Ni sababu ipi muhimu sisi wazazi tunakuwa na mtoto zaidi ya mmoja?

Inaweza kujirudia watu wakaanza kuishi mamia ya miaka kama wa kwenye Biblia[emoji1787], labda miaka 900 hivi kama kina Methuselah wa Biblia.
Kwa siku hizi utaambiwa kutaka kuishi miaka mingi sana ni ubinafsi na uharibifu wa mazingira.

Kutapitishwa azimio la Umoja wa Mataifa ku regulate miaka ya watu kuishi na kuweka limit.

Ukitaka kuishi zaidi ya miaka fulani mingi sana unapelekwa huko dark side of the moon uende kuwa sample katika some government experiment 🤣🤣🤣.
 
Ukisoma SoMo la biology, baadhi ya topic kama ecology, genetics, reproduction utagundua dhumuni moja wapo la kuzaa ni kuhakikisha gene(kizazi) chako kinaendelea ku exist miaka yote duniani. Sasa chance ya kizazi/gene za kizazi chako kuendelea ku exist ni kuwa na idadi kubwa ya watoto kuongeza chance ya kizazi chako kuexist duniani. Wewe jiulize swali mama yako mzazi Yuko above 70years anataman umzalie wajukuu Tena wakati mwingine ukiwa na mmoja anapambana upate na wengine.
 
Sababu zipi zilikufanya uhitaji kupata mtoto huyo uliyenaye?
 
Hiyo ina maana kwamba, kuzaa sana ni ishara ya ujinga na umasikini.
 
Mpango wa Elon Musk kuwafanya binadamu waishi sayari nyingine ni mzuri labda na overambitious pia kwa karne hii, ila utakuwa msingi mzuri kwa vizazi vijavyo kumfanya binadamu kuwa "multiplanetary species".

Mimi naona bora hizo dola zake kwa sasa angezipeleka zaidi kuboresha mazingira ya hapa duniani ya sasa kupitia teknolojia za kuboresha mazingira, dunia iachane na fossil fuels kabisa, ipambane na njaa, kansa, uzee, ajali n.k lakini yeye inaonekana haya kwake sio kipaumbele zaidi ya binadamu kwenda Mars.
 
Hiyo ina maana kwamba, kuzaa sana ni ishara ya ujinga na umasikini.
Hahaa,

Mkuu sasa unataka kuniingiza kwenye matatizo ya kuwanyanyapaa rafiki zangu wenye watoto wengi, ambao wametumia turufu yao kwa haki zao kabisa, za kikatiba na kiutu.

Hiki suala ni tata sana kwa sababu wakati kuna watu wanasema kuzaa sana ni chanzo kikubwa kabisa cha uharibifu wa mazingira, na kunazuia maendeleo ya kiuchumi, kuna wengine pia wanaosema kuwa dunia inakabiliwa na tatizo la watu kutozaa vya kutosha.

Kwa hakika tunaona nchi zilizoendelea kiuchumi na kielimu watu wanapunguza idadi ya watoto. Korea ya Kusini ni mfano mmoja tu, lakini kuna nchi nyingi za Ulaya zina birth rates ndogo.

Kwa hesabu za United Nations Population Division za mwaka 2015 mpaka 2020 nchi za Afrika zilikuwa na average ya 4.4 fertility rate, Asia 2.2, Europe 1.6, Latin America and the Caribbean 2.0, North America 1.8, Oceania 2.4

Unaweza kusema kuwa nchi zenye umasikini na ujinga zaidi zina fertility rate kubwa zaidi.

Kwa hivyo, inawezekana pia nchi fulani zikawa zinahitaji kuongeza uzazi, na nchi nyingine zikawa zinahitaji kupunguza uzazi ili ki balance.

Unaweza kuangakia namba na kujua nani anahitaji kuongeza na nani anahitaji kupunguza.
 
Sawa,

Sasa Elon si anaweza kukuambia kuwa kashawekeza kwenye Tesla, gari la kuanza kutumia umeme, kuhusu hayo mambo ya mazingira, kwamba anaweza kufanya mambo mawili kwa wakati mmoja.
 
🙏🙏
 
Kwa mantiki hiyo hupendi dunia kuendelea kuwa na watu as per your satisfaction with only one kid.

NB; assuming that the rest of the earth will be satisfied with only one child as well.

And my question is "kwanini hupendi dunia iendelee kuwa na watu?"
 
IQ kubwa
 
Hapana,

Again, nakujibu kwa sababu umeniuliza, sina nia ya kumnyanyapaa yeyote. Maamuzi ya kuzaa au kutozaa vyovyote ni ya mtu binafsi, ni haki za kikatiba na kibinadamu.

But kuna vitu nafikiri kuwa ni kweli, mimi binafsi, kwa kuangalia facts and figures.

Kwa sasa dunia inaweza kufikia extinction level event kwa watu kuzaliana zaidi kuliko kwa watu kupunguza kuzaa.

Ukiangalia hesabu za carbon emission na global warming na mambo mengi ya mazingira, na ukweli kwamba the single biggest contributor ni idadi ya watu, ni wazi kwamba, kwa sasa, msisitizo hapo ni "kwa sasa", kuongeza watu duniani kunaweza kuleta madhara makubwa sana kuliko kupunguza watu kwa sasa.

