaondoka jioni, mi nimewakuta Sana home watu wa dizaini hii.
saleni, hukupata tena dili jingine la pharmacy?
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]daah aiseee...
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Mzee anajikaushaa kama vile hakukutendea ubayaaa...!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…