Ni kituko kuingia mkataba wa USD billion 42 za mkopo kwa ajili ya mradi mmoja tu wa kutengeneza natural gas refinery

Ni kituko kuingia mkataba wa USD billion 42 za mkopo kwa ajili ya mradi mmoja tu wa kutengeneza natural gas refinery

Tanzania bado haija-sini mkataba wa kujenga natural gas refinery ila uko mezani mpaka sahivi

Mwanasheria wa serikali alitaka mazungumzo zaidi juu ya mkataba kwa sababu kuna mambo bado kama serikali hajaridhika nayo

Wito ni huu tunaomba serikali isi-sini huo mkataba iangalie option nyingine billion 42 ni nyingi sana kwa mradi mmoja tu na kwa nchi maskini kama Tanzania

Mfano usd billion 42 unaweza tengeneza miradi ifuatayo na itakua na faida kubwa sana
  • Aluminium smelter
  • Copper smelter
  • Pig iron smelter
  • Glass smelter
  • Spinning
  • Paper pulp
  • Oil refinery
  • Petrochemical plant
Kweli.
Ila BI CHURA KIZIWI na Mwigulu wake watakusikiliza?!
 
Bosi unajua hata hesabu za kutoa na kujumlisha?

Kama toka Tupate Uhuru haijafika Dola Bilioni 42 miaka 5 iliopita ndio itafika?

Mwaka 2019 Deni la Taifa ni $24B sasa hivi Roughly $34B ongezeko kama la $10B miaka 5, far from $42B figure.

Hatuna hio hela na wala Hatukopesheki hio figure hata tukitaka,
Nadhani pengine hujaelewa nini namaanisha. Tunaweza kukopa hiyo sababu ya kukopa kufanyia mradi mkubwa kama huo. Lakini hatuwezi kukopa pesa kubwa hiyo kuja kujenga mwendokasi au daraja.

Pia nimekueleza mkopo sio wa mwaka mmoja, sio kwamba pesa yote unapewa mwaka huo huo. Btw kuna madhara makubwa kuchukua mkopo wa aina hiyo lakini haimaanishi hatuwezi kukopesheka
 
Wakati wa Mwinyi kulikuwa IPTL, wa Mkapa kulikuwa na Bulyankuru, North Mara, na Mkwere kulikuwa na Songas. Wakati wa Negotiation kipindi hicho wananchi walipewa moyo kuwa neema inakuja.

Matokeo:

Songas: wananchi walilipa tozo kubwa ya umeme kuliko bei ya soko, serikali ikapoteza umiliki wa share na kodi, tozo na gawio vikawa nehi.
Madini: Serikali ilipewa share chini ya 2%; msamaha wa kodi wa kudumu wakapewa wawekezaji na mwisho ikatupeleka kwenye makinikia crisis.

Facts kuhusu LNG: Ni kweli initial investment cost yake ni yakutisha. Mathalan, Serikali inahitaji sio chini ya TZS trilioni 75 ili kuwekeza katika LNG. Serikali haina huo uwezo. Matokeo yake Investors wanaongeza gharama za uwekezaji hadi kufikia zaidi ya TZS trilioni 100 ili kuweka mazingira ya fursa ya kuipunja serikali kwenye share na kodi.

Hakika nawaambia, Nivigumu kwa serikali kupata deal fair katika uwekezaji wa LNG kuliko Ngamia kupenya kwenye tundu la sindano. Kutokana na mvuto mkubwa wa ufisadi, Katika baadhi ya nchi akitokea mtu anataka deal la gesi au wese linyooke, beneficiaries kutoka pande zote, malaka na mwekezaji umwondoa katika ramani daima.

Kwa kuwa tuna uhaba wa kutisha wa wataalamu (kiuchumi na kiteknolojia - hapa simaanishi wenye vyeti bali wanaoijua hiyo sector vilivyo) na hatuna hata robo ya mtaji, ingekuwa busara tukasubiri hadi tutakapopata wajuzi (watoto wetu). Kizazi cha kwanza, cha pili na cha sasa Afrika kimeshindwa kuivusha Afrika.

