Ni halali Wazanzibari kufanya kazi za Watanganyika?

Fanya yako unapo jadili ndo unaleta ubaguzi, kama hauna kazi kalime sasa Zanzibar ni kamji kadogo eti ukababane huko huko kwa nn? Wao ndo wanakuja huku kwa wingi . Ubaguzi mbona hapa Bongo mnajifanya mpo makabila machache ndo kila kitu ukienda tu hapo kilimanjaro kupata ardhi ni ishu hamuoni huu ujinga!!!!

Wale Wana mifumo yao waacheni waendelee mnataka kuleta undungu kweny eneo la watu kwa kubebana .watanganyika ni wabaguzi mno hata kama mmi ni mtanganyika ...wenzenu Zanzibar wanalinda tamaduni zao kama wamoja nyie mtakaje? Bora wazanzibar huko ofisini kuliko wachaga na wahaya roho mbaya kabisa nyie
 
Habaguliwi mtu. Haki ni haki haibagui. Tunazungumzia Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na haki zake zilizomo!!
Wewe Ulitakaje Kwani, Hivi Hata Kwenye Sinia Kaka na Mdogo wake hawaendi Matonge Sawa Kuna Muda Anamwachia Ashibeee, Mimi Nikiangalia Sioni Tatizo Apo Maana Tanganyika Tumewazidi Zanzibar Kwa Vingi Hivyo Hatuwezi Kungangania Ardhi Yao kuchenga Uko Kati Tuna Mapori Mengi Huku Bara, Pia Kwenye Upande Wa Ajira Tukisema Tuajiri Sawa waTanzania Ni wengi Na Bado Nafasi Hazitawatosha Ndio Maana Wanajaribu Kubalance Na Wazanzibar... Kifupi Tutafute Khela Hizi Nyuzi Nyengine Ni Njaa Tu
 
I like this guy.......
 
Hoja yako ni dhaifu sana!!
 
Habaguliwi mtu. Haki ni haki haibagui. Tunazungumzia Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na haki zake zilizomo!!
Kote Kuna ubaguzi sasa muungano wa nn? Wakati ndani tu tuna matatizo hata hao wazanzibar kipind cha uchaguzi wanagwanyika .. Tatizo mkikaribishwa kwa watu mnaleta ujuaji mwingi
 
ubgunge ni suala la mungano, huhitaji kuwa na kitambulisho cha mzanzibari mkaazi kugombea, labda baraza la uwakilishi ndio linahitaji kitambulisho cha mzanzibari mkaazi.
Jaribu tu ndugu yangu...
 
Kuna kitu umazungumza hapo alafu mm bado sielewi.

Kuna mawili hapa naomba ufafanuzi;

Je, Ni kuwa nafasi zikitoka za ajira mtu yoyote anaomba awe mzanzibar, awe mtwara au singida.

Je kuna asilimia ya nafasi zinaenda kwa ajili ya wazanzibari tu, mtu mwingine ambae sio mzanzibari hawezi kuomba?
 
Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya MT na sheria ya uraia, Wazanzibari ni Watanzania kwa hivyo wanayo haki kikatiba kufanya kazi popote katika JMT. Ikiwa katiba haifai inapaswa kurekebishwa na hivyo ni jukumu letu sote tunaoona hivyo kupigania mabadiliko ya katiba kwa vitendo na siyo kulalamika tu kwenye keyboard. Amkeni tudai katiba mpya. Wazanzibari watabakia kuwa Watanzania hadi hapo katiba itaposema vingine na itasema vingine pale tutapoipigania kwa vitendo.
 
Inavoonekana hakuna Watanganyika. Kwa nini??
 

Hili bandiko lako limejikita katika kuomba kura za waZanzibar hakuna cha ziada.Huu Muungano umejaa upuuzi mwingi.
 
Miaka mingi mbele Tanganyika tusipokaa kwa akili hawa watatutia vidole mchana mchana, taratibu wanaanza kuota mapembe nakuona tunawahitaji kuliko wanavyotuhitaji.

System isipokuwa makini na wazee kuitana pembeni kuanzisha taratibu za siri kuihami Tanganyika na watanganyika basi kuna hatari ya Watanganyika kwa wingi wao kuwa watumwa aka chuma ulete kwa Wachache wazanzibar.

Wazanzibara wanaamini ni waarabu na through this wengi wanatokomea Oman nakuishi huko na hata kupewa ajira huko na kufanya maisha huko, Oman tusipokuwa makini nao through this wanakuja kuleta bomu kubwa sana pale siku moja huku tukiwa tumeshapata hasara kuuubwa sana pale na tutajikuta tunagharama kuubwa ya kulipa.

Tukae kwa akili sana kujihami na hawa watu, CCM muache kuangalia tu maslahi ya chama na mambo mambo yenu ya siasa, mnajukumu pia kuhakikisha Tanganyika inakuwa salama kisiasa, kiuchumi, kitechnolojia nk kwa kutumia akili nyingi na kubwa sana. With this akili fupi fupi na wawaza siasa muda wote tunakwenda kujizamisha wenyewe.
 
Haki na ubaguzi ni mambo mawili tofauti, ni kama dini na udini!!
Hamkawii kuwaita wavivu basi waache wafanye kazi zao na huku pia waje kufanya izo kazi!! Mtu ukienda kule siku mbili tatu unakuja na Uzi watu wa kule wavivu basi waache wafanye kazi zao.
 
Mzanzibar akikohoa tu, Tanganyika linatetemeka.

Wazanzibar nafasi zote za serikali ya mapinduzi ya Zanzibar zao peke yao

Nafasi zote za Ajira kwenye mambo ya muungano wana uhakika wa kupata 25% , na bado hawazuiwi pia kupata pia hata katika zile 75% zilizobaki

Kwenye mambo yasiyo ya muungano yale ya Tanganyika, Wazanzibari bado wana haki ya kupata ajira kwa sababu kigezo ni awe MTANZANIA mwenye sifa.

Ardhi la Tanganyika lote wana haki nalo, ila ardhi ya Zanzibar ni yao peke yao!.

Wazanzibar wamefanikiwa kuondoa suala la mafuta kwenye muungano, wanataka wakiyagundua yawe yao peke yao. Ila Yakigundulika Tanganyika basi mafuta hayo yanakua ni ya TANZANIA, yaani yetu sote!

Hivi kiukweli haki bin haki, Mtanganyika ananufaika na nini kwenye huu muungano?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…