Ni mara ya 6 tunashuhudia utiaji saini bomba la mafuta Hoima - Tanga

Ni mara ya 6 tunashuhudia utiaji saini bomba la mafuta Hoima - Tanga

Movie zinaendelea!
Hakuna mradi hapo..
Wanaharakati na watetezi wa mazingira washafungua kesi kibao huko kuzuia huu mradi sababu sehemu kubwa ya huu mradi athari za mazingira hazijaangaliwa..
Barclays UK ni one of the banks/financier wa hii project ameshajitoa na kuna Bank ya Ufaransa pia imeshanyoosha mikono pia.
 
Wafadhili walikuwa hawamtaki dikteta Magufuli John ila sasa japo wamemuondoa lakini ni kama bado hawana imani na Samia.

Kadri ccm watakavyoendelea kung'ang'ania madaraka ndivyo watanzania tutakavyozidi kukosa mambo mengi tofauti na kama wangekuwa wameondoka madarakani. Ni sawa tu na Zanu PF kule Zimbabwe.
 
Believe me hakuna cha Bomba la mafuta wala nini , Wanangu wa lasaba waliokimbilia Tanga kutega uvibarua kwenye hlo igizo la Bomba la mafuta nawasihi warudi makwao wasije wakakuta wake zao washazalishwa
Mu7 anacheka tu manake anajua ataendelea kusaini na marais tofauti tofauti wa TZ yeye akiwa yuleyule miaka yote ijayo
 
Inashangaza kwa kweli.
Mikataba ya iptl,dowans,aggreko,makampuni ya uchimbaji madini ,gas,nk saini Mara moja klia kitu kimeenda!lol

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Mhhh hata Mimi nikajisemea huwa kinasainiwa nn kila siku watu wanasign wanasign tangu Ruge Mutahaba na Mengi wako hai bado linasainiwa tu...Mzee wetu amgekuwepo ungesikia "jamani perekeni pendekezo tusaign vitu vyote pamoja sign nazo zimekuwa nyingi mno watani zangu Waganda nasema uongo ndugu zangu? Ili Pesa za kusafiri safiri tuzifanyizie kazi nyingine....tusaign kila kitu pamoja Museven akikubali fedha tutajenga daraja rire linaunganisha kagera na Uganda iri wanaume wa Tz nao wakachumbie huko na kandarasi tutatoa bure kabisa kutoka Tz au Jeshi letu kabisa kwaajili ya kujenga . daraja.....just joking life is too short...Rip genius.
 
Aug 5. 2017 Museveni alikuja Tanga kuweka jiwe la msingi, baadaye JPM alienda Uganda kusaini, September 2020 Museveni alikuja Dar kutia saini, Museveni akaja tena Chato kusaini, April 11, 2021 Rais Samia akaenda Uganda kusaini, jana Mseveni kaja tena Dar kusaini. Dah!

Kazi iendelee.
===============
Ukweli ni kwamba.....
===============
Though sina taarifa za uhakika ila nashawishika kuamini kuwa ujenzi unafanywa kwa phases na unafanywa na makampuni tofauti,hivyo kila mjenzi anapopatikana contract inasainiwa
 
Mhhh hata Mimi nikajisemea huwa kinasainiwa nn kila siku watu wanasign wanasign tangu Ruge mtahaba na Mengi wako hai bado linasainiwa tu...Mzee wetu amgekuwepo ungesikia "jamani perekeni pendekezo tusaign vitu vyote pamoja sign nazo zimekuwa nyingi mno watani zangu Waganda nasema uongo ndugu zangu? Ili Pesa za kusafiri safiri tuzifanyizie kazi nyingine....tusaign kila kitu pamoja Museven akikubali fedha tautajenga daraja rire linaunganisha kagera na Uganda kandarasi tutatoa bure kabisa kutoka Tz......just joking life is too short...
Sasa muulize musaidiwe kuelewa huwa wanasign nini?
 
....Inawezekana mkataba una kurasa nyingi za kusaini!
 
Kuna tatizo la utoaji wa habari za kinachosainiwa. Kwenye mradi huu wa ujenzi wa bomba la mafuta, kuna mikataba mingi inayosainiwa, wananchi hatuambiwi jumla ya mikataba na kinachosainiwa ni nini. Wanadhani alichosaini JPM ni kile kile alichosaini Samia, na Samia alipokwenda kusaini Kampala ndio kile kile kilichosainiwa hapa Dar.

Kwenye hii mikataba iko ya intergovermental, na host goverment. Intergoverment ni mikataba ya serikali za Uganda na Tanzania, ambayo imesainiwa pande zote. Host government ni mkataba wa sisi Tanzania ni host tuu wa bomba la mafuta. Mwenye mafuta ni Uganda, mchimbaji ni Total, ndie mwenye bomba. Tanzania tunapitisha tuu. Mfano ule mkataba wetu wa asilimia 16% ya free carried shares kati ya Tanzania na Barrick, imesainiwa mikataba 12!.

Hivyo hata baada ya kisainiwa mikataba iliyopo, bado kuna mingine itafuata.

Problem ni information.

Pia vyombo vya habari wakikutana na waziri wa Nishati , Waziri wa Mambo ya Nje au Mkurugenzi Mkuu wa TPDC huwa wanakuwa wasikilizaji tu, hawaulizi maswali ya kutaka ufafanuzi, mikakati n.k

Tutegemee waandishi wa habari watakuwa wadadisi kama wanaJF na kutumia uzi huu wa comment hii ya Paschal Mayalla kama 'framework' ya uandishi wao na pia 'yardstick' ya kutumia kuwahoji wakubwa iwe ni kwa Prof. Palamagamba Kabudi kuhusu 'mahabusu wa kisiasa' au Dr. Medard Kalemani kuhusu 'Luku' au Dr. Dorothy Gwajina na covid-19 n.k
 
Kuna tatizo la utoaji wa habari za kinachosainiwa. Kwenye mradi huu wa ujenzi wa bomba la mafuta, kuna mikataba mingi inayosainiwa, wananchi hatuambiwi jumla ya mikataba na kinachosainiwa ni nini. Wanadhani alichosaini JPM ni kile kile alichosaini Samia, na Samia alipokwenda kusaini Kampala ndio kile kile kilichosainiwa hapa Dar.

Kwenye hii mikataba iko ya intergovermental, na host goverment. Intergoverment ni mikataba ya serikali za Uganda na Tanzania, ambayo imesainiwa pande zote. Host government ni mkataba wa sisi Tanzania ni host tuu wa bomba la mafuta. Mwenye mafuta ni Uganda, mchimbaji ni Total, ndie mwenye bomba. Tanzania tunapitisha tuu. Mfano ule mkataba wetu wa asilimia 16% ya free carried shares kati ya Tanzania na Barrick, imesainiwa mikataba 12!.

Hivyo hata baada ya kisainiwa mikataba iliyopo, bado kuna mingine itafuata.

Problem ni information.
Leo naona umerudi 2017, hongera sn
 
Back
Top Bottom