Ni kweli watoto wa English Medium wana IQ kubwa kuliko wetu kayumba?

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
Kazi ya elimu sio kumuingizia mtu vitu kichwani, kazi ya elimu ni kumsaidia mtoto kuugundua na kuufanyia kazi uwezo alionao.

Shule zetu za Kayumba hazimpi mtoto nafasi ya kuuonyesha na kuuvumbua uwezo alio nao bali mazingira yanamfanya awe mjinga zaidi hata kama anatapa A.

Mazingira ya Shule binafsi idadi chache ya wanafunzi, umakini wa walimu, ufatiliaji wa karibu na chakula bora (boarding) vinakuwa vichocheo vya mtoto kufunguka na kujitambua mapema. IQ yake inahamasishwa na sio kuhafifishwa.


Mimi si mtaalam wa elimu, ila nimesoma mahala hili wazo limenishangaza ila kama nimeelewa.

Nini maoni yako, kuna ukweli wowote.
 
Intelligence ni very complex trait ambayo inakua influenced na genes na mazingira. Kwahiyo obvious watoto wa EM watakua na IQ kubwa kuliko Kayumba.
Hii naona kama inamamntiki.
Ukimchukua German Shephard ukamfuga kama mbwa koko mtaani huko lazima awe tofauti ha huyohuyo akifugwa katika mazingira bora. Nadhani hii siri wanasiasa wanajua ndio maana watoto hawapelekwi mjimwema S/M
 
Kama hazipo ni hazipo tu..🤣
Ni kama kumpaka punda rangi, hakumfanyi ageuke kuwa Pundamilia
1000017437.jpg
 
Inasemekana kule uwezo unazikwa, unafichwa unafukiwa huku kwa kulipia uwezo unqvutwa, unawekwa wazi unafunuliwa kilingana na rasilimali zilizopo.

Hii unazungumziaje.
Mkuu sio kweli, utofauti huku ni kiingereza na huku ni kiswahili, mtoto kama ana uwezo ana uwezo tu kama hana ni hana tu utahangaika sana
 
Nafikiri hata watoto wanatofautiana kiasi kuhusu hizo elimu mbili
Wa Private wanapewa kazi nyingi za kufanya kiasi ambacho kinamfanya awe nyumbani zaidi kumalizia masomo
Hapo anakuwa na nidhamu pia, badala ya kuzunguka mitaani au kwenda kuwinda na mbwa

Unakumbuka World Cup Qatar, Japanese walivyokuwa wanaokota taka uwanjani?
Hao wamelelewa tangu wadogo na kufundishwa kila kitu katika uhalisia
Huko Japan watoto hawafanyi mitihani yoyote darasani mpaka wavuke darasa la Nne

Miaka hiyo wanafundishwa kwa vitendo tu
 
Kuna mwalimu ni ndugu yangu anafundisha shule ya vipaji (TABORA BOYS) huwa ananiambia kuwa huwa wana utaratibu wa kuwaadhibu wanafunzi waliofanya vibaya hususan wale wa advance,anakwambia kuwa wanafunzi kumi wa mwisho darasan wa HGL,PCM na PCB wengi kama sio wote ukiangalia historia yao wametoka shule private tena kubwa tu,walimu huwa wanajiuliza kwamba hawa wanafunzi wanaofanya vibaya ni kwamba wameshindwa kuendana na mazingira ya shule za umma au huko walikotoka walikuwa spoon feed yaani wanarahisishiwa kila kitu japo IQ zao ni ndogo!!!??? Anasema kuwa wanafunzi wanaochaguliwa shuleni kwao kutoka hizi st kayumba ni vipanga balaa na ndio wanaoshika nafasi za juu darasani,sema kwa upande mwingine hawa wa private anasema ni wazuri mno kwenye debate kutokana na kuwa na msingi waliojengewa kutoka hizo private schools
 
Kama hazipo ni hazipo tu..🤣

Kuna mwalimu ni ndugu yangu anafundisha shule ya vipaji (TABORA BOYS) huwa ananiambia kuwa huwa wana utaratibu wa kuwaadhibu wanafunzi waliofanya vibaya hususan wale wa advance,anakwambia kuwa wanafunzi kumi wa mwisho darasan wa HGL,PCM na PCB wengi kama sio wote ukiangalia historia yao wametoka shule private tena kubwa tu,walimu huwa wanajiuliza kwamba hawa wanafunzi wanaofanya vibaya ni kwamba wameshindwa kuendana na mazingira ya shule za umma au huko walikotoka walikuwa spoon feed yaani wanarahisishiwa kila kitu japo IQ zao ni ndogo!!!??? Anasema kuwa wanafunzi wanaochaguliwa shuleni kwao kutoka hizi st kayumba ni vipanga balaa na ndio wanaoshika nafasi za juu darasani,sema kwa upande mwingine hawa wa private anasema ni wazuri mno kwenye debate kutokana na kuwa na msingi waliojengewa kutoka hizo private schools
Huu mtazamo wa kumuwekea ugumu mwanafunzi nao umekaaje?
Yaani mtoto akeshe kutafuta materials na kusoma hadi saa tisa usiku wakati walimu walitakiwa kumpa kila uwezo wake unachokihitaji ili afaniliwe.

