Ni muda sasa sijawahi kumbuka ndoto yoyote niliyoota

Ni muda sasa sijawahi kumbuka ndoto yoyote niliyoota

Sio KUKEMEA. Ni KUJIZATITI.

Unajua maana ya KUJIZATITI???

You FORTIFY yourself, UNAKITA NGOME NA MIPAKA.

Lazima uwaonyesha MIPAKA baina yako na wao, na wakae kabisa wakitambua HILO na walitambue kwa DHATI bila masihara.

Hii ni SHERIA ya ulimwengu. Sheria ya UHURU kwa kila MJA.

Ukishasema SITAKI hata Mungu mwenyewe hawezi kukusogelea. UNAKITA NGOME mpaka pale utakapoamua VINGINEVYO.

Cc: min -me Extrovert
Kukita ngome kwa maana ya kuwa na msimamo thabiti juu ya kumuelekea Mungu, hapo nimekupata vyema kabisa
 
Of course it's happening inside our head, Harry, but why on earth should that mean, that it's not real?"

But for real (pun not intended), dreams are a way of our brain to process the things we've experienced in our life, hence why in dreams you will usually encounter things you very recently experienced. They aren't real in the same way as our daily lives, like when a building collapses in your dream it obviously won't have the same effect as a building collapsing in real life, but dreams are real in the same sense that our regular thoughts are.
 
Habari za asubuhi wadau

Kama kichwa cha habari kinavyo sema. Nina uhakika kila siku naota ndoto nikiwa usingizini, lakini cha ajabu ni kwamba nikiamka tu asubuhi sikumbuki ndoto hata moja.

Ni muda mrefu sina kumbukumbu ya ndoto yoyote ile, naota ndoto zaidi ya tatu lakini asubuhi ifikapo nikijaribu kukumbuka nashindwa.

Hili ni tatizo au ni hali ya kawaida tu? Ni zaidi ya miaka mitatu sasa nimekuwa na hali hii. Nifanye nini?
Wewe kama mimi tu mkuu. Halafu naambiwa sijui nimefungwa na wachawi nisiote na kujua maono sasa wanaoniambia ajabu wana life gumu kuliko mimi sasa sijui kati yangu na wao aliyefungwa nani
 
Sasa we ndoto inakusaidia nini maishani mwako??
Binadamu mnapenda kujitengenezea matatizo
 
Yani ww n kama mm tu! Days be4 hili tatizo nilikuwa naota hadi mambo ya kesho yangu yatakuwaje, nitakutana na nan au nitafanya nini au nini kitatokea kesho au siku za mbeleni. Na ndoto zangu zilikuwa very straight! Hadi shule nilikuwa naota hadi mitihan kuwa swali fuln nitalikuta kwenye paper. Kuna kipindi niliambiwa na jamaa yangu kuwa ndoto nazoota niwe naziweka siri yani nisiwe nawambia watu kwa madai kuwa kufanya hivyo najiweka hatarini sana na nguvu za giza. Nilimpuuza ila baada ya saiz kushindwa kukumbuka chochote nimeanza kupata mashaka. Mm sasa hivi naweza kuota ndoto uck nikakaa kitandani kabisa ili niihifadhi hiyo ndoto ila nikilala tena nikaamka hata nifanyaje sikumbuki kabisa. Nitakumbuka niliamka uck ili niihifadhi ndoto hiyo lkn wapi. Wengine humu mnaweza kudhan hii haiwezekani ila mm ndiyo hali niliyofikia. Saiz ili niikumbuke ndoto ambayo nikiota uck nikabahatika kuamka uck huo huo basi lazima niihifadhi kwa njia ya maandishi🤔, amini kila kitu kiliumbwa kikiwa na maana yake! Hakuna kilichoumbwa alafu hakina maana. Ukiona hakina maana basi ujue ww ndo hujui maana yake.
Ni kweli kabisa si kila ndoto ni ya kusimulia hasa hizi zenye maono,,na mfano mzuri tunaupata katika vitabu vitakatifu pale Yusuphu rehema na amani ziwe juu yake alipomwambia baba yake kuwa nimeota nyota 11 na mwezi vikinisujudia,baba yake akamwambia usiwaambie ndugu zako kwani shetani ataleta uadui kati yenu

Kwahiyo hayo mambo yapo,,na nyengine ni za maonyo

Binafsi huko nyuma nilikuwa sio mtu wa ibada,siku moja niliota malaika wamekuja kuchukua roho yangu ingawa sikuwaona lkn nilihisi uwepo wao karibu yangu,nikajuta sana na kutamani ningefanya ibada,wakachukua roho yangu na ikawa inapaa kwenda mbinguni,najiona kabisa napaa kwenda mara nikashtuka,nilitafakari sana na ukawa mwanzo wa kujikurubisha kufanya ibada,,,na kwa mujibu wa quran roho ikitoka kwanza chap inaenda kwa muumba kisha inarejeshwa kwa mhusika kaburini,kwahiyo nami niliota hivyo hivyo roho ikienda mbinguni,na ni sahihi sikuwaona malaika kwasababu ukifa ndio utawaona live kabisa
 
Of course it's happening inside our head, Harry, but why on earth should that mean, that it's not real?"

But for real (pun not intended), dreams are a way of our brain to process the things we've experienced in our life, hence why in dreams you will usually encounter things you very recently experienced. They aren't real in the same way as our daily lives, like when a building collapses in your dream it obviously won't have the same effect as a building collapsing in real life, but dreams are real in the same sense that our regular thoughts are.
It's possible that our past experience is involved, but remembering it after waking up is a must.
 
