UmkhontoweSizwe
Platinum Member
- Dec 19, 2008
- 9,454
- 8,894
Basi we huzijui siasa za ndani za chadema.Sidhani kama Lissu yupo kwenye ramani Za kugombea Urais sidhani Na sidhani kabisa
Sent using Jamii Forums mobile app
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Basi we huzijui siasa za ndani za chadema.Sidhani kama Lissu yupo kwenye ramani Za kugombea Urais sidhani Na sidhani kabisa
Sent using Jamii Forums mobile app
==============================
Baada ya michango mingi iliyowekwa hapa kuna dhana niliyoigusia tu (Internal politics within CDM) na wengi kuuliza kwa nini sikuifafanua. Hapa chini naiongeza ingawaje mwanzoni sikuipa kipaumbele.
Dhana ya 5.
Maadui wa ndani wa CDM walitaka kumuua Lissu ili watimize malengo 3 yafuatayo.
1. Lissu aondoe ushindani katika uchaguzi ujao wa mwenyekiti.
2. Lissu aondoe ushindani katika uteuzi ujao wa mgombea uraisi ifikapo 2020.
3. Lissu atumiwe kama kafara ili kuipa CDM mvuto wa kuonewa huruma na kuichukia serikali katika uchaguzi wa 2020.
Mkuu kumbe BAVICHA walipeleka baruwa kwa IGP na DCI kuripoti kutishiwa kwa Lissu tarehe 24 Aug., 2017.Ujinga wa Lissu ni kufanya mambo kama mwanakijiji sijui wa wapi tu!!! Anajua kabisa ukitishiwa au ukiona dalili hatari kwa usalama wako ni wapi pa kwenda kutoa taarifa! Aliishia kuita press conference akidhani ni siasa! Matokeo yake ndo hayo...
Sent from Moto G
Unapoweka dhana (theories) unapaswa kuwa mkamilifu (exhaustive).Kote ulikuwa unavuta the main points zako
Umejaribu kuzungukaa weee kumbe sababu kubwa ni dhana namba 5
Unapoweka dhana (theories) unapaswa kuwa mkamilifu (exhaustive).
Unapaswa kuweka kila kitu hata kama utakuja kikanusha baadae, kama ilivyokuwa kwa dhana namba 1.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kama huijui systems (au holistic) analysis basi hutanielewa. Nilichofanya ndio mlolongo wa kisayansi katika utafiti wa aina yoyote ile.Hyo namba 1 ulisema haipo, sasa uliiandika ili ujaze booklet au?
Kama huijui systems (au holistic) analysis basi hutanielewa. Nilichofanya ndio mlolongo wa kisayansi katika utafiti wa aina yoyote ile.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hapana.Kwahiyo ndio upo kwenye utafiti su umetuletea mrejesho wa utafiti wako?
Kuripoti tishio la kuuawa hawawezi kuripoti BAVICHA; anaripoti mhusika. Kila ukiripoti ni lazima polisi wakuulize unamtilia shaka nani? BAVICHA hawawezi kujibu hilo swali itakuwa ni heresay. Je, kwa nini Lissu mwenyewe hakuripoti?Mkuu kumbe BAVICHA walipeleka baruwa kwa IGP na DCI kuripoti kutishiwa kwa Lissu tarehe 24 Aug., 2017.
Hii ni kufuatia taarifa ya mkutano wao wa hadhara. Soma uzi huu.
IGP aanikwa kumbe Lissu aliripoti kuwindwa, Walinzi waliondolewa, askari wanaolinda spika na mawaziri walijifungia
Kwa kweli sina majibu ya maswali yako. Mimi nilileta taarifa zilizowekwa kwenye bandiko lingine nikitumaini zitasaidia mjadala.Kuripoti tishio la kuuawa hawawezi kuripoti BAVICHA; anaripoti mhusika. Kila ukiripoti ni lazima polisi wakuulize unamtilia shaka nani? BAVICHA hawawezi kujibu hilo swali itakuwa ni heresay. Je, kwa nini Lissu mwenyewe hakuripoti?
