Hance Mtanashati
JF-Expert Member
- Sep 7, 2016
- 20,137
- 26,189
Kuwa na mtoto zaidi ya mmoja sababu ni hizi;Habari za muda huu ndugu zangu. Nimekaa, nikafikiria, Mimi ni mzazi wa mtoto mmoja wa kike.
Sasa issue kubwa nataka kufahamu nimeona kama nimeridhika au sina sababu maalumu ya kuongeza mtoto. Najiweza sana kiuchumi, mimi kijana mdogo ila mwanangu yupo anaishi na mama yake Uingereza (Mama mtanzania age 27) nilimpeleka mwenyewe. Anajiweza. Na pia sipo nae kimahusiano kwa sasa ila nina mtunza huyu binti.
(Nia nikutoa point za uchumi na uhusiano). Sasa sina Wazo lolote la kuongeza mtoto, yaani nina mapenzi yaliyopitiliza kwa huyu niliye nae.
Wazee sababu ipi inafanya mtu awe na watoto zaidi ya mmoja au wengine kupitiliza hadi watano. Nini sababu?
Au huwaga ni bahati mbaya tu, mimba hiyo?
1)Agizo kutoka kwa M/Mungu i.e Zaeni muongezeke mkaijaze dunia.
2)Unapanua ukoo/ jina.
3)Ukiwajengea msingi imara wa upendo watasaidiana wao kwa wao kuliko ukikazaa kamoja halafu ukafariki.
4)Ni raha kuwa na watoto angalau watatu au wanne na wawe jinsia tofauti (Ke na Me).Ke atabeba majukumu ya mama na Me atabeba majukumu ya baba.