Kuna level ambayo tukiifikia kupunguza watu kutakuwa ni hatari, lakini hatujaifikia sasa na iko mbali sana bado.

Yani kuna happy medium figure ya average fertility rate tunatakiwa kuifikia, hatujaifikia, mimi nasaidia dunia iifikie hiyo figure.
 
Shida inakuja kwamba, wanaotakiwa kuongeza hawahitaji, na wanaotakiwa kupunguza ndio wanazidi kufyatua watoto.

Mtu hana kitu kabisa lakini anazaa watoto kibao kama ngedere, imagine ofa ya pesa ingetolewa bongo ingekuwaje.
 
Shida inakuja kwamba, wanaotakiwa kuongeza hawahitaji, na wanaotakiwa kupunguza ndio wanazidi kufyatua watoto.

Mtu hana kitu kabisa lakini anazaa watoto kibao kama ngedere, imagine ofa ya pesa ingetolewa bongo ingekuwaje.
Mkuu Korea Kusini huko kuna kampuni ya ujenzi imetoa ofa ya US $ 75,000 kwa wafanya kazi wake kwa kila mtoto aliyezaliwa katika miaka miwili iliyopita na kila ntoto atakayezaliwa.

Vipi kampuni ya Bongo ikitoa ofa hiyo?
 

Asante kwa ufafanuzi mzuri.

Why umeamua kuchukua part ya kusaidi ili wanadamu tufikie hiyo figure.? Au ndio Uhuru?
 
Mkuu Korea Kusini huko kuna kampuni ya ujenzi imetoa ofa ya US $ 75,000 kwa wafanya kazi wake kwa kila mtoto aliyezaliwa katika miaka miwili iliyopita na kila ntoto atakayezaliwa.

Vipi kampuni ya Bongo ikitoa ofa hiyo?
Nahisi inaweza ikawa maangamizi, mass destruction.
 
Asante kwa ufafanuzi mzuri.

Why umeamua kuchukua part ya kusaidi ili wanadamu tufikie hiyo figure.? Au ndio Uhuru?
Kila mtu ana wajibu wa kuitunza dunia ili si tu iendelee kuwapo kwa vizazi vijavyo, bali pia iwe na mazingira bora. Pengine hata mazingira bora zaidi ya yaliyopo sasa.

Kama mimi nilivyoikuta dunia haijaharibiwa na walioniachia, na mimi nataka niwaachie wengine dunia ambayo sijachangia kuiharibu sana. It's only reasonable for any person who is not overly selfish.

Ni kama vile nimepewa switch ya kuchangia kuilipua dunia kwa kiasi fulani kidogo, nikaambiwa unaweza kuibonyeza switch hii na kupata personal glory ya kuwa na watoto wengi, ukaiharibu dunia kwa watoto wa watoto wa watoto wa watoto wao, au unaweza ukakataa kubonyeza switch hiyo, na kuwa na mtoto mmoja.

Uamuzi wangu wa kuwa na mtoto mmoja umekuwa rahisi zaidi kwa sababu mimi, kinyume na watu wengi, sioni kuwa na watoto wengi kuwa ni jambo la fahari.

I am more about quality of life ninayompa mtoto mmoja kuliko quantity of life ya kuwa na watoto wengi.

Na pia, kwa watu ambao tunatoka familia ambazo tayari zina utamaduni wa kuzaa watoto wengi, kuna watoto wengi sana wa familia wanahitaji kulelewa, na watoto hao wanakua kwenye umasikini na kuwa watu wazima tegemezi, tunaweza kuanza kusaidiana kuumaliza au kuupunguza umasikini kwa watu waliopo kwanza, kabla ya kuongeza watu wengine wengi tu ambao tunaweza ku struggle kuwapa maisha mazuri.
 
Nakushauri usome post no 25.
 
Mkuu, ukiondoka; mali unazoziacha sio zako tena... ni za warithi/ uliowaacha hai.

Wao ndio watajua wanaziangaliaje, kama wakizinywea bia au wakiamua tu kuzitom#bea hadi ziishe wewe haikuhusu kabisa! [emoji41][emoji23]
Umejibu kwa ufasaha kabisa.
 
Shida inakuja kwamba, wanaotakiwa kuongeza hawahitaji, na wanaotakiwa kupunguza ndio wanazidi kufyatua watoto.

Mtu hana kitu kabisa lakini anazaa watoto kibao kama ngedere, imagine ofa ya pesa ingetolewa bongo ingekuwaje.
Suala kubwa hapa ni kipato, elimu, utamaduni, dini na mfumo wa maisha.

Kuhusu Kipato ni kama ambavyo utaona malofa wengi mfano hata jukwaani tu hoja kuu ya kuwa na watoto wengi ni ili wasaidiwe uzeeni.

Kuhusu elimu watu wengi wanaosoma muda mrefu huwa wanapata fursa ya kujifunza maisha ya binadamu wengine na kupuuza nyingi ya tamaduni au dini zao.

Mfumo wa maisha pia nao una mchango wake, mfano kama nchi sehemu kubwa ya raia wake wanafanya kazi za misimu, hawana umeme au ni watu kidini sana lazima utegeeme watazaana kwa kasi sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…