Hiyo kitu siijuagi kabisa. Kiufupi mm n mshamba na hiyo kitu!
Kuna Uzi upo hapa JF waweza utafuta andika Tahajudd (meditation) umeandikwa na Mtambuzi

Utajifunza aina mbalimbali za kufanya meditation

Kiufupi itakusaidia Sana kuamsha nguvu zako za kundarini au kiroho

Kama upo DSM amka saa nane au tisa utaona akili yako itavyokuwa nyepesi na mambo yaliyojufunga yatafunguka.

Cosmic power inachilia mida hiyo
 
Kukita ngome kwa maana ya kuwa na msimamo thabiti juu ya kumuelekea Mungu
Sio kumuelekea Mungu, ni kujielekea mwenyewe.

Huhitaji kumuelekea Mungu popote, you only need to EXERT your own power and go deep within.

Nimekwambia hapo ukiona huoti ndoto kuna uwezekano watu au viumbe fulani au nguvu fulani ya kiteknolojia WANAZITEKA fahamu zako au WANAFUTA KUMBUKUMBU ZAKO. They hijack your memory and your power to see.

Na hii ni kwa sababu UMEWARUHUSU kwa kujua ama kwa kutokujua.

Sasa FUTA HIYO RUHUSA na Uiondoe kabisa.

QUASH IT AND NULLIFY IT in its entirety and FORTIFY YOURSELF.

TAKE CHARGE OF YOUR LIFE AND BECOME THE ONE IN AUTHORITY.
 
Ni kweli kabisa si kila ndoto ni ya kusimulia hasa hizi zenye maono,,na mfano mzuri tunaupata katika vitabu vitakatifu pale Yusuphu rehema na amani ziwe juu yake alipomwambia baba yake kuwa nimeota nyota 11 na mwezi vikinisujudia,baba yake akamwambia usiwaambie ndugu zako kwani shetani ataleta uadui kati yenu

Kwahiyo hayo mambo yapo,,na nyengine ni za maono

Binafsi huko nyuma nilikuwa sio mtu wa ibada,siku moja niliota malaika wamekuja kuchukua roho yangu ingawa sikuwaona lkn nilihisi uwepo wao karibu yangu,nikajuta sana na kutamani ningefanya ibada,wakachukua roho yangu na ikawa inapaa kwenda mbinguni,najiona kabisa napaa kwenda mara nikashtuka,nilitafakari sana na ukawa mwanzo wa kujikurubisha kufanya ibada,,,na kwa mujibu wa quran roho ikitoka kwanza chap inaenda kwa muumba kisha inarejeshwa kwa mhusika kaburini,kwahiyo nami niliota hivyo hivyo ndoto ikienda mbinguni,na ni sahihi sikuwaona malaika kwasababu ukifa ndio utawaona live kabisa


Unapokuwa umefika hatua nzuri ya kuota na jambo kutokea unabidi kuwa mkimya Sana

Kuwaambia inaweza kuwa vizuri ikiwa umelenga kkuwasaidia in positive way
 
Nilikuaga sifatilii mambo ya ndoto, sababu ya kufatilia ilianza hapa....

Dingi angu mdogo alifariki,....kuna jambo jema nilimtendea, muda huo mie nliona kama wajibu tu wa mtoto kwa mzazi (japo ni jambo ambalo lilipaswa kufanywa na wanae wa kuzaa na walikua na uwezo ila hawakufanya) kumbe kile kitu mzee alikipokea kwa namna ya pekee kabisa.

Baada ya msiba muda umepita, nikaanza kuota ndoto 1 tu hiyo hiyo kila siku yani kinachobadilika ni nguo tu ila ndoto ile ile.

Naota nipo upande wa pili wa barabara nae yupo upande mwingine, basi nikimuangalia anatabasamu halafu anapunga mkono kuniaga, nataka kuvuka barabara nimfate magari yanapita yanapita mara anapotea. 🙄Hii ndoto ilidumu miaka hadi nikaanza kuhisi kero. Siku moja nikaota hiyo ndoto ila wakati mzee kakaa barabarani nikaingia dukani nikaanza kumuuliza dada anaeuza duka, eti yule mzee pale ni baba angu ila kila siku anatokea ananichekea na kuniaga maana yake nini, dada muuza duka akajibu mie sijui maana yake tafuta mtu mzima akuambie.

Asubuhi nimeamka tu sijatoka kitandani nikampigia dada angu (ana duka) nikamueleza ile ndoto na imekua ni muda sasa akajibu "mie sijui maana yake mpigie baba akuambie" nikamcall baba mdogo mwingine (mdogo ake na marehemu). Akasema nipe nusu saa nakupigia.

Si ndio akaniambia, marehemu alikua anafurahia sana pale hospital nyakati zake za mwisho akinishukuru kwa jambo hilo, ni jambo alikua analisema mara kwa mara, namshukuru eve bila yeye leo nisingekua hapa"

Na hiyo kuota pande mbili za barabara siwezi kumfata ndio hivyo he is dead siwezi kumfata.

Baada ya kuambiwa ile maana ukawa ndio mwisho wa ndoto sijawahi kumuota tenaaaa....kumbe haikua ndoto ulikua ni ujumbe ambao nlikua sijui maana yake.

May his soul keep resting.🙏
 
It's possible that our past experience is involved, but remembering it after waking up is a must.
I think we forget our dreams really quickly after we wake up because dreams happen in the same part of our brain that handles muscles.

As soon as you wake up and start moving, the memories of the dream get crowded out by your muscles doing stuff.
 
Back
Top Bottom