Sent using Jamii Forums mobile app
Serikali hii haipendwi na watanzania bali watu wanaidshi kwa Uoga wanaogopa visasi kukomoana kubambikiana kesi, serikali ya CCM hawajawahi kujibu hoja kwa hoja za Lisu bali hutumia polisiccm kumtisha kumnyanyasa kumsachi nyumbani kwake, kutaka kumpima mkojo ili abambikiwe kesi za unga nk, nyie CCM na serikali yenu humukuwa mkifahamu watanzania wanampenda Lisu kiasi hiki, mlidhani Lisu hana watu lakini baada ya jaribio la kumuua kukwama mmetambua kuwa wapo watanzania wengi pamoja na mataifa mengi yanamuunga mkono na huko kenya anapotibiwa amepewa Ulinzi mkubwa na matibabu bora chini ya uangalizi mkubwa sana, kwa taarifa yako ingawa umekuja na story ndefu sana mtuhumiwa namba mija ni Bashite, Le mutuz na wenzako kadhaa hilo halina ubishi na wananchi wengi ndivyo wanajua.Nasema "alietaka kumuua" kwa sababu ukiangalia yale matundu ya risasi upande wake wa gari utajua kuwa hawa watu hawakutaka kumtishia tu. Walidhamiria kumuua.
Niungane na Watanzania wenzangu kumuombea Tundu Lissu dua/sala ili apone kikamilifu, Amin.
Nimejiuliza maswali mengi kuhusu shambulio hili la kipekee kwa mbunge (sijui kama kulikwishatokea shambulio jingine kama hili), hapa Tanzania.
Yafuatayo ni malumbano ya kifikra ndani ya nafsi yangu kuwa ni nani hawa waliotaka Tundu Lissu afe. Maoni yako yanahusika, tafadhal.
Nimefikiria wahusika katika dhana 4. Nitazichambua hizi dhana moja moja.
Dhana zenyewe ni hizi. Washambuliaji ni:
1. Vichaa fulani tu. (Random act)
2. Raia wenye chuki na Lissu kwa kuikalia kooni serikali.
3. Serikali yenyewe
4. Watu wenye chuki na serikali (false-flag attack) ili waisingizie serikali uovu huu.
1. Vichaa fulani tu. (Random act)
Hii inawezekana lakini inakinzana na taarifa za kuwa Lissu alikuwa anafuatiliwa na magari kwa kipindi kirefu. Huu mpango ulisukwa na pia walijua wanaemtaka hadi kumfuata mpaka nyumbani kwake. Sidhani hii ilikuwa ni Random Act. Dhana hii ni potofu.
2. Raia wenye chuki na Lissu kwa kuikalia kooni serikali.
Hii inawezekana kabisa. Wengi walimshutumu Lissu kwa kupinga sera zote za serikali (mimi nikiwa mmojawao). Kuna watu walikwenda mbali zaidi na kusema wanataka serikali iwaruhusu wamuue. Ndio maana kuna umuhimu wa kuwakamata na kuwafikisha mahakamani watu hawa.
Katika demokrasia watu tunashambuliana vikali kwa hoja na sio kwa kuumizana au kuuana. Kama hii itathibitika, basi kuna umuhimu wa kuwapatia ulinzi wanasiasa machachari wanaoibua hisia kali.
Kuna uwezekano mkubwa dhana hii ni sahihi.
3. Serikali yenyewe
Kuna watu mitandaoni wanadhani ni serikali yenyewe ndio imeunda hii mbinu ya kumuua Lissu ili awaondolee kelele. Wengi wanasema Lissu amefichua siri nyingi za serikali kufikia kuwa tishio kwa hii serikali.
Kwa maoni yangu huu ni upuuzi. Serikali hii inakubaliwa na watanzania wengi. Hoja karibuni zote alizotoa Lissu dhidi ya serikali zinaweza kujibiwa kirahisi sana. In fact, baadhi ya shutuma za Lissu zinaipaisha serikali kwa Watanzania. Kelele za Lissu zinaweza kuwa baraka (blessing) kwa CCM ifikapo 2020. Kumuua Lissu kutajenga hisia za uonevu na kuwaonea huruma CDM ifikapo uchaguzi mkuu. Serikali haiwezi kufanya kosa hilo.