Kutokana na human capital kuwa chini Tz, kwa sasa wadanchi hawajui kinachoendea na athari zake, wamelala dolo. Ila hakika nawaambia uvunaji ukianza, hawa waliolala dodo wakiona foleni za mameli makubwa zikitia nanga mtwara na kuondoka na mitungi ya gesi kwa kasi ya kutisha huku Tz ikipata nehi kwenye kodi na shares, wataamka, watahoji na wataliamsha hali itakayopelekea kutokea yale yaliyotokea Niger Delta. Hivyo, tafadhali wakubwa zetu, chukueni taadhali stahili ili deal la LNG liwe baraka na siyo laana kwa taifa. Inasisitizwa LNG siyo mradi wa mchzo mchezo haijawahi tokea nchi yeyote ya kusini mwa jangwa la sahara kuwa na deal nono la aina hiii. tukipata deal fair tutatoboa, tukitanguliza ubinafsi imekula kwetu mazima na kwa watoto/wajukuu wetu.

Note: wanaosema hela anatoa mwekezaji hivyo wananchi na serikali hawana cha kupoteza. hawajatafakari vema, hawaoni mbali, hawakumbuki ya Bulyankuru na hawana upeo sahihi kuhusu mantiki ya fedha za mwekezaji. Fedha za mwekezaji utolewewa kwa sharti la serikali na wananchi kupoteza haki zao za asili hasa share na kodi kwenye mradi husika (ndio maana huwa mikataba ya aina hiyo inafichwa kwani mkiona mtapofuka macho).

Kama Botswana wameweza kwenye Almasi kwa nini sisi tunashindwa?

Mungu awaongoze viongozi wetu mtuvushe salama kwenye LNG.
 
As far as ‘oil and gas’ investment rationale is concerned and overestimation ya huo mradi.

As far as how that debt will be repaid based on the share of barrel; bear in mind price ‘flow and ceiling’ in the contract and minimum debt commitment.

Ukisoma hii mada ni ujinga mtupu; ni hoja za watu kutoa kichwani kwao tu.

Not that we did not warn you, huyo mama hizo hela anazopewa kirahisi ni debt trap, ili huko mbele aje aachie hiyo gas kirahisi.

Ni mataahira tu ndio yanaweza mtukana Magufuli, unadhani rahisi kuwabadili tabia watu wasio jali mustakabali wa nchi wanaojali matumbo.

Huo mkataba kwa sasa utasainiwa tu, ni rahisi sana kuwaona wasaliti not necessary wao wenyewe wanajua kama wanatumika. Shida ni uwezo wao mdogo kutokujua wanacho promote-take it from me Zitto, January, Nehemia na huyo marehemu Mafuru; hizo akili za haya mambo hawana. Na ndio waliowafikisha hapo.
 
Kwani wewe Kalamu unataka hii gesi ya Lindi waifanyie nini? Isichimbwe? Au unataka wewe ndiyo uwe kwenye nafasi ya kusaini mkataba? Badala ya Kitila Mkumbo na Hamza??

Acheni hizo wivu wa kisenge, nchi inachelewa mambo ya kipuuzi!!
Ni wapi ulipo soma nikihitaji hayo unayo nipakazia mimi?
Kutaka taratibu za uwazi zifanyike kwenye mikataba hiyo ni "wivu"?

Hao hao ulio wataja, sasa wanajulikana kuwa ni vikaratasi vya chooni tu; baada ya sakata la DP World. Siwezi hata siku moja kutamani kuwa kwenye nafasi waliyopo wakitumika kulihujumu taifa.
 
Kama haujui ujuwe haujitajiki. Wanojuwa kuwa mkataba unaendelea wamejibu hapo kwenye post namba #68.

Ondoa makasiriko usojekuga kabla ya wakati wako
Sasa ni kipi kipya hapo ambacho ni tofauti na nilicho eleza kabla ya hiyo #68?
 
Wabunge wa chama tawala ni ccm ukimtoa Luhaga Mpina, waliobaki ni wanafiki hawaaminiki wapo kwa maslahi yao ya Ubunge na chama, hawawezi kumkatalia Mwenyekiti wao Rais Samia.
 
Kikubwa tu niwaambie watanzania wenzangu tunatakiwa tujue kwamba kupitia signing ya hio deal familia zitakazoshiriki katika kupitisha hilo zitageuka mabillionea wa kutisha ndani ya week chache zijazo ikiwemo wabunge watakaoshiriki.

Kwao hili ndio main focus na wala si madhara ambayo yatatokana na huo mkataba au faida ambayo itapatikana kwa Watanzania. Watu wanatafuta u trillionaire kwa mgao wa 10% ambao utatolewa na hao wazungu ili waweze kukabidhiwa vitalu vya gas hio.