Mbona Kama Ulaya kumejaa spoon feeding na ndio wametuletea wakina Elon Musk.
Ufafanuzi kidogo
 
Nafikiri hata watoto wanatofautiana kiasi kuhusu hizo elimu mbili
Wa Private wanapewa kazi nyingi za kufanya kiasi ambacho kinamfanya awe nyumbani zaidi kumalizia masomo
Hapo anakuwa na nidhamu pia, badala ya kuzunguka mitaani au kwenda kuwinda na mbwa

Unakumbuka World Cup Qatar, Japanese walivyokuwa wanaokota taka uwanjani?
Hao wamelelewa tangu wadogo na kufundishwa kila kitu katika uhalisia
Huko Japan watoto hawafanyi mitihani yoyote darasani mpaka wavuke darasa la Nne

Miaka hiyo wanafundishwa kwa vitendo tu
Sisi likizo ilikuwa
Kuzurura
Kuwinda ndege
Ligi za ndondo
Kuvua fish mitoni
Kukimbiza tumbili porini
Kuogelea
Kwenda kuchuma matunda porini
Kutengeneza bunduki za majani ya magbi, magari ya mabox, mbao, mabati, miti na fujo zote. Labda ndio mqana shule ya mtaani kwetu wavulana waliochaguliwa kuendelea na Sec walikuwa watano tu.

Hii ya kumpa challenge mtoto likizo itafaa kama haitafanyika kama kumkeep bize bali challenge za holiday backage zilipaswa kuwa practical zaidi.
 
Ni kweli kabisa na hapo ndio unakuta watoto wengine wanaanza na wizi wa mahindi na mihogo na karanga kwenye mashamba ya watu
Sio kwamba hawajui kuwa wanaiba la hasha, wanajua vizuri na hapo ndio wanakuwa nayo mpaka wanakuwa wabunge na mawaziri, polisi na hata ofisa wa ardhi
Jichanganye sasa kwa hao watu walioanza wizi tangu wana miaka 10
Kuhusu challenge za holidays ni jukumu la mzazi kuwahimiza kumaliza maswali mapema na kufurahia holiday pamoja ingawa wazazi wengi huwa wanaona watoto kama adui na kupiga tu
Ila kama mzazi anaewapenda wanae ni vizuri pia kuweka mda wa kuwa nao na hata kuwatoa na kuwapeleka sehemu badala ya kuwaachia kama vibaka
 
Ni kweli kabisa na hapo ndio unakuta watoto wengine wanaanza na wizi wa mahindi na mihogo na karanga kwenye mashamba ya watu
Sio kwamba hawajui kuwa wanaiba la hasha, wanajua vizuri na hapo ndio wanakuwa nayo mpaka wanakuwa wabunge na mawaziri, polisi na hata ofisa wa ardhi
Jichanganye sasa kwa hao watu walioanza wizi tangu wana miaka 10
Kuhusu challenge za holidays ni jukumu la mzazi kuwahimiza kumaliza maswali mapema na kufurahia holiday pamoja ingawa wazazi wengi huwa wanaona watoto kama adui na kupiga tu
Ila kama mzazi anaewapenda wanae ni vizuri pia kuweka mda wa kuwa nao na hata kuwatoa na kuwapeleka sehemu badala ya kuwaachia kama vibaka
👏👏👏
 
Huu mtazamo wa kumuwekea ugumu mwanafunzi nao umekaaje?
Yaani mtoto akeshe kutafuta materials na kusoma hadi saa tisa usiku wakati walimu walitakiwa kumpa kila uwezo wake unachokihitaji ili afaniliwe.

Mbona Kama Ulaya kumejaa spoon feeding na ndio wametuletea wakina Elon Musk.
Ufafanuzi kidogo
Nadhani hatujaelewana mkuu,ninapozungumzia spoon feeding ina maana nyingi,mojawapo ni kumkaririsha mwanafunzi badala ya kumfundisha aelewe ili aweze kusolve same problem katika namna tofauti(walimu watakuwa wananielewa) yaani mwanafunzi awe competant based kuliko theoretical ya kukaririshana kwa ajili ya kufaulu mitihani na ndicho kitu kinachofanyika katika shule za private nyingi wanazalisha wasomi wenye ufaulu mkubwa wa mitihani lakini kichwani ni watupu.lakini pia mara ngapi tunasikia juu ya wizi wa mitihani unaofanywa na hizo shule private maana ile ni biashara hivyo watafanya kila namna kuboost biashara na njia mojawapo ni kuiba mitihani ambayo hiyo huikuti katika shule za serikali au kama ipo basi ni kwa uchache means mtoto anayefaulu huku ni kichwani kweli kweli na ndio hao hata wakienda ngazi zinazofuata za elimu basi wataendelea kuwa wazuri academically
 
Back
Top Bottom