Kwa hiyo dhana hii ni potofu
4. Watu wenye chuki na serikali (false-flag attack) ili waisingizie serikali uovu huu.
Hii dhana inahusisha watu wanaoichukia serikali (sio lazima wapinzani, inaweza kuwa watu wa nje) wanaotaka kumuondoa Rais Magufuli madarakani ifikapo 2020 kwa kuihusisha serikali yake na mauaji ya Lissu.
Serikali ya Magufuli imeathiri maslahi ya watu wengi sana wa ndani na wa nje. Akiendelea hivi hivi ana uhakika kabisa wa kupita ifikapo 2020. Sasa utaitoaje hii serikali madarakani ifikapo 2020. Jenga chuki kwayo.
Kama nilivyoeleza kwenye dhana namba 3, watu wakiamini kuwa serikali imemuua Lissu kinyama basi watawaonea huruma CDM na kuichukia CCM. CDM watachukua dola ifikapo 2020.
Je ni nani hawa wanaotaka kufanya unyama kama huu na kuisingizia serikali ya CCM (false-flag attack)?
Nina dhana nyingine 2 au 3 hivi (mfano, internal politics within CDM) lakini ni za pembeni sana na uwezekano wake ni karibu na sifuri. Kwa sasa hayo ndio malumbano yanayoendelea kichwani mwangu.
Please tell me I am not crazy.
==============================
Baada ya michango mingi iliyowekwa hapa kuna dhana niliyoigusia tu (Internal politics within CDM) na wengi kuuliza kwa nini sikuifafanua. Hapa chini naiongeza ingawaje mwanzoni sikuipa kipaumbele.
Dhana ya 5.
Maadui wa ndani wa CDM walitaka kumuua Lissu ili watimize malengo 3 yafuatayo.
1. Lissu aondoe ushindani katika uchaguzi ujao wa mwenyekiti.
2. Lissu aondoe ushindani katika uteuzi ujao wa mgombea uraisi ifikapo 2020.
3. Lissu atumiwe kama kafara ili kuipa CDM mvuto wa kuonewa huruma na kuichukia serikali katika uchaguzi wa 2020.
Nimeweka maoni yangu kama chachu na sio neno la mwisho.Uchambuzi wako ni wa kisiasa zaidi, mojakwamoja umeegemea upande wawashika dola, kifupi hujachambua ila umekuja kutudhihirishia unasema nini, kwanz umeonesha ni mwanasiasa moja kwa moja tena wa
Polisi ndiyo wanatumika kuwabambikia kesi chadema kila siku nani aombe Ulinzi wao?Inawezekana ni kweli hakwenda polisi kuomba ulinzi, badala yake akaitisha press conference na kijipigia debe la kisiasa.
mada ndefu huwa ngumu wengi kuzisoma, kwa kifupi tambua kuwa serikali hii ya kibabe kidikteta huwa haipendi kukosolewa ama kuonyeshwa udhaifu wake wa kiutendaji imekuwa ikimunyanyasa Lisu kupitia Polisiccm pindi akiwakosoa kila mtanzania analijua hilo.Nimeweka maoni yangu kama chachu na sio neno la mwisho.
Lengo hapa ni kuwa watu kama wewe mje mkosoe au muunge mkono maoni yangu. Lakini hasa nilitegemea wachambuzi walete dhana mbadala na kuelezea kwa nini wanafikiria dhana zao zina mashiko. Hii ndio ilikuwa dhamira ya bandiko langu.
Kwa mfano, sikuitetea serikali katika dhana no.3 bali nimeeleza sababu zangu kwa nini nilifikiri dhana ile ni potofu. Nilitegemea mtu mwengine aje atoe mdahalo wake unaoelezea kwa nini serikali ilitaka kumuua Lissu.
Mijadala ya Great-Thinkers ndivyo inavyoendeshwa hivi. Ni malumbano na kila mmoja anatoa hoja zake. Mimi nikisema hoja hii ndio sahihi ni lazima nitoe maelezo ya kuwashawishi wengine. Asiekubaliana na mimi nae anakuja na hoja zake mbadala mpaka tunakubaliana au tunakubaliana kutokukubaliana.