Jiwe alikuwa sahihi kusitisha aina hii ya mikataba ila walafi hawako tayari kuacha fedha za bure za hongo in expense ya Taifa. Akija kiongozi mwenye uchungu na taifa hili tutarudi kule kule kushtakiana Ulaya na kudaiwa fidia za ma trillions.
 
Yani huwa nashangaa the way Rais SAMIA anavyokomaa na nishati safi.nchi 70% ni wakulima na wanaoishi kwa chini ya USD 1 kwa siku,middle class wanaojiweza kama Wafanyakazi na wafanyabishara wachache bado nao kutumia gas majumbani ni kwa machale sababu ya gharama-bado kila siku majukwaani ni mwendo wa nishati safi.
Sasa hiyo nishati safi atatumia nani kwa statistics kama hizo.
Tuboreshe uchumi wa watu,hayo mambo ya nishati safi yatakuja yenyewe
 
Kikubwa tu niwaambie watanzania wenzangu tunatakiwa tujue kwamba kupitia signing ya hio deal familia zitakazoshiriki katika kupitisha hilo zitageuka mabillionea wa kutisha ndani ya week chache zijazo ikiwemo wabunge watakaoshiriki.

Kwao hili ndio main focus na wala si madhara ambayo yatatokana na huo mkataba au faida ambayo itapatikana kwa Watanzania. Watu wanatafuta u trillionaire kwa mgao wa 10% ambao utatolewa na hao wazungu ili waweze kukabidhiwa vitalu vya gas hio.

Jiwe alikuwa sahihi kusitisha aina hii ya mikataba ila walafi hawako tayari kuacha fedha za bure za hongo in expense ya Taifa. Akija kiongozi mwenye uchungu na taifa hili tutarudi kule kule kushtakiana Ulaya na kudaiwa fidia za ma trillions.
Kwa madeni ya nchi aliyotengeneza huyo mama.

Nchi aina bargaining power tena.

Kinachofuata ni hadithi za machawa kwanini, huo mkataba lazima usainiwe.

Huyo mama lazima atolewe hapo 2025 ameshafanya damage ya kutosha kwa taifa.

Siasa za Tanzania ni predictable, miaka mitano mingine ya huyo mama; only god knows matatizo zaidi atakayotengeneza.
 
Usibishe jambo usilolijua

Mradi ni wa dola bil 42. Wala sio uongo.
Ni zaidi ya Trillioni 100.
Sasa ikiwa Qatar moja ya plant kubwa kabisa duniani kwenye LNG mpaka sasa umegharimu 28 B baada ya expansion sababu wana capacity kubwa kabisa kwenye train zao na hizo ndio gharama wewe unaleta number kichwani tu 42B. Labda niambie capacity kwa maana Tanzania itakuwa number moja duniani?
 
Sasa ikiwa Qatar moja ya plant kubwa kabisa duniani kwenye LNG mpaka sasa umegharimu 28 B baada ya expansion sababu wana capacity kubwa kabisa kwenye train zao na hizo ndio gharama wewe unaleta number kichwani tu 42B. Labda niambie capacity kwa maana Tanzania itakuwa number moja duniani?
Hawa watu hawaelewi tukiwaambia hao watu kama hakina Zitto ni compromised.

Hakuna mtu mwenye akili timamu angeweza tetea mradi ambao ni over estimated wa $42 (billion).

Wana genge lao la wajinga la hakina Zitto na Makamba, wanajazana upumbavu wa local contents kwenye hoja zao, with limited knowledge on the repayment of the sums in contract terms.

Kwa sasa ni too late, nchi ishakuwa cornered, mikopo ya WB ni private. Ni wawekazi hao-hao ndio wame channel hela huko WB kutoa hiyo mikopo ambayo ni non-sustainable lazima waingie hiyo mikopo ya hovyo.

Sasa ni rahisi kuvunja mkataba wa DPW kama hawajawekeza kwenye phase, hawawezi vuna tu bure-bure na wakati Waliji commit kwenye uwekezaji through IGA.

Iła huko kwenye Oil and Gas, na aina ya wawekezaji Shell, Equinox na Exxon Mobil. Hao ni biggest players in the world. They don’t come bigger than, that in the private industry of oil gas popote duniani as a team.

