Ni lini Serikali ya CCM itanunua laptop kwa kila mwanafunzi kuanzia shule za kata?

Kwann tuzidiwe na Rwanda, Taifa dogo na ni waafrika wenzetu?

Rwanda hata bandari, ziwa au migodi ya Dhahabu hawana.

Tukienda hivi, watatutawala one day.
Naona unaongea tu bila kufikiri sawasawa. Kwani tatizo letu kubwa hulijui? Hizo laptop atazinunua nani? Zitatunzwa na nani? Kuna mtu anayejali kuhusu mali ya umma nchi hii? 👇👇👇



Anza na kubadili mfumo wa fikra za watu kwanza. Wanajua wanachokitaka? Falsafa yao jumuishi kama taifa ni ipi? Wanataka nini? Viongozi wetu wana maono?

Fikiri sawasawa na usijikite katika matokeo na/au dalili za ugonjwa. Tafuta chanzo cha ugonjwa ili upate tiba sahihi. Vinginevyo ni kazi bure...

 
Kwani Rwanda na CCM Ina tofauti Gani?

Pesa za umma Nchi hii zinaibwa kiasi Gani na Mafisadi?
 
Kwamba kujua kuwa njaa inachangia ufaulu hafifu wa wanafunzi darasani inahitaji takwimu!!

Subiri uchaguzi umekaribia, nitaleta takwimu bila wasiwasi.
 
Hata sijahitaji kusoma sana, Waandikie madaftari laptop atanunua Baba wakifika Chuo.
Serkali ya CCM ina mambo mengi ya kufanya.
 
Hata sijahitaji kusoma sana, Waandikie madaftari laptop atanunua Baba wakifika Chuo.
Serkali ya CCM ina mambo mengi ya kufanya.
Sawa,

Wananchi tutachagua chama kitakachokuja na sera ya kuhakikisha chakula mashuleni kinarudishwa, walimu wanalipwa overtime, laptop wa watoto shule za msingi zinatumika, shule za kata zinaunganishwa Kwa Nishati ya dollar au umeme Nchi nzima.

Wao CCM wapuuze tu, vyama viko vingi😀
 
Kila mwanafunzi ana dawati kweli?! Naona tuanzie hapa kwanza!
Wanakaa Hadi SITA dawati Moja,

Mzazi ukikagua madaftari yalivyojikunja sababu ya kubanwa wanapoandika utachoka.

Ikiwa hatuangalii Elimu, tutafanya nini kizuri?

Ikiwa wanakaa Hadi sasa kumi bila hata kikombe Cha uji, watamwelewa mwalimu akifundisha?

Tunawasubiri Wabunge majimboni, mtatueleza vizuri.
 
Hap
Hapo point ni Masrahi ya walimu na miundo mbinu ya Shule, Mambo ya chakula na laptop ni uduanzi tu hatuna pesa za kuchezea wazazi watimize wajibu wao wa kusomesha.
 
Shule za serkali hazina shida watu watulie watoto wasome, Si elimu ni bure bwana.
 
Unataka takwimu sio?

Tutawapandisha watoto jukwaani tuwaulize ikiwa Huwa wanaelewa somo la HISABATI wakiwa hawajapata chochote tumboni.
 
Unataka takwimu sio?

Tutawapandisha watoto jukwaani tuwaulize ikiwa Huwa wanaelewa somo la HISABATI wakiwa hawajapata chochote tumboni.
We bloody ni mwongo sana ko ukisoma hujala hesabu haipandi? Inaelekea watoto wako ni vilaza sana yani inataka upewe kila kitu?
 
Hap

Hapo point ni Masrahi ya walimu na miundo mbinu ya Shule, Mambo ya chakula na laptop ni uduanzi tu hatuna pesa za kuchezea wazazi watimize wajibu wao wa kusomesha.
Unasahau kuwa wazazi ndio walipa Kodi wanaonlipa mshahara mwalimu kupitia Kodi?

Wazazi tunawahudumia wakiwa home,

Wakiwa shuleni, tunataka Kodi zetu zisinunue v8, zisifujwe Kwa kuibwa, chakula kwenye ghala za Serikali zihakikishe watoto wetu Nchi nzima wanapata japo kikombe Cha uji!!
 
Madarasa na vyoo ni mtihani,Leo unawaza computer!
 
We bloody ni mwongo sana ko ukisoma hujala hesabu haipandi? Inaelekea watoto wako ni vilaza sana yani inataka upewe kila kitu?
Hawapewi Bure, ni Kodi zetu wazazi Nchi nzima tunalipia,

Kwani huko CCM hakuna UMOJA wa wazazi?

Wayajua majukumu Yao mbali na u chaguzi?
 
Madarasa na vyoo ni mtihani,Leo unawaza computer!
KAZI ya ubongo ni kuchakata mipango,

Ikiwa ni mambo mema, tuwe na vision hiyo, hata kama Si Leo, baada ya miaka 5 yufanikiwe.

Maendeleo ni hatua .

Kukosa maono ndo kunasababisha viongozi watumie hovyo pesa zetu wakidhani hazina KAZI, zimezidi,

Kumbe laptop Kwa Kila mwanafunzi Nchi nzima, overtime Kwa walimu nk nk havijalipia.
 
Madarasa na vyoo ni mtihani,Leo unawaza computer!
Mbona wewe huna gari Kwa Mfano, lakini likipita vogue, unajisemea moyoni, one day nitanunua nami vogue!!
 
Tuunge mkono jitihadi za serikali muelekeo ni mzuri tutafika tu, tunapoenda na ni pazuri kuliko tulipotoka, kweli nahisii serikali pia itazame mitaala ya ufundishaji shule za kata lugha wapo nyuma sana ukilinganisha na shule za English medium wakazanie lugha hii ya kibiashara maana ndiyo imekua ikitumika popote duniani kasoro sehemu chache kiswahili bado kina soko nje ila bila kuweka nguvu kwenye lugha ya Kiingereza tubapoteza dira kimataifa pia itusaidie kiushindani kidunia

Pia maboresho ya kimazingira madarasa, maabara ofisi za walimu vyoo nk kuweka learning environment conducive,pia madaraja wapandishwe walimu wenye vigezo kwa wakati, maboresho ya mishahara, vitendea kazi viwe advanced technology imebadilika pia tusione vishikwambi pekee vitatosha.

Walimu wajengewe uwezo wa kimkakati ya kuwawezesha elimu, seminar, mikopo,

Nchi kama Finland [emoji1103] ndiyo nchi pekee kada ya walimu inalipa vizuri kushinda kada zote hata madaktari hawaoni ndani so ni mipango wachukue maoni wayafanyie kazi tuwe na jamii iliyoelimika wabunifu na taifa lenye maendeleo
 
Yote ni mema ,

Pia ni muhimu Serikali ikahakikisha Kila mtoto anapata hapo kikombe kimoja Cha uji Nchi nzima Kwa kuanzia Ili uwepo ushirikiano kati ya mwalimu na mwanafunzi.

Pia in the long-run ziwepo laptops mashuleni Kwa wanafunzi.
 
Maofisini tu hazipo ndio apewe kila mwanafunzi!!?? Nchi ya hovyo sana ..... Nchi Zima inatumia mifumo lakini ofinisini hakuna internet hakuna laptops Wala desktops ....ndio ziende Kwa wanafunzi....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…