Ni mkoa gani mzuri kwa kuanzia maisha from Zero?


Nenda Dar, specific Mbagala stand au Temeke stereo tafuta connection na wasukuma toroli za mizigo zile ndogo. Tengeneza toroli kwa bajeti ya pesa yako. Endeleza harakati.

Nenda kwenye majiji yenye msongamano,
Dar (Mbagala, Temeke, K/koo), Mbeya (Mwanjelwa, Kabwe etc), Mwanza, Dodoma nk.

Nunua trey tatu za mayai hapa gharama kwa tray 7000 - 10000 kutegemea na msimu, sufuria kubwa yenye uwezo wa kuchemsha mayai mkaa, chumvi kisha ingia mtaani kuuza mayai ya kuchemsha. Ukizoea mji tafuta vijana wengine wasiojiongeza wabebeshe tray kadhaa na wewe utaanza kuwa muajiri.

All the best
 
Shukrani sana mkuu
 
Wezi wapo kila mahali Mkuu,

Ila kwa kuanzia maisha kwa unafuu patakufaa, isitoshe hata vyumba viko karibu na barabara ya kuingia city centre.
Shukrani mkuu
 
Maisha huwa hayana adabu njia anazo ziona rahisi mwenzako zinaweza kuwa ngumu kwako na njia ngumu kwa mwenzako zinaweza kuwa rahisi kwako jaribu popote
Sawa mkuu
 
Jibu sahihi.
Popote utakapoamua unaweza kutoboa maisha hayana formula kikubwa imani usitegemee watu kukupa opinion za kweli kuhusu mji sahihi kutafuta maisha akili yako inapokwambia ndio hukohuko wish all the best
 
Njoo Dar, nenda mbagala au kongowe tafuta chumba cha 20, lipa miez 3. Tafuta mkokoten, weka matunda na miwa anza harakati. Huna motot huna mke utatoboa.
 
Katika maisha yako tafuta sehemu ambayo itakupa changamoto na kuamsha morali ya utafutaji

Unaweza kaa penye unafuu wa maisha lakini mfuko wa suruali hautuni kulingana na eneo hilo kutokuwa na mzunguko kiuchumi
 
Chumba mimi nimepanga nalipa kodi 20000 kwa mwezi.
Vyumba vipo kuanzia 15000 +
Anayesema eti maoni yangu ni "dagaa mchele" hajui kitu.
Wakati nafika mjini Nilipewa kazi ya kuhudumia kitimoto (napenda sana).
Kurunzi
Chumba cha 20k huku mburahati au manzese midizini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…