Aaaargh, ilikuwa ukimsikiliza January; na huyu mwanakijiji wa sasa Biteko.

Goodluck
 
Tuna haraka ya nini? Eti muwekezaji anakuja na hizo hela sisi hatuko kwenye risk, unaijua akili ya bepari mzungu Vs akili ya mwafrica anayewaza wizi.

Siku tutakapobadiri katiba na kumuondolea Rais kinga yakutoshitakiwa, spika wa Bunge nk, tutakapokuwa na uchaguzi huru, TISS watakapohojiwa bungeni, raia watakapokuwa wameacha uoga na wako tayari kuifia nchi yao nk HAPO SASA NDIO TUNAWEZA KUKAA CHINI NA KUISIGN MIRADI HII.
 
Hawa watu hawaelewi tukiwaambia hao watu kama hakina Zitto ni compromised.

Hakuna mtu mwenye akili timamu angeweza tetea mradi ambao ni over estimated wa $42 (billion).

Wana genge lao la wajinga la hakina Zitto na Makamba, wanajazana upumbavu wa local contents kwenye hoja zao, with limited knowledge on the repayment of the sums in contract terms.

Kwa sasa ni too late, nchi ishakuwa cornered, mikopo ya WB ni private. Ni wawekazi hao-hao ndio wame channel hela huko WB kutoa hiyo mikopo ambayo ni non-sustainable lazima waingie hiyo mikopo ya hovyo.

Sasa ni rahisi kuvunja mkataba wa DPW kama hawajawekeza kwenye phase, hawawezi vuna tu bure-bure na wakati Waliji commit kwenye uwekezaji through IGA.

Iła huko kwenye Oil and Gas, na aina ya wawekezaji Shell, Equinox na Exxon Mobil. Hao ni biggest players in the world. They don’t come bigger than, that in the private industry of oil gas popote duniani as a team.

Aaaargh, ilikuwa ukimsikiliza January; na huyu mwanakijiji wa sasa Biteko.

Goodluck
Wanaongeza number ili wavune kwenye cost recovery. Hapa ngoja niweke mfano mwepesi ili atayepita anaweza kuelewa. Mfano una kiwanja Kariakoo lakini uwezo huna wa kujenga, anakuja mwekezaji mimi nitajenga gharama nitakata kwenye kodi nikimaliza gharama zangu miaka 10 ya faida unasema deal. Anajenga nyumba kwa Bil 1 akimaliza anakuja anakwambia nimetumia Bil 3, msimamizi wako kapewa chake anasema kweli Bil 3 hapo imekula kwako matokeo utalipa mara 3 bila kujuwa. Mwekezaji anapokuja na gharama kubwa ni kwa maslahi yake maana cost recovery ni 100% hapo serikali ni kuwa on top kuhakikisha gharama ni sahihi ukipata wapiga ma deal wanasema wewe andika tu 42 sisi tuna approve nani analipa hizo gharama? serikali.....
 
Wanaongeza number ili wavune kwenye cost recovery. Hapa ngoja niweke mfano mwepesi ili atayepita anaweza kuelewa. Mfano una kiwanja Kariakoo lakini uwezo huna wa kujenga, anakuja mwekezaji mimi nitajenga gharama nitakata kwenye kodi nikimaliza gharama zangu miaka 10 ya faida unasema deal. Anajenga nyumba kwa Bil 1 akimaliza anakuja anakwambia nimetumia Bil 3, msimamizi wako kapewa chake anasema kweli Bil 3 hapo imekula kwako matokeo utalipa mara 3 bila kujuwa. Mwekezaji anapokuja na gharama kubwa ni kwa maslahi yake maana cost recovery ni 100% hapo serikali ni kuwa on top kuhakikisha gharama ni sahihi ukipata wapiga ma deal wanasema wewe andika tu 42 sisi tuna approve nani analipa hizo gharama? serikali.....
Hawawezi fanya hivyo kwani profit sharing inakuwa based na hiyo 42b usd.
Hiyo Liquified natural gas Tanzania ingeharakisha tu ichimbwe kwani kadiri muda unavyozidi kwenda ndio thamani yake inazidi kushuka, kwani sasa hivi dunia inaenda kuachana na nishati chafu mafuta, gases na makaa ya mawe.
Tunaelekea kwenye solar power, batter, wind etc
 
Back
Top Bottom