Ni nani alitaka kumuua Tundu Lissu?
Na je ikibainika serikali ndo imehusika mtaficha wapi sura zenu?
 
Naanza na kutoa pole kwa watz wenzangu juu ya Mh.Lissu kwa janga lililomkuta..
Kwamfano Siku imetokea Mara Mungu amejaalia hao wahalifu wakakamatwa na IKIBAINIKA kua serikali haikuhusiana kabisa na matendo hayo..
HAO WENYE KUISHUTUMU SERIKALI YETU YA AWAMU YA 5,JE NYUSO ZAO WATAZIWEKA WAPI??

Sent from Calculator Phone vesion007
Labda itakua serikali ya lumumba ya japan

Sent using Jamii Forums mobile app
 
TUSUBIRINI TUWE NA SUBRA NA TUZIDI KUMUOMBEA MH,LISSU APONE
NAUHAKIKA AKIJA SALAMA ANAYO MENGI SAANA YA KUSEMA NA WALIOMFANYIA,
HUKU NA SERIKALI PIA IKIENDELEA NA UCHUNGUZI WAKE.
SIONI FAIDA YA KUMWAGIANA POVU HUMU PASIPO NA SABABU YOYOTE

Sent from Calculator Phone vesion007
 
Umewahi ona Hakimu akajihukumu labda ije tume ya nje, tokea Uhuru wapi serikali iliwahi sema inahusika au mwembe YANGA, nwangosi, Nape, Roma, Saanane, Ulimboka, Mtikira, ................

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aache propaganda kuteka watu na kuwapoteza ktk utawala wake hii inaashiria kushindwa kujibu hoja nzito kuhusu utawala wake anachokifanya anawakamata na kutaka kuwaua wale wenye uthubutu wa kuhoji ..my take ajue madaraka yanaisha huenda akimaliza muda wake akaishi uhamishoni kwa sababu hii katiba piga ua lazima itabadilishwa haipiti miaka kumi tutapata katiba mpya ..na ccm ipo siku wataondoka hili suala wasijifariji kwamba watabaki milele wakitawala e.g.zanzibar shein alishindwa uchaguzi ; bagbo na yahya jameh ..namhurumia sana magufuli na shein kwani attack wanazofanya ndio zinazoofisha utendaji wa serikali zao hii leo wameshindwa hata kuongeza mishahara ..kuajiri ..zimebaki porojo tu na kidiplomasia tumedondoka vibaya mikopo elimu ya juu hakuna tena hivyo mwambieni magufuli ccm ikitoka au katiba ikibadilishwa anayo kesi ya kujibu ukonga apaone tu kwa kuwapeleka akina manji na yeye ataingia ..hii mtanikumbuka

Cc keki ya harusi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serkali ndio wauaji
Makonda anavuja damu za watu yule mda utasema
 
Kabla ya kushutumu serikali watu wameshindwa kuhoji hili wakati katika CV ya Mbowe hakuna sehemu hata moja inayoonyesha Mbowe aliwai hata kupitia Mgambo au JKT lakini kabla hata ya Police kutoa statement tayari Mbowe alikuwa ameshataja mpaka aina ya silaha iliyotumika kumshambulia Lissu je alijuaje kama silaha iliyotumika ni SMG au machine gun hapa namnukuu '' Gari iliyokuwa inamfata nyuma ghafla ilitoa bunduki aina ya machine gun SMG na kuanza kumiminia risasi'' swali la kujiuliza alijuaje wakati hapakukutwa silaha eneo la tukio ?
Parochial Mind.
 
Back
Top Bottom