Ni Kosa gani la ovyo ulilowahi kufanya tangu uanze kuendesha gari?

Ni Kosa gani la ovyo ulilowahi kufanya tangu uanze kuendesha gari?

Hahaha hao kama una safari ya mbali wanafaa.. watakusaidia njiani kupunguza usumbufu usumbufu wa wenzao..!
Labda mjeda nitambeba kiroho safi...
Hawa wengine wanaovaa kaki au nyeupe, watanisamehe.....

Nimetokea kuwachukia sana..niwaonevu sana wale watu..

Wakiniomba lift nawaambia naishia mita chache tu hapo..
 
View attachment 2183189
Namfukuza Ranger.. Ameshaingia kwenye radar yangu.. Kumbe kuna Lorry mbili kati.. Nikahisi ninaweza kuzimaliza.. Aisee Lorry la kwanza limeisha naona TD42 Civilian inapanda.. Breki nimeshachelewa nitagusa Lorry.. Ikabidi nidownshift gear niingie pembeni..!uzembe..
MUNGU ni mwema..!
Ila hapo mkuu umetoa gari kizembe kwa kweli daah kati ya jambo nililojifunza haswa kwenye barabara kubwa ni hakuna kumgeza wa mbele yako hata kama mnaligi lazima nione mbele kinachokuja hapo ungekya barabara za mbeya tungeshakusahau
 
Hahahaha 😂😂😂😂🤣 nimecheka sanaaaaa!!! Jinsi ulivyoingia CHA KIKE...kwahiyo ulivyogusa upande WA kushoto uliwasha taa au?.

Mwaka Jana na Mimi nilijichanganya kipindi naenda mwanza nakumbuka gari ilikuwa speed 120 alafu nikashindwa kubalance speed na Kona ingawa Ile Kona haikuwa Kali Ila niliamini gari inalala vizur,aisee Ile Kona ilikuwa ya upande WA kushoto kwahiyo ilinazalimu nikae kulia kabisa upande WA pili ili kuipunguza makali.

Abiria walikuwa hawajui lolote linaloendelea Ila Ile situation ilikuwa mbaya sanaa maana Akili ilishakata Tamaa
Katika jambo hautakiwi kulifanya ni kuhama upande..stay on your lane...
 
😅😅 ishanikuta na gari la watu ( brevis) nimeingia njia moja tukuyu huko sasa wakati wa kurudi kidogo mda ulikuwa umeenda si nikaomba kama kutakuwa na njia shortcut basi nikaelekezwa pale safari ikaanza 😂😅 sasa nimetembea parefu kidogo nikafika sehemu imenyooka halafu mkeka safi haa accerate chini kumbe bana nimekaribia kwenye makutano ya barabara kuu (mbeya-kyera) nkaanza kuona kama taa hivi kushika break nshachelewa basi nilienda nikaruka barabara vuuuupuuu bahati nzuri hakukua na gari inapita mda huo basi bhana nikavutwa pale pia gari haikuumia maana nilienda kuingia shambana nilichanika tu mdomo
 
View attachment 2183189
Namfukuza Ranger.. Ameshaingia kwenye radar yangu.. Kumbe kuna Lorry mbili kati.. Nikahisi ninaweza kuzimaliza.. Aisee Lorry la kwanza limeisha naona TD42 Civilian inapanda.. Breki nimeshachelewa nitagusa Lorry.. Ikabidi nidownshift gear niingie pembeni..!uzembe..
MUNGU ni mwema..!
Option uliyochagua ilikua very risky, bora ungekubali kuvamia roli. Dereva wa Costa asingeelewa kinachoendelea mngekutana face to face.

Kongole kwa dereva wa costa.
 
Ila hapo mkuu umetoa gari kizembe kwa kweli daah kati ya jambo nililojifunza haswa kwenye barabara kubwa ni hakuna kumgeza wa mbele yako hata kama mnaligi lazima nione mbele kinachokuja hapo ungekya barabara za mbeya tungeshakusahau
Kama title inavyosema.. Kosa la ovyo..!

