Ni muda sasa sijawahi kumbuka ndoto yoyote niliyoota

kuota ndoto na kikatokea niunabii au kipawa watu wenyekipawa hiki wanafatiliwa sana na wachawi.hivyo unaweza kufungwa kichawi au ukajifunga mwenye kwa uzinzi n.k
Mkuu ni kweli kabisa, Basi ni vyema kuzidisha sala na maombi tu maana adui yako huwezi mjua
 
Ndoto ni zaidi ya ndoto tu.

Wengine sisi ndoto ni ulimwengu wa pili wa yale yajayo au yaliyokwisha tokea.

Tatizo wengine mnaishi kama ng'ombe bandani hamuijui nguvu ya maombi kupata mafunuo.
 
Hayo uliyo sema yanafikirisha sana kaka, kwasababu kama mtu huna uadui na watu, kwanini bado wanaamua kukuchezea. Ila naamini njia pekee ya kutafuta usalama ni kumuelekea Mungu pamoja na kuomba ulinzi wake.
 
Ndoto ni zaidi ya ndoto tu.

Wengine sisi ndoto ni ulimwengu wa pili wa yale yajayo au yaliyokwisha tokea.

Tatizo wengine mnaishi kama ng'ombe bandani hamuijui nguvu ya maombi kupata mafunuo.
Sasa mkuu, unanishauri nifanye nini ili kuondokana na tatzo hili
 
Wakristo, Mungu alisema akitaka kuongea nasi basi atazungumza nasi kwa njia ya ndoto. Hivyo, kwa Mkristo sio vizuri kupuuza ndoto maana ni taarifa inayobidi kuifanyia kazi.

Hata Shetani pia anatumia ndoto kutoa taarifa zake. Kwa hiyo unahitaji umakini kujua taarifa ya Mungu ni ipi na ya Shetani ni ipi.

Sasa Shetani mara nyingi hupenda kuharibu taarifa alizopewa mtu kwa kumsahaulisha ndoto aliyoota. Hivyo ni muhimu kumuomba Mungu akukumbushe ndoto na ukiweza unapoamka, iandike ndoto yako kisha utaipatia maana - wakati mwingine ndoto ni mafumbo, maana zake ni mpaka uyafumbue.
 
Hayo uliyo sema yanafikirisha sana kaka, kwasababu kama mtu huna uadui na watu, kwanini bado wanaamua kukuchezea. Ila naamini njia pekee ya kutafuta usalama ni kumuelekea Mungu pamoja na kuomba ulinzi wake.
usishangae hilo br ukishapigwa mhuri wa kichawi kila utakapo enda lazima wachawi wakusalimie kwanza iwe kwakukuchezea au kukukwamisha mchawi furaha yake nikuona wengine wanatabika.
 
Hayo uliyo sema yanafikirisha sana kaka, kwasababu kama mtu huna uadui na watu, kwanini bado wanaamua kukuchezea. Ila naamini njia pekee ya kutafuta usalama ni kumuelekea Mungu pamoja na kuomba ulinzi wake.
Mchawi hana akili! Hawanaga sababu, wengine wanazo... Ila ukitaka kuijua na kuielewa hii dunia basi hutataka kucheka na mtu na utachukia watu wote. Automatically tuna tabia ya kumchukia mtu ghafla pasipo na sababu ya msingi. Kumbe ni wivu tu! Hasa sisi Waafrika.

Ukitaka kuwa mchamungu hakikisha huna makandokando yoyote! Mchamungu, mchamungu kweli!

Na ukitaka kuwa kigagula mshirikina basi hakikisha unakuwa kigagula bin mshirikina kweli! Mfano wa hilo ni wafanyabiashara wa Kariakoo.

Binadamu tuna kasumba sana!
 
NAKAZIA
 
usishangae hilo br ukishapigwa mhuri wa kichawi kila utakapo enda lazima wachawi wakusalimie kwanza iwe kwakukuchezea au kukukwamisha mchawi furaha yake nikuona wengine wanatabika.
Ni kweli wachawi hawapendi waone mtu anapitia hali nzuri, lakini mkuu mimi napiga maombi tu mwanzo mwisho hasa wakati wa kulala na kuamka
 
Ni kweli kwamba ni lazima uchangue njia moja, na ukiwa hueleweki ndyo hapo unawapa nafasi maadui. Ila pia ni muhimu kujikinga kwa kumtegemea Mungu hasa. Mkuu nimekuelewa vyema sana hapo.
 
Ndoto ni moja wapo ya Njia ambayo Mungu anatumia kuwasiliana na Binadamu!

Kumuonya, kumpa njia ama kumpa Ujumbe juu watu wake wa karibu ama juu ys Mtu mwingine.....!

Ukiona unaota Ndoto hafu unasahau, cha kwanza jua kwamba wewe sio Mtu wa kawaida, kuna kitu unacho, na hicho ulichonacho ndo Mungu anatumia Ndoto kukufikishia Ujumbe, ila Shetani kwa kujaribu kuua kile ulichonacho anaingilia ndoto zako kwa kukufanya Usahau...!

Naongea kwa Uzoefu, nimepita unachopitia, ni mambo ya kiroho, coz chochote kinachotendeka Duniani kilianzia kwenye Ulimwengu wa Kiroho, na ukizuia Ndoto za Mtu, umezuia jana ya Mtu, so wewe unaishi tu kwa sababu kumekucha na unapumua....!

Lengo lako la kuishi limezuiwa kwenye Ndoto...!
 
Je umebadili nyumbani ya Ibada, namaanisha mahali ulipokuwa unasali ndipo unaposali sasa?
Kuna kipindi nilikuwa uhamishoni ikanibidi nisali kanisa fulani kwa miezi minne, nikapatwa na hiyo hali ya kutokukumbuka ndoto, mpaka baada ha kuondoka hapo tena nikarudi kwenye hali ya kawaida.
 
unatumia njia gani kupata maana za ndoto ulizoota?
 
Kama ni mambo ya kiroho basi tiba yake itakuwa ya kiroho pia. Mkuu umesema ulishawahi kupitia hali hii, uliwezaje kujitoa au kupona?
 
Mimi naishi sehem moja kwa muda mrefu sasa, na nyumba ya ibada ninayo hudhuria ni moja tu
 
Mbaya ni kwamba hata ukifa unaweza usijue ukadhani Bado umelala,wengine tupo kwenye ndoto ndefuuu zisizoisha,ni juzi tu nimeota ndoto ndani ya ndoto.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…