Samahani kama ulifikiri mimi ndie mwenye majibu yote. Ningemjua aliefanya unyama huu ningekimbilia polisi badala ya kuja JF.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi sina chama bali ninaunga mkono juhudi za serikali hii. Hapo nyuma nilimshambulia sana Lissu kwa hoja zake potofu dhidi ya serikali hii. Hoja zote za Lissu dhidi ya serikali hii ni nyepesi sana na zinajibika kirahisi. Serikali haina haja ya kumuua kwa sababu hana hoja nzito. Nitarudia tena hapa:Serikali hii haipendwi na watanzania bali watu wanaidshi kwa Uoga wanaogopa visasi kukomoana kubambikiana kesi, serikali ya CCM hawajawahi kujibu hoja kwa hoja za Lisu bali hutumia polisiccm kumtisha kumnyanyasa kumsachi nyumbani kwake, kutaka kumpima mkojo ili abambikiwe kesi za unga nk, nyie CCM na serikali yenu humukuwa mkifahamu watanzania wanampenda Lisu kiasi hiki, mlidhani Lisu hana watu lakini baada ya jaribio la kumuua kukwama mmetambua kuwa wapo watanzania wengi pamoja na mataifa mengi yanamuunga mkono na huko kenya anapotibiwa amepewa Ulinzi mkubwa na matibabu bora chini ya uangalizi mkubwa sana, kwa taarifa yako ingawa umekuja na story ndefu sana mtuhumiwa namba mija ni Bashite, Le mutuz na wenzako kadhaa hilo halina ubishi na wananchi wengi ndivyo wanajua.
Ni ukosoaji gani wa Lissu kwa serikali unaotaka niuelezee kwa nini haukufuatwa. Lete hapa.mada ndefu huwa ngumu wengi kuzisoma, kwa kifupi tambua kuwa serikali hii ya kibabe kidikteta huwa haipendi kukosolewa ama kuonyeshwa udhaifu wake wa kiutendaji imekuwa ikimunyanyasa Lisu kupitia Polisiccm pindi akiwakosoa kila mtanzania analijua hilo.
Hoja zipo nyingi na si nyepesi hivyo labda ujibu kwa kudhani unavyofikiri ndilo jibu, Zipo wapi zile bilion 251 zilipotea wizara ya ujenzi kwa kuwalipa makandarasi hewa? Vipo wapi vyeti vya Bashite mshauri mkuu wa Mtukufu? Yupo wapi Ben sanane aliyehoji PhD feki ya mtukufu, ? Ujenzi wa uwanja wa ndege chato, ununuzi wa ndege kwa cash vilibalikiwa na Bunge? Tenda za ununuzi na ujenzi zilitangazwa wapi? Na bei ya ndege ni bei halisi? Zipo wapi zile nyumba za serikali alizojiuzia Mtukufu akagawa kwa mdogo wake na ingine kwa hawala yake ambao hawakuwa watumishi wa umma? Nakupa hayo machche kwanza maana Hoja ni nyingi na maswali ni mengi sana.Mimi sina chama bali ninaunga mkono juhudi za serikali hii. Hapo nyuma nilimshambulia sana Lissu kwa hoja zake potofu dhidi ya serikali hii. Hoja zote za Lissu dhidi ya serikali hii ni nyepesi sana na zinajibika kirahisi. Serikali haina haja ya kumuua kwa sababu hana hoja nzito. Nitarudia tena hapa:
Lete hoja yoyote ile ya Lissu dhidi ya serikali hii na nitaijibu hapa, sasa hivi.
Na kwa taarifa yako mimi sio msemaji au muajiriwa wa serikali.
Sent using Jamii Forums mobile app
tokea 1998 lisu alipiga kelele juu ya mikataba mibovu ya uwekaji na Mtukufu alikuwa waziri kipindi hicho na wabunge wa CCM wakapitisha mikataba hiyo leo hii Mtukufu anajidai kupiga kelele kana kwamba hakuwa sehemu ya waliopitisha mikataba mibovu.Ni ukosoaji gani wa Lissu kwa serikali unaotaka niuelezee kwa nini haukufuatwa. Lete hapa.
Sent using Jamii Forums mobile app