Barabara za Mbeya zina shoulders.. Ningekimbilia huko huko..!
 
Option uliyochagua ilikua very risky, bora ungekubali kuvamia roli. Dereva wa Costa asingeelewa kinachoendelea mngekutana face to face.

Kongole kwa dereva wa costa.
Aisee Nilivae Lorry..!!ningeonekana learner kabisa.. Nashindwa kufanya maamuzi ya haraka kwenye hatari.. Option ya pembeni ndio imesave..
Dereva wa basi naye mzoefu kama mimi.. Anajua kusoma mchezo..!
 
Kosa la hovyo kufanya. Niliendesha gari nikiwa vyombo sana[emoji849]
Sitahau hii siku maana gari iliacha njia na kuingia mtaroni, nikakata network kama nusu saa hivi kuja kushtuka raia wameshajaa kibao wakijua nimeshadead. Ile gari iliuzika kama skrepa ila namshukuru Mungu nilitoka salama.

DON'T DRINK AND DRIVE.

Sent from my SM-N960U using JamiiForums mobile app
 
Kuna siku parapanda ingelia sema Mungu hakupenda Tu,tulikua tunatoka kumwangalia mgonjwa makete huko hospitali moja ya masista,sasa wakati narudi ilikua usiku tuko na washakaji wawili ebwana mida ya usiku kama saa tano hivi naona Kwa mbele pikipiki imepiga full then Kwa mbele yangu ni overtake Ile nataka Ku overtake lahaulah la Kwata kumbe sio pikipiki ni mbaula imewasha jicho moja then tuko speed aisee kama sio busara za Yule jamaa wa semi trailer ilikua Ile nyimbo yetu maarufu ndungu marafiki na jamaa waimbe.nilitukana sana hii kitu ya kutukana nahisi madereva wote!
 
Niliingia ofisin asbh na mapema, nikiwa na bashasha na furaha zote, kuna sehem ya kupark, Mara nyingi huwa naingia straight kupaki ili nikiwa natoka nirudi reverse, lakini siku hyo nikasema napark kwa reverse,

Bahati mbaya sana kule mbele ukuta umepinda pinda, mimi nikaanza kureverse huku namwangalia demu mmoja alikuwa anapita, Nikasikia tu Puuuuuuuuuuu, Taa ya nyuma na Bampa vimemwagika.

Siku yangu ilikuwa mbaya sana asbh asbh kwa gharama za kijinga
 
Me mwaka 2020 hapo nipo na gari jipya (kwangu jipya), sasa nikaona ngoja nilionje maana speed 260 wapi hapa Dar nitaitest, nikaenda Tanga kupitia Bagamoyo.

Baada ya siku mbili nikarudi. Sasa njiani nikasema ngoja nijaribu kupiga kibati hadi mwisho. Mvua ilikua imetoka kunyesha barabara ina madimbwi dimbwi ya maji.

Nikatafuta mahali njia imenyooka. Bwana nikakoleza kibati hadi 200 hivi. Kwa bahati mbaya nikapishana na Roli kubwa sasa ile likarusha maji yakajaa kwenye kioo cha mbele.

Ile kupanic nikataka kuwasha wiper zipunguze maji, sasa hapo nimetoka kutumia gari la Toyota nimehamia Mjerumani, aisee Toyota wipers zipo kushoto hafu taa kulia, mjerumani kinyume chake, dah aisee nilipanic sioni kitu mbele hafu nipo kibati mbaya.

Nashukuru Mungu njia ilikua imenyooka na haina magari zaidi ya ilo roli tuliopishana. Ilipokuja kukubali wipers nilirudisha speed maximum 80 aisee.
*****[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mi bhana siku niko speed na v8 mara ghafla nikapishana na lori si ikabidi mimi mle ndani nikwepeshe kichwa (kama nakwepa ngumi)nikajikuta porini tyre zinazunguka hewani zote